Clouds FM yasababisha Jide kutoshirikiana na wasanii wa Bongo

juvenile davis

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2015
Posts
4,752
Reaction score
4,467
Kama tunavyojua ya kwamba Lady Jay dee komandoo hana mahusiano na redii clouds fm,sasa hali hiyo imefanya huyu dada hata nyimbo zake kutochezwa katika kituo hicho.

Kumbuka clouds washakuwa katika tafrani na wasanii kama Mapacha,Sugu,Rama dee n.k,lakini hao wote waliomba msamaha na walisamehewa na bado nyimbo zao hazichezwi pale wala hata interviews hawapewi wala nini! Sasa huyu dada nadhani anaona aibu kuomba radhi clouds fm kwa kuwa anajua hata akiomba msamaha bado hawatacheza nyimbo zake, kitendo cha Jide kugombana na clouds fm kimemfanya akose ushirikiano na wasanii wote wa tanzania na hico kujikuta hakuna msanii anaeomba kufanya collable na yeye.

Hii inatokana na kwamba wasanii wanaogopa endapo watamshirikisha hii maana yake nyimbo haitapigwa clouds fm na ndio redio kubwa Tanzania nzima,ukitaka wimbo wako uvume ni lazima udili na hawa majamaa,kazi ipo
 
Ilikua zamani mkuu! Sio sasa!

Clouds sasa Kama joka la kibisa! Unaweza usipite kwao Na ukatoka, now days artists wanategemea video zaidi, Kama Ni Video tunaongelea tv station ambapo Clouds tv haina ubora WA eatv!

Kwa sasa artist wanaitegemea zaidi eatv coz nyimbo ikipewa airtime hapo Ni East and central Africa kwa wakati mmoja!
 
Hata kabla sijamaliza kuisoma hii habari imebidi nikimbilie kukosoa. Rama Dee hakuwai kuomba msamaha waliomba msamaha ni mapacha. Sugu walipatanishwa na aliyekuwa waziri wa habari na michezo kipindi kile Emanuel nchimbi.
 
Mkuu siku hizi mambo yamkebadilika sana, wasanii wanategemea zaidi Video na katika TV, Clouds hawanusi hata chembe kwa EATV, maana siku hizi wameongeza vipindi vingi mno vya muziki, kuanzia Muziki Mnene, Mperampera, Bongo Hits na nyingine. Hivyo wasanii siku hizi wanadili zaidi na video kuliko audio.
 
Haingizi,maana shows hapati.kumbuka tangu atoe Ndindindi hajafanya show sehemu yoyote[/QU
juzi tu hapa kigamboni jide alikua na show ya birthday ya eatv..hii inadhihirisha huna uhakika na unachokizungumza
 
Mtoa posti mi nakuonea haya japo sikujui,maneno gani haya ya kinyonge na kitumwa kabisa,hivi jide anahitaji mbeleko kweli?The ndi ndi ndi hujaisikia au unajitoa fahamu,Clouds wana haki na huo mfumo wao ni kituo huru,lkn wasitumie vibaya uhuru wao kunyongesha wasio jitambua.
 
Rama Dee na Sugu hawakuomba msamaha mkuu,acha kupotosha watu.

Nchimbi aliwapatanisha Sugu na Ruge ambao beef yao ilikuwa inahusu project ya malaria.
 
Haingizi,maana shows hapati.kumbuka tangu atoe Ndindindi hajafanya show sehemu yoyote
We ni pimbi na muongo lini sugu aliomba msamaha? Pili peperusha bendera ya Roma linapigwa kituo gani? Mbona inajulikana kuliko nyimbo nyingi tu zinazopigwa radioni?
 
Mtoa mada umechelewa wapi? Siku hizi watu wanatumia Sana internet, kwahiyo hizi redio zipige zisipige muziki unawafikia watu popote walipo
 
kama kuna wasanii hapa nchini wanainyenyekea clouds basi mashabiki wao au wasanii kuna kichaa kati yao. jide mama kaza labda wakufuate wao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…