Yoyo Zhou
Senior Member
- Jun 16, 2020
- 126
- 215
Wawakilishi kutoka vyombo vya habari vya kawaida kama vile Shirika la Utangazaji la serikali ya Kenya (kbc), wataalam maarufu wa ndani, na Ubalozi wa China nchini Kenya walihudhuria hafla hiyo.
Naibu mhariri mkuu wa CGTN, idhaa ya lugha nyingi chini ya CMG, An Xiaoyu alitoa maelezo kwa wawakilishi kuhusu umuhimu wa kihistoria wa kipindi cha mjadala. Mkutano huo ulifanyika Beijing kuanzia tarehe 15 hadi 18 J
ulai, na kupitisha azimio la kuimarisha mageuzi ya kina ili kuendeleza usasa wa China. An alisema maendeleo ya hali ya juu ya China na ufunguaji mlango wa hali ya juu utaleta uhakika wa thamani katika ulimwengu uliojaa misukosuko na mabadiliko na kuunda fursa zaidi za maendeleo.
"Afrika ni bara lenye idadi kubwa ya nchi zinazoendelea, sawa na China, nchi nyingi za Afrika kama Kenya zinatafuta njia zao za kisasa bila kushindwa kuleta maendeleo na furaha kwa watu wake. Njia ya kisasa ya China ya kuleta maendeleo imeonyesha kuwa kunanjia mbadala za kuifanya nchi kuwa ya kisasa zaidi ya jinsi nchi za Magharibi zilivyofanya,” alisema.
Afisa Mkuu Mtendaji wa Taasisi ya Sera Afrika,Profesa Peter Kagwanja , alisema kuwa ufunguaji mlango wa China na ushirikiano kati ya China na Afrika unatoa fursa nyingi za maendeleo katika nyanja mbalimbali tofauti na nchi za magharibi ambazo zimejenga kuta ili kuzuia ushirikiano.
Naibu Chansela wa Chuo Kikuu cha Nairobi Profesa Stephen Kiama alisema kuwa ushirikiano kati ya China na Afrika ni uhusiano unaotoa fursa nyingi za maendeleo kwa bara la Afrika ,hususan nchini Kenya kwani wengi wa wanaohitimu kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi wanaajiriwa katika makampuni mengi ya China nchini Kenya na sehemu mbalimbali duniani.
“Tukiendelea namna hiyo tutaendelea kufungua njia nyingi za watu wetu kupata riziki kwa sababu sasa wanaweza kuajiriwa na kampuni za kichina hapa nchini,duniani na hata China.Kama Chuo Kikuu cha Nairobi tunaendelea kufungua njia za watu wetu kupata riziki”