Chura wa Kihansi na safari ya Marekani

Chura wa Kihansi na safari ya Marekani

John Joba kwa kipindi kile walipohamishiwa USA, hapa Tz wataalamu wetu hawakuwa na capacity ya kuwalea na kuwakuza hao vyura.

Ukumbuke walitoka 'porini' na hakuna aliyekuwa anajua aina ya vyakula au mahitaji yao yalikuwa kivipi. Hata hao wa Toledo na Bronx walifanya kazi kubwa sana na utafiti kuweza kudocument taarifa zao, na kuna kipindi walibakia 72 tu katika captive facility yao. Tim Hermann aliandika papers kuhusu utunzaji wa vyura hawa.

Hata hivyo NEMC kwa kushirikiana na UDSM na SUA walijenga uwezo wa wataalamu wa nchi hii kuweza kuwatunza, kuwaendeleza na kuwarudisha porini kwenye makazi yao ya asili.
Nashukuru kwa ufafanuzi..kwa kuongeza tu ni kuwa wakati wale vyura wako Marekani tafii ziliendelea kwa kiasi kikubwa sana huku Tanzania juu ya chanzo hasa cha kupungua kwao kule porini. Hawa chura kule kiasi walikuwa wanapatikana katika bonde moja tu na moja ya mahitaji yao ya mazingira ni "wetness ya eneo lao", watu wa lower Kihansi wakaweka spray ili kuwawekea huo unyevu lakini bado walitoweka, na baadae ikagundulika pia wanashambuliwa sana na fungus, na ikabidi liwekwe sharti la "kuosha" viatu kwa kukanyaga dawa ukiwa unapanda kule mlimani. Badaa ya hapo UDSM walipeleka Mtaalam pale Brox Zoo na baada ya ghrama za kuwatunza kuwa kubwa na kuonesha uwezo wa kuzaa vizuri wakiwa in captivity ndio, serikali ya Tanzania kwa ushirikiano na World bank wanakubaliana kujenga maabara ya kuwatunza pale UDSM na kule Kihansi. Ila kwa sasa idadi kubwa iko Kihansi chini ya uangalizi wa Tawiri.
 
Kitu nilichojifunza kwa Wazungu (White people) jambo linaweza likawa simple and clear, lakini wao wakalifanya lionekane ni jambo gumu sana kutekelezeka with alot of complications.
Lengo kuu ni hili ukubali mawazo yao na ideology yao kwenye jambo lao na hatimaye kufanikisha mipango yao juu ya jambo lao.

Nipende kunukuu kidogo moja kati ya sentesi yako bitimkongwe ''Ukumbuke walitoka 'porini' na hakuna aliyekuwa anajua aina ya vyakula au mahitaji yao yalikuwa kivipi''.

Je, walishindwa kujua aina ya chakula chao na mahitaji yao?

Tuna wataalam wengi tu wenye Intellectual ability ya Wildlife Conservation, Environment Science pamoja na Forest Conservation.
Kama wanyama kama Simba, Chui, Duma, Paka mwitu na Fisi (ni wanyama walao nyama - Carnivorus) na ukitaka kujua mahitaji yao lazima ufanye utafiti katika ecosystem yao.
Most of Class Amphibians (Vyura) ni wanyama walao wadudu - (Insectivorus) na ukitaka kujua mahitaji yao lazima ujue ecosystem yao - Interaction between biotic and abiotic components around they are surrounding.

Nafikiri changamoto kubwa kwetu ingekuwa Technological Factor (Well Equiped Instruments for Restoration) lakini nyingine ni possible zinawezekana.

So nafikiri kila jambo ni uthubutu tu ukiamini unaliweza na itakuwa hivyo, ukiamini you are not well prepared to tackle that kind of challenge na itakuwa hivyo hivyo pia.

That's why ''Fortune favours the Brave''
 
Most of Class Amphibians (Vyura) ni wanyama walao wadudu - (Insectivorus) na ukitaka kujua mahitaji yao lazima ujue ecosystem yao - Interaction between biotic and abiotic components around they are surrounding
Easier said than done. Na wala siyo kuwa nadharau utaalamu wa wanasayansi wetu, lakini vitu kama mahitaji yao maalumu kwenye ecoystem yao (mfano, ule unyevu) vilikuwa havikueleweka hapo awali. Hata hizo fedha za kugharamia huo utafiti wa awali zisingetolewa na serikali kwa ajili ya chura. Ungeambiwa hiyo siyo kipaumbele.
 
Easier said than done. Na wala siyo kuwa nadharau utaalamu wa wanasayansi wetu, lakini vitu kama mahitaji yao maalumu kwenye ecoystem yao (mfano, ule unyevu) vilikuwa havikueleweka hapo awali. Hata hizo fedha za kugharamia huo utafiti wa awali zisingetolewa na serikali kwa ajili ya chura. Ungeambiwa hiyo siyo kipaumbele.
Tumeaminishwa hivyo na itaendelea kuwa hivyo?

Tatizo kidogo tunaomba misaada kwa wenzetu ambao na wao pia wanachangamoto zao kwa sababu nobody is free from problem.

Hakuna cha bure in this world of Capitalism, chochote wanachokifanya kwa ajili yetu sio kwa ajili yetu bali ni kwa ajili yao. Kwa sababu super power anataka aendelee kuwa super power na sisi Kama Third world Country we must pay that price.
 
Easier said than done. Na wala siyo kuwa nadharau utaalamu wa wanasayansi wetu, lakini vitu kama mahitaji yao maalumu kwenye ecoystem yao (mfano, ule unyevu) vilikuwa havikueleweka hapo awali. Hata hizo fedha za kugharamia huo utafiti wa awali zisingetolewa na serikali kwa ajili ya chura. Ungeambiwa hiyo siyo kipaumbele.
Bitimkongwe kwa sasa serikali inagharamia hawa chura kwa kiasi kikubwa sana, wanatumia umeme 24/7, kuna siku umeme ulikatika katika maabara yao pale Kihansi kwa sababu jenerata wanalotumia lilileta shida, ilibidi jenereta ya dharura ikimbizwe kule kutoka Morogoro mjini...kwa agizo la serikali!
 
CHURA WA KIHANSI
  • Taxonomy
[emoji117]Kingdom⟹ Animalia
[emoji117]Phylum ⟹ Chordata
[emoji117]Class ⟹ Amphibia
[emoji117]Order ⟹ Anura
[emoji117]Family ⟹ Bufonidae

Vyura wa kihansi kwa jina la kisayansi wanajulikana kama "Nectophrynoides asperginis" ni aina ya vyura wadogo ambao wanapitikana Tanzania tu, katika mkoa wa Iringa kwenye bonde la mto Kihansi na chakula chao ni wadudu (insectivorus). Chura wa kihansi ni chura pekee katika jamii ya vyura waliopo duniani kwa sababu vyura hawa hutaga mayai na kukaa nayo kwenye kifuko kilichopo ndani ya chura mwenyewe hadi muda wa kuanguliwa unapofika na ndipo hutoa vitoto hai.Kwa lugha rahisi ni kwamba Chura hawa huzaa kwa sababu hatagi mayai yakaonekana bali hukaa ndani ya chura mwenyewe.

IUCN (International Union For Conservation of Nature) walifanya utafiti na kugundua kuwa vyura wa kihansi wapo kwenye hatari kubwa ya kutoweka (Extinct in the wild). Awali uharibifu wa makazi yao ya asili uliotokana na utengenezaji wa bwawa la Kihansi kwa ajili ya kuzalisha umeme ulionza mwaka 1995 na kukamilika mwaka 2000 na kupelekea kupungua kwa kiasi kikubwa cha maji kwa asilimia 90 ambacho kilikua kinatiririka kutoka kwenye maporomoka ya bonde la mto kihansi. Lakini taarifa nyingine za waatalamu zinataja kuwa sababu za kutoweka kwao huenda zilisababishwa na utumiaji wa mbolea za kikemikali (artificial fertilizer) katika vyanzo vya maji yanayotiririka katika mto huo. Huku pia huwepo wa aina fulani ya fungus wanaojulikana kama chytrid. Hata hivyo mradi huo wa umeme ulisababisha uharibufu wa makazi yao ya asili na kusababisha kukosekana kwa unyevu nyevu wa kutosha na kupungua kwa mimea katika bonde hilo.

Matokeo ya uchunguzi wa IUCN kwa kutumia miongozo ya "IUCN RED LIST CATEGORIES AND CRITERIA":-
2004→ Critically Endangered (CR)
2006→ Critically Endangered (CR)
2009→ Extinct in the wild (EW)



Vyura wa kihansi kutokana na uharibifu wa makazi yao ya asili. Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wadau wengine wa mazingira kama vile World Conservation Society na Benki kuu ya Dunia walianzisha project ambapo takribani vyura 500 walichukuliwa na kupelekwa Marekani kwa ajili ya kuhifadhiwa na kuongeza idadi yao hili kuzuia athari ya kutoweka duniani, waligawanywa na kuhifadhiwa katika Zoo sita huko Marekani. Bronx Zoo na Toledo Zoo ndizo ambazo ziliweza kuwahifadhi na kufanikiwa kuongeza idadi yao. Maonyesho ya kwanza ya Vyura wa Kihansi nchini Marekani yalifanyika katika Toledo zoo mwaka 2005. August mwaka 2010 kundi kubwa la vyura wa kihansi walisafirishwa kutoka Bronx Zoo na Toledo Zoo mpaka Tanzania na kuhifadhiwa katika chuo kikuu cha Dar-es-salaam kwa ajili ya uzalishaji na kuongeza idadi yao kabla ya kurudishwa katika makazi yao ya asili.

1. Je, wewe kama mdau wa mazingira na maliasili za nchi ya yako, je kulikuwa kuna ulazima wa vyura hawa kusafirishwa na kupelekwa nchini Marekani na wakati Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam kulikuwa na maabara ambayo ingeweza kuongeza idadi yao kama walivyofanikiwa kuongeza idadi hiyo na kuwarudisha katika makazi yao ya asili?
2. Na bado tunaendelea kusema ni vyura pekee wanaopatikana Tanzania tu, kama nilivyotype mwanzoni mwa uzi huu. Kama waligawanywa katika Zoo 6 nchini Marekani na Zoo 2 tu kati ya hizo 6 ndizo zilifanikiwa kuongeza idadi yao. Kwa nini hizo zoo 4 zilizobaki walishindwa kuongeza idadi yao maradufu?
3. Je, wasomi wetu wa wildlife management wa SUA, MWEKA na UDSM walishindwa wapi kuhusiana na uhifadhi na uzalishaji wa vyura hawa na kupelekea kusafirishwa mpaka nchini Marekani?
4. Je, kama ni issue ya teknolojia na vifaa vya uhifadhi na uzalishaji wa vyura hao, walishindwa kuviinstall hapa hapa katika maabara zetu na kupunguza usumbufu na gharama za usafirishaji wa vyura hao?

Namalizia kwa kusema kwamba Wazungu sio wajinga hata kidogo.
Utakuta Sasa Marekani ndo itakuwa inaongiza kwa kuwa nao wengi
 
Sasa huko Marekani hawapo maana nao waliwaona Tanzania kwa mara ya kwanza,huo utaalami wa kutunza waliupata wapi? Hapa ni uhakika kwamba tulipigwa.
 
Sasa huko Marekani hawapo maana nao waliwaona Tanzania kwa mara ya kwanza,huo utaalami wa kutunza waliupata wapi? Hapa ni uhakika kwamba tulipigwa.
Haikuwa rahisi....waliwatengenezea artificial environment maabara na ilikuwa kama trial and error, walikufa sana kipindi cha mwanzo na ilichukua muda hadi walipoanza kuzaliana huko maabara
 
KIHANSI FROG ARTICLE

The Dynamics of Re-introduced Kihansi Spray Toad Nectophrynoides asperginis and other Amphibians in Kihansi Gorge, Udzungwa Mountains, Tanzania

Wilirk Ngalason, Cuthbert L Nahonyo and Charles A Msuya.
Department of Zoology and Wildlife Conservation
,
University of Dar es Salaam,
P. O. Box 35064, Dar es Salaam,
Tanzania.
Corresponding author, e-mail: wilirk@udsm.ac.tz
 

Attachments

Nilisikiaga hao vyura wakihamishwa eneo lao wanaloishi wanaacha kuzaa wanakua wanataga mayai kama vyura wengine.
Sijui zilikua story za vijiweni pale bomaroad
Ulidanganywa
 
Haikuwa rahisi....waliwatengenezea artificial environment maabara na ilikuwa kama trial and error, walikufa sana kipindi cha mwanzo na ilichukua muda hadi walipoanza kuzaliana huko maabara
Kweli kabisa na hapa issue ilikuwa ni financial muscle. Je Serikali ya Tz ingeweza kutoa fedha nyingi zile kwa kufanyia majaribio tu ya ecolojia ya chura? Utafiti ulichukua kama miaka tisa kabla ya kupata population ya kutosha kuweza kuwarudisha Tz, je hizo fedha zingetolewa na serikali yetu?

Unaweza kuuliza ni faida gani kwao wanapata? Kwanza kwa kuwa wao ni wataalamu wenye uzoefu wa muda mrefu kwa hivyo wanajiongezea umaarufu. Pili wao wakiomba fedha kwenye serikali yao kwa ajili ya utafiti ni rahisi kupatiwa. Tatu wale vyura wako kwenye zoos (Toledo na Bronx) ambazo zinaingiza fedha kwa mamilioni na hao vyura ni sehemu ya vivutio katika hizo zoos.
 
Back
Top Bottom