Ruge ndiye aliyeufanya mziki wa bongo flavor ukae kibiashara, namaanisha yeye ndiye aliyetengeneza soko lake ndani na nje, na yeye ndiye alishika soko lao, East Afrika walichemka, kina majizzo walijikita kwenye burudani lakini Ruge peke yake ndo alijikita kwenye biashara, kabla ya Ruge kuupeleka mziki huo level za kimataifa aliurasimisha ukawa na haadhi hapa nchini, nani mkulu angekaa enzi hizo kusikiliza Julietha na nyambizi? Ulichukuliwa kihuni tu, alifanya juhudi kuua hipo hop kabisa ili wasanii wote waimbe wakiwa civilized! Na kupitia makundi yote ya ki hip hop gangsters yalikufa, hapo kabla ungesikia EastCost wana bifu na TMK wanaume japo wote walionekana machoko mbele ya Nako2Nako na Kikosi cha mizinga, huku unamkuta fid q na pale dudubaya, mabifu ya kuhuni kabisa, Ruge alipofanikiwa kuua hipo hipo akamgeuza na fid q kuwa muimba taarabu siku hizi, pima uwezo wa Ruge alipomwambia Mrisho Mpoto Mjomba, acha ufala tafuta hela, muziki wako uingize hela, tangu hapo mjomba anaimba nini? Zaidi ya kualikwa Ikulu ka mwanasiasa, kazi ya Ruge katika hiyo industry ni kubwa japo yapo ya hovyo pia alifanya, amewanyonya wasanini lakini ni yeye aliyewasaidia leo kila msanii analilia ngoma yake ichezwe clouds
Hata asipocheza ngoma yako ila anajua fitina zote za hiyo industry coz he blooded to build it, jiulize tangu diamond ametoswa na clouds kuna show gani ya maana amewahi kuifanya ya kumuingizia mkwanja? Kama alivyompandosha atamshusha tu, yaani diamond asahau kukanyaga Ikulu tena mark my words, hao wasanii wote ambao Ruge kawalea na kuwakuza anaouweza kuwa destroy kama alivyofanya kwa wengine kina Saida tena dada yake, na wengine kibao, THT wakati inaanza alikuwepo kina Vumilia na tangu alipotoka kujiunga na band hadi leo hasikiki!
Kwakifupi dogo diamond anakosea sana na management yake inamdanganya, alimzingua Bob junior na Kiba waliomsaidia hadi ruge na kina babu tale kumjua, anamzingua na Ruge aliyemsaidia kufika hapo alipo leo, clouds ilikuwa haipiti siku bila kusikia nyimbo ya diamonds sasa hivi ameota mapembe subiri tu promo atakayopewa kiba utashangaa.....!