Clouds Media kuendesha shindano la DC bora, RC bora na Waziri bora. Washindi 5 wa kwanza kuzawadaiwa!

Ndio tumefikia huku?! Kuna haja gani ya kuchagua Dc bora huku kesho yake anaweza kuamka kaenguliwa!? Au ndio itakuwa tiketi ya yeye kuendelea kubaki madarakani kwa muda mrefu.! Maana upande ule upepo huwa hautabiriki kwake muda wowote wakt wowote lolote linaweza tokea
 
Naona hii radio imekosa vipindi sasa na eamua kuwa tume ndogo ya uchaguzi ya kutafuta viongoz bora. Hapa naona kitengo cha marketing kinajaribu kutafuta namba ya Ku win mioyo ya viongoz kujenga reputation serekalini.
 
Kiuhalisis ni kwamba mtu akishachaguliwa kuwa DC, RC au Waziri tayari huyo ni Kiongozi Bora, kwa sababu hakuna mwenye uwezo wa kuona na kuweka vigezo vya ubora wa viongozi hao zaidi ya Rais wa Nchi. Kitendo cha kuchagua DC,RC na Waziri Bora ni kumkosoa Mhe. Rais.
 
To me, Amos Makala has outsmarted all, he is the best.
 
Ma-Dc kama wa wilaya za Tanganyika, Nanyumbu, Kasulu, Kaliua, Tandahimba nao wanashiriki?

Au hilo Shindano nia kwa ajili ya Ma-Dc kama Jojo wa Kisarawe, Sophia Mjema, Jerry Muro wa Arumeru?
 
h
Mama mjema anatakiwa awe RC u DC ni kumuonea
uu ni uhuni tu kuna ma dc wanapenda sana kucheza na media ila kazi hazifanyiki na hawajafanya chochote kwao ila wale madc wanaopiga kazi kimya kimya hawawezi kuonekana n,nyie hamuoni hadi sasa wa mjini ndio wanaonekana maana wanajua kucheza na kamera huu ni usanii mwingne
 
Ma-Dc kama wa wilaya za Tanganyika, Nanyumbu, Kasulu, Kaliua, Tandahimba nao wanashiriki?

Au hilo Shindano nia kwa ajili ya Ma-Dc kama Jojo wa Kisarawe, Sophia Mjema, Jerry Muro wa Arumeru?
Mkuu hata Patrobas Katambi anashiriki!
 
Kasesera na Godwin Gondwe kama nawaona vile!
 
Wewe ni ndugu wa makonda, mimi nasema ukweli, mama mjema alitakiwa kuwa RC na makonda hafai kuwa hata DC
 
Hawa Clouds huwa hawajifunzi tu kiherehre chao hakikomi pamoja na kujipendekeza kote wameambulia aibu bado hawasikii tu, sasa huyo Jokate ana mda gan kazini mpk awe bora kuliko wengine au wanawashindanisha kwa kiki
 
Twende na RC DSM kwa kazi kubwa aliyoifanya Kupambana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…