Clouds Tv imekosa studio yenye hadhi kipindi cha Sports Bar?

John Gregory

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2019
Posts
1,137
Reaction score
2,147
Habari wakuu,

Nimeshangaa sana kuona hii studio/chumba cha habari wanachotumia Clouds Tv katika kipindi cha Sports bar mpaka nikajiuliza kwa nini wameamua kufanya hivyo? Je, wamekosa resource? Ubahili? Au ukata?

Kwakweli chumba cha habari ni kama wapo ndani ya 'contena' au kabatini, Yaani wamebanana mno mpaka hata ukiangalia namna walivyokaa unaona kabisa hawako comfortable nahisi wakati mwingine hata harufu ya kinywa nahisi hutawanyika huku magoti yakigongana! Ujumbe kwenu Clouds, Je, mmekosa kabisa chumba cha habari ambacho wachambuzi watakuwa comfortable zaidi kama EATV ma wengineo?



 
Ukiacha Azam media(kiasi wanajitahidi),media nyingine ni ushuzi mtupu..hakuna uwekezaji wa kueleweka..ni ujanja ujanja tu..uwekezaji wakuanzia personnel hadi studio settings.
 
Clouds TV kuhusu setup za studio kwenye TV hawajawahi kufanikiwa katika vipindi vyote. Setup zao yani huwa kama za startv
 
Hawa jamaa wamekosa mvuto
 
Clouds TV kuhusu setup za studio kwenye TV hawajawahi kufanikiwa katika vipindi vyote. Setup zao yani huwa kama za startv
Kuna kipindi kilikuwa ijumaa kinaitwa Washa kideo atleast pale walijitahidi..vingine hovyohovyo..
 
Studio za media nyingi bongo hazikujengwa kwa matumizi ya studio. Yaani media ilizaliwa ikalikuta jengo ambalo lilijengwa kwa matumizi mengine.
 
CLOUDS WAMECHOKA HAOOOO, WANASUBIRI KUFA KIUME
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…