Chuo Kikuu Kampala kinawatesa Watanzania

Chuo Kikuu Kampala kinawatesa Watanzania

bne

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2016
Posts
1,679
Reaction score
2,016
1718997769811.png

Chuo kikuu cha Kampala tawi la Tanzania kimekuwa na tabia ya kuwatesa watanzania wanaosoma kozi mbalimbali hapo chuoni kwa kuwawekea mazingira magumu hasa inapofika nyakati za mitihani ili washindwe kufanya mitihani na badala yake wafanye mitihani ya marudio ambayo inalipiwa bei ghali sana.

Baadhi ya wanachuo wanaosoma ktk chuo hicho wameulalamikia utawala wa chuo hicho kwa kufanya matendo hayo ambayo yanawaumiza sana.

Mwanachuo mmoja ambae alionekana amechanganyikiwa alisema amezuiwa kufanya mtihani wa mwisho sababu tu eti anadaiwa hela za kulipia mtihani wa suppliment.

' Yaani nashangaa nimelipa ada yote ya chuo lakini naambiwa sitaweza kufanya mtihani wa mwisho kisa eti nadaiwa ada ya suppliment, kama nimeweza kulipa ada yote ya mamilioni nashindwaje kulipa ada ya suppliment kwa baadae?", aliuliza mwanachuo huyo. " "Kwa kawaida wanapaswa kuniruhusu nifanye mtihani wangu wa mwisho lakini wazuie cheti changu hadi hapo nitakapolipa hela hiyo ya suppliment "

Wanachuo hao wameuomba uongozi wa chuo kurekebisha hali hiyo na pia kuiomba mamlaka husika kutupia Jicho malalamiko hayo la watanzania wengi wataendelea kuumia.

PIA SOMA

- Kamwe USIJARIBU kusoma Chuo cha Kampala Dar es Salaam

- DOKEZO - Chuo Kikuu cha Kampala chini Tanzania kinawadhulumu wafanyakazi wake
 
Sasa kama kweli unadaiwa si ulipe yaani unampangia anayekudai ulipe lini, yaani umalize chuo ndo uje uchukue cheti na ukifa je.Lipeni hela za watu , elimu ni gharama
 
Sasa kama kweli unadaiwa si ulipe yaani unampangia anayekudai ulipe lini, yaani umalize chuo ndo uje uchukue cheti na ukifa je.Lipeni hela za watu , elimu ni gharama
Mambo ya kumzuwia mtu kufanya mtihani kisa hakulipa ada,mzee mkapa aliyapiga marufuku 1999,zuwia cheti,si Kuna clearance form mwisho wa siku kabla ya kupewa vyeti?
 
Mambo ya kumzuwia mtu kufanya mtihani kisa hakulipa ada,mzee mkapa aliyapiga marufuku 1999,zuwia cheti,si Kuna clearance form mwisho wa siku kabla ya kupewa vyeti?
Katafute chuo cha mkapa ukasome usiwapangie watu.Wafanyakazi wa chuo hicho na huduma zingine zinategemea ada za wanafunzi.

Ningekubali kuwa wananyanyaswa kama wakati wa mtihani wanabambikiwa vitu na kuwasingizia kuwa wamefanya udanganyifu, nk.

Ada na malipo mengine kamilisha hakuna mjadala.Tumeona hata wanafunzi wa UDSM wakikaziwa kulipa ada.Lipa ada, Kampala university kazia Uzi hapo hapo na hata wale wanaodaiwa elfu 10 wakaziwe hadi wakamilishe deni
 
  • Kicheko
Reactions: apk
Mambo ya kumzuwia mtu kufanya mtihani kisa hakulipa ada,mzee mkapa aliyapiga marufuku 1999,zuwia cheti,si Kuna clearance form mwisho wa siku kabla ya kupewa vyeti?
Mada inasema Kampala wewe unaongelea Mkapa.
 
  • Thanks
Reactions: apk
Katafute chuo cha mkapa ukasome usiwapangie watu.Wafanyakazi wa chuo hicho na huduma zingine zinategemea ada za wanafunzi.Ningekubali kuwa wananyanyaswa kama wakati wa mtihani wanabambikiwa vitu na kuwasingizia kuwa wamefanya udanganyifu, nk.Ada na malipo mengine kamilisha hakuna mjadala.Tumeona hata wanafunzi wa UDSM wakikaziwa kulipa ada.Lipa ada, Kampala university kazia Uzi hapo hapo na hata wale wanaodaiwa elfu 10 wakaziwe hadi wakamilishe deni
Kuna sheria za nchi husika,Kama unataka kufanya mambo utakavyo kafanye kwenu
 
Chuo kikuu cha Kampala tawi la Tanzania kimekuwa na tabia ya kuwatesa watanzania wanaosoma kozi mbalimbali hapo chuoni kwa kuwawekea mazingira magumu...
Kwani ada ya supplementary aijafutwa vyuo vote?
 
Halafu iweje pawe na ada ya supplementary?..nilisup sikumbuki kulipa ada ya kusapua
 
Hao mwaka 2014 au 2015 kama sijakosea walikula ada za wadogo zangu wa kike hapo , walilipia kozi wakaja kuambiwa imefutwa na ada hawajapewa mpaka leo nawaona kama scammer tu.
 
  • Thanks
Reactions: bne
Unapataje sup chuo cha mtaa kama hicho, ambacho lengo mama ni kutafuta ada na michango ili kijiendeshe?.

Ungesoma UDSM, UDOM, SUA au MZUMBE unge-disco semister ya kwanza tu.

Acheni anasa zisizo na msingi, someni kwa bidii hayo mengine unajikuta umeyaepuka kirahisi.

Kampala kazeni hivyo hivyo, mliwekeza ili mpate faida na siyo kutoa msaada au kuonea huruma vijana wasiopenda kujituma
 
Mnasomaje vyuo vya uchochoroni hivyo ambayo hata kujulikana duniani havijulikani?
 
Angekua anadaiwa ada ni sawa lkn ada ya kozi nzima kaishalipa yote. Anachodaiwa ni hela za supp. Je ni halali?
Kama ndo utaratibu wa chuo alipe tu hakuna janja janja kwenye elimu.
 
Back
Top Bottom