Congo crisis. Imeandikwa na Malisa GJ

Congo crisis. Imeandikwa na Malisa GJ

Movic Evara

Senior Member
Joined
Jan 31, 2018
Posts
197
Reaction score
431
Mgogoro wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) umebeba historia ndefu inayohitaji muda mrefu kuielezea, lakini nitajaribu kuifupisha kwa kuangazia mambo machache muhimu.

Mpelelezi wa Kiingereza, John Speke, katika kitabu chake Journal of the Discovery of the Source of the Nile (1863), aliandika kuwa asili ya Watutsi ni Pembe ya Afrika (Ethiopia, Somalia, Djibouti), na kwamba walihama katika karne ya 12 wakielekea eneo la Maziwa Makuu. Walifanya makazi yao katika maeneo ya kaskazini-magharibi mwa Ziwa Tanganyika, eneo ambalo kwa sasa ni Rwanda, Burundi, na Congo. Walipowasili, walikuta wenyeji ambao Wahutu na Watwa, ambao waliishi nao kwa amani. Wahutu na Watwa walikuwa wakulima, huku Watutsi wakiwa wafugaji.

Wakoloni waligawa maeneo ya kiutawala bila kuzingatia kijamii iliyokuwepo, na hivyo kuna jamii zikajikuta mataifa mawili. Kwa mfano, Wamasai walijikuta Kenya na Tanganyika. Watutsi walijikuta Belgiam Congo na German East Africa (Tanganyika), wakati huo Rwanda na Burudi yakiwa majimbo ya Tanganyika.

Baada ya WWI Ujerumani ilinyang'anywa makoloni yake yote. Germanan East Africa ikagawanywa, Rwanda, Burundi wakapewa Ubelgiji kama nchi moja Ruanda-Urundi, na Tanganyika ikapewa Uingereza. Jamii ya Watutsi nayo ikazidi kugawanyika kati ya Ruanda-Urundi, Congo, Uganda na wachache Tanganyika.

Pamoja na kuwa wachache kwa idadi lakini walijikuta wamegawanyika katika mataifa tofauti ingawa walikuwa watu wa jamii moja, walioongea lugha moja, wenye mila na desturi zinazofanana.

Watutsi waliojikuta eneo la Kivu (Congo) hawakupata ushirikiano mkubwa kwa watu wa eneo hilo kama Wabembe, Wavira, na Wanyindu, kwa sababu ya kujiona wa hadhi ya juu (ubugabire). Watutsi waliojipata Congo walikua wachache, sehemu kubwa ilibaki Ruanda-Urundi.

Walishauriwa kuhamia Ruanda-Urudi, lakini hawakua wanyarwanda wala Warundi. Ni Wakongomani waliozaliwa Congo. Babu zao walifika hapo toka karne ya 12 lakini mipaka ya wakoloni illiwafanya wajikute katika mataifa tofauti tofauti.

Wale walioangukia Ruanda-Uurundi waliendelea kujiita Watutsi, walioangukia Congo hawakujiita Watutsi. Wakajitambulisha kwa eneo wanalotoka, safu za Milima ya Mulenge. Kwahiyo wakajiita Banyamulenge, yani watu kutoka Mulenge. Lakini ni Watutsi, wametengwa na wenzao kwa mipaka ya wakoloni.

Ni sawa na wamassai wa TZ na wale wa Kenya. Ni jamii moja ila wametengwa na mipaka ya Wakoloni. Serikali ya Kenya haiwezi kuwafukuza Wamasai wa Kenya waje Tanzania. Itakua dhambi ya ubaguzi. Mipaka ilipowekwa waliojikuta Kenya wakawa raia wa Kenya hivyo, hali kadhalika waliojikuta Tanzania.

Watutsi wa Congo pamoja na kujiita Banyamulenge, bado hawakupata ushirikiano kutoka kwa jamii nyingine za Kivu. Hii ni kwa sababu walijiona daraja la kwanza kabla ya wengine (Ubugabire). Hata wakoloni walipokuja waliwatreat kama daraja la kwanza na kuwapa favors nyingi. Kwa sababu ya 'Ubugabire' hawakutaka kuchangamana sana na wenyeji, hivyo wakaongeza mwingiliano na Watutsi wa Rwanda.

Mwaka 1959, mfalme wa mwisho wa Rwanda, Mutara III, aliuawa. Baada ya kifo chake, Rwanda iliingia katika machafuko ambapo Wahutu waliokuwa zaidi ya 80% waliwashambulia Watutsi, wakiwatuhumu kupendelewa na Wakoloni wa Kibelgiji. Maelfu ya Watutsi walikimbilia Kivu kwa ajili ya usalama wao. Walipofika huko, waliungana na wenzao (Banyamulenge), idadi ikaongezeka.

Mwaka 1962, Rwanda ilipata uhuru, na Gregoire Kayibanda akawa Rais. Kwa mara ya kwanza, Wahutu walishika madaraka baada ya utawala wa kifalme wa Watutsi kwa miaka mingi. Kayibanda alikakandamiza Watutsi na kupendelea Wahutu wenzake. Watutsi wengi walikimbilia uhamishoni, hasa maeneo ya Kivu. Wakaenda kuungana na wenzao (Banyamulenge).

Mwaka 1973, Kayibanda alipinduliwa na Mkuu wa Majeshi, Jenerali Juvénal Habyarimana, ambaye alijiapiza kuwatokomeza Watutsi. Kwa miaka 21 ya utawala wake, Watutsi waliteswa vikali. Waliondolewa kwenye nafasi za kijeshi, mashirika ya umma, na siasa. Wengi walifungwa gerezani au kuuawa. Hali hii iliwafanya Watutsi wengi zaidi kukimbia Rwanda na kuelekea maeneo mbalimbali ikiwemo Kivu. Walioenda Kivu wakaenda kuongeza idadi ya Banyamulenge.

Baadhi ya wanajeshi wa Kitutsi hawakuridhika na ukandamizaji uliofanywa na Habyarimana. Wakajiorganize kupambana. Wakati huo Kagame akiwa askari wa NRA ya Uganda akimsaidia Museveni vita vya msituni. Mwaka 1983 hadi 1985 alienda kozi ya kijeshi TMA, Moduli. Alipohitimu akarudi Uganda kumsaidia Museveni vita vya msituni na hatimaye mwaka 1986 wakafanikiwa kuchukua nchi. NRA ikawa sehemu ya jeshi la Uganda kabla ya kubadilishwa muundo mwaka 1995 kuwa UPDF.

Kagame akawa mkuu wa intelijensia ya jeshi. Baadae akaenda masomoni Marekani. Akiwa huko RPF ikaanzishwa na Jenerali Fredy Rwigyema kupambana na Serikali ya Habyarimana. Lakini Jenerali Rwigyema akauawa kwa guruneti akiwa uwanja wa vita. Kagame akalazimika kukatisha masomo na kurudi Rwanda kuongoza RPF akishirikiana na Alexis Kanyarwenge. Museveni akampa msaada wa fedha, silaha na chakula. RPF ikaweka kambi Uganda eneo la Kabale, Burundi eneo la Muyinga na Congo maeneo ya Kivu, Uvira na Goma.

Mwaka 1994, askari wa RPF wakatungua ndege ya Rais Habyarimana ikiwa inakaribia kutua uwanja wa ndege wa Kigali ikitokea Dar es Salaam kwenye mazungumzo ya Amani alikuwa na Rais Cyprien Ntaramira wa Burundi. Wote wawili walikufa papo hapo.

Kuuawa kwa Rais Habyarimana kuliamsha hasira za Wahutu na kusabisha mauaji ya Kimbari ambapo Watutsi na Wahutu wenye msimamo wa wastani waliuawa kikatili kwa kucharangwa mapanga. Hali hiyo ilisababisha Watutsi wengi kukimbia nchi yao. Wapo waliokimbilia Tanzania, Uganda, lakini wengi zaidi walikimbilia eneo la Kivu.

Kwa kifupi, idadi ya Watutsi eneo la Kivu iliongezeka siku hadi siku. Watutsi walioenda Kivu wengi hawakurudi Rwanda hata baada ya vita kumalizika. Ilikuwa vigumu kutofautisha Mtutsi mwenye asili ya Congo (Banyamulenge) na Mtutsi wa Rwanda, kwa sababu wote wanaongea lugha moja, mila na desturi moja.

Kwahiyo hisia za Wakongomani kwamba Banyamulenge ni wageni zikaanza kupata nguvu kutokana na uhamiaji mkubwa wa Watutsi maeneo ya Kivu kaskazini na kusini. Wakati huo Congo ikiitwa Zaire Rais Mobutu Sese Seko alikataa kuwatambua Banyamulenge kama raia wake, na akazuia wasipewe vitambulisho vya taifa.

Wakati hayo yakiendelea Congo, kule Rwanda, kikundi cha waasi cha RPF chini ya Paul Kagame kilifanikiwa kuyashinda majeshi ya serikali na kuchukua dola baada ya yale mauaji ya kimbari. Askari wa jeshi la Rwanda, ambao wengi walikuwa Wahutu (Itarahamwe), walikimbilia Congo. Walipofika kule, wakaanzisha kikundi cha waasi cha kupigana na serikali ya Rwanda kilichoitwa FDLR. Kikundi hicho kikaungwa mkono na serikali ya Mobutu. Hivyo Mobutu akawa anawapa silaha wapigane na serikali ya Kagame ili kurudisha utawala wa Wahutu madarakani.

Wakati Mobutu akisaidia waasi kuangusha serikali ya Rwanda, kulikia na vikundi vya waasi zaidi ya 40 vinapigana na jeshi lake. Moja kati ya vikundi hivyo ni Alliance of Democratic Forces for the Liberation (AFDL) kilichokuwa kinaongozwa na Mzee Laurent Kabila, ambaye ni Mluba wa Katanga, kusini mashariki mwa Congo karibu na Ziwa Tanganyika.

Baada ya miaka karibu 30 ya kupigana msituni, hatimaye nguvu zikapungua. Akawa haendi tena mstari wa mbele. Mara kwa mara alikuja kupumzika nyumbani kwake Msasani jijini DSM, akimuachia Kanali Reuben Um-Nyobe kuongoza kikosi msituni.

Mobutu alipoamua kuwasaidia askari wa FDLR (Intarahamwe) kupigana na serikali ya Rwanda, Kagame nae akaamua kumuunga mkono Laurent Kabila na kikundi chake cha AFDL ili wamng'oe Mobutu. Yaani, serikali ya Rwanda ikaunga mkono waasi wa Congo kwa sababu serikali ya Congo inaunga mkono waasi wa Rwanda. ‘Scratch my back, and I will scratch yours’.

Wakati huo, inadaiwa serikali ya Rwanda ilikuwa imepata silaha nyingi kutoka Ufaransa na UK, kwa hiyo Kagame alijipima akaona ana nguvu za kupigana na Mobutu. Wakati huo Kagame alikuwa Makamu wa Rais chini ya Pasteur Bizimungu, lakini yeye ndiye aliyeongoza kila kitu. Sababu za kumuunga mkono Kabila;
1. Ethnicity (Waluba na Watutsi wanaelewana)
2. Mobutu kuunga mkono FDLR (Intarahamwe)
3. Uwepo wa rasilimali nyingi sana eneo la Kivu, hasa madini.

Eneo la Kivu ni eneo la kimkakati sana na mabepari wote duniani wanalitolea macho kutokana na utajiri wake. Kivu ina madini ya Coltan ambayo yanatumika kutengeneza simu na laptop. 80% ya coltan yote duniani inatoka Congo (unaweza kugoogle kama huamini). Yani kwa kifupi bila Congo hakuna smartphones wala laptop duniani.

Kivu pia kuna madini ya tin yanayotumika kutengenezea solder za kuchomelea vifaa vya kielektroniki kama radio, TV, simu, nk. Kuna madini ya Tungsten yanayotumika kutengenezea silaha. Na pia kuna Cobalt inayotumika kutengeneza betri mbalimbali zikiwemo za magari. Kama haitoshi Kivu kuna dhahabu nyingi mno. Eneo la Kivu ni eneo lenye dhahabu nyingi zaidi duniani ambayo bado haijachimbwa (The most unexplored gold site globally).

Kagame aliona fursa. Wakati huo Rwanda ilikuwa imetoka kwenye vita na machafuko ya muda mrefu. Akataka rasilimali za jirani. Lakini atazipataje wakati yeye na Mobutu hawaelewani? Akakaamua kumuunga mkono mzee Laurent Kabila. Lakini akaweka masharti. Nikikusaidia kumng'oa Mobutu, eneo la Kivu Kusini, lenye Watutsi wengi (Banyamulenge), litajitenga na Congo na kuwa nchi inayojitegemea.

Alishapiga hesabu za mbali za kuifanya Kivu kuwa sehemu ya Rwanda baada ya kujitenga DRC. Kabila akasema poa tu. Ashapigana miaka 30 msituni bila mafanikio? Sasa kapata "kamserereko" ka kwenda Ikulu akatae? Kagame nyuma yake walikuwepo Ufaransa na Uingereza akasema twende kwa maandishi. Mkataba ukasainiwa mji mdogo wa Lemera, Kivu Kusini. AFDL ikapewa support ya silaha na pesa, ikaamsha dude kupigana na majeshi ya serikali (FARDC).

Wakati Mobutu anajaribu kupambana na AFDL, vikaibuka vikundi vingine vya waasi zaidi ya 40 kupigana na majeshi ya serikali. Vita ikiwa imepamba moto, Rwanda ikajitosa rasmi kupigana na serikali ya Mobutu kwa kisingizio cha kuwatafuta wanamgambo wa Intarahamwe waliokimbilia Congo. Uganda nayo ikaingiza jeshi kuwatafuta waasi wa LRA. Mobutu kaona "nini cha kufia" akadaka chopa akatokomea zake Moroco. Kesho yake tar.17 Mei 1997, Laurent Kabila akatangazwa Rais mpya wa Congo. Vita hii ikabatizwa jina vita vya kwanza vya Congo (1996-1997).

Alipoingia Ikulu Kabila alifuta jina Zaire na kurudisha Congo (Jamhuri ya kidemokrasia). Baadae alifikiria kuiachia Kivu, eneo lenye utajiri mkubwa wa madini adimu duniani. Akasema "to hell with Lemera Agreement" akautupilia mbali mkataba wa Lemera. Akasema Kivu itabaki Congo na madini ya Kivu yatajenga Congo. Full stop. Ashakuwa Rais utamfanya nini?

Kagame hakuamini macho yake. Alishawaza jinsi ambavyo Rwanda ingekuwa Dubai ya Afrika kwa rasilimali za Congo. Lakini ghafla aligeukwa na mshirika wake Laurent Désiré Kabila. Akamfuata "Godfather" wake mzee Museveni. Mzee akasema kama katugeuka tumpige. Wakatafuta kikundi cha Waasi wakiunge mkono. Wakapata Rassemblement Congolais pour la Démocratie (RCD), kilichoongozwa na Jenerali Ernest Wamba dia Wamba. Kikundi kikapewa silaha na fedha kikaanza kumshughulikia Kabila.

RCD ikaanza kuchapana na jeshi la Congo (FARDC) ikiwa na backup ya Rwanda na Uganda. Vita vikapamba moto. Rwanda na Uganda nao wakaingiza majeshi Congo kusaidia waasi wa RCD. Kabila akaona anazidiwa, akaomba msaada Angola na Chad. Nchi hizo zikaleta vikosi vyake Congo. Mapigano yakawa makali sana. Eneo la mashariki mwa Congo likageuka machinjioni. Watu walikufa kwa wingi, mpaka maiti zikatapakaa barabarani bila kuzikwa, zikawa zinadonolewa na ndege.

Hii iliitwa Vita ya Pili ya Congo (1998–2002), iliyokua mbaya zaidi katika historia ya vita zote Afrika. Imebatizwa jina "Vita Kuu ya Afrika". Inakadiriwa watu laki tano walipoteza maisha huku mamilioni wakikimbia nchi. Mapigano yaliendelea, huku vikosi vya Rwanda na Uganda vikichota madini. Katikati ya mapigano mgongano wa kimaslahi ukajitokeza.

Jasin Stearns, katika kitabu chake Dancing in the Glory of Monsters, anasema Kagame alishindwa kuelewana na "godfather" wake Museveni juu ya mgawanyo wa mali. Hali hiyo ilifanya kikundi cha RCD kipasuke na kuzaliwa vikundi viwili. Cha kwanza kikajiita RCD-Goma kikiongozwa na Kanali Emile Ilunga (hiki kilisaidiwa na Rwanda) na cha pili kikajiita RCD-Kisangani, kikiongozwa na Jenerali Mbusa Nyamwisi (kikisaidiwa na Uganda).!
 
CONGO CRISIS - Part 2

Baada ya kundi la RCD kuvunjika, yalizaliwa makundi mawili ambayo ni RCD Goma (liliungwa mkono na Rwanda) na RCD Kisangani (likiungwa mkono na Uganda). Aliyekua Kiongozi wa RCD Ernest Wamba Dia Wamba akaamua kukaa pembeni baada ya kugundua wanatumika kupigana kwa maslahi ya watu wengine.

Kwahiyo makundi haya yakapata viongozi wapya. RCD-Goma ikaongozwa na Kanali Emile Ilunga na RCD-Kisangani, ikaongozwa na Jenerali Mbusa Nyamwisi. Ikumbukwe kabla kundi la RCD halijavunjika, lilikuwa limeshikilia maeneo mengi ya migodi huko Goma, Bukavu, na Katanga. Sasa baada ya kuvunjika, ukatokea mgogoro wa kugawana maeneo. Mgodi upi uende RCD Goma na upi uende RCD Kisangani.

Kwa hiyo wakaanza kupigana tena wao kwa wao. Ikapigwa vita moja kali sana pale Kisangani, ikabatizwa jina la ‘Six Day War’ maana ilipiganwa kwa siku sita. RCD-Goma, ikawatandika vibaya sana RCD-Kisangani. Tar.10 June 2000 RCD Kisangani ikaachia migodi yote na kukimbia. RCD-Goma wakataka RCD-Kisangani wabadili jina lao maana mji wa Kisangani haukuwa chini yao tena. Hatimaye, RCD-Kisangani wakabadili na kujiita RCD-ML, yaani Rally for Congolese Democracy - Liberation Movement.

RCD - ML walikimbilia kwenye milima Mikeno karibu na hifadhi ya Virunga kujipanga upya. RCD-Goma wakaendeleza mapigano kuelekea Kinshasa. Lakini kufika Bukavu wakakumbana na upinzani kutoka wanamgambo wa Maï-Maï waliokua wamepewa silaha na serikali za majimbo kupigana na askari yoyote mgeni kwenye ardhi yao.

Maï-Maï waliongozwa na Kanali Musa Sindi upande wa Kivu Kusini na Sheikh Ntabo Ntaberi kwa Kivu Kaskazini. Kwa hiyo safari ya RCD Goma kwenda Kinshasa kumng’oa Laurent Kabila ikakutana na kizuizi cha Maï-Maï. Wakachapana sana. Watu zaidi ya 1,000 wakapoteza maisha.

Kwahiyo vita ya kumng'oa Laurent Kabila ikawa ngumu maana vikundi vingi vya waasi vilianza kupigana vyenyewe kwa vyenyewe. Hali hiyo ilifanya vita kuwa ngumu zaidi, maana watu walipigana bila mpangilio. Risasi zikafyatuliwa hovyo hovyo na wananchi wengi wakapoteza maisha.

Wakati mapigano makali yakiendelea huko mashariki mwa Congo baina ya vikundi vya Waasi na wanamgambo wa Maimai, hali ikatulia mjini Kinshasa na Rais Kabila akapata nafasi ya kupumua kidogo. Maadui zako wakipigana wewe utafanya nini zaidi ya kunywa supu na chapati 2 kujipongeza?

Lakini alichosahau Kabila ni kwamba Kagame ni Jasusi mwandamizi. Wakati wa kusaini mkataba Lemera, Kagame alimchomekea "watu wake" kwenye kikosi chake cha ulinzi. Mmojawapo ni Luteni Rashid Kasereka, Mtwa wa Kivu Kusini mwenye asili ya Rwanda. Januari 16, 2001, Luteni Kasereka alimfyatulia Rais Kabila risasi 4 za tumbo na kumuua papohapo.

Jumuiya ya kimataifa ikamtuhumu Kagame kuhusika, lakini akakanusha na kusema ni madai yasiyo na msingi. Baada ya kifo cha Mzee Kabila, mwanae Joseph akaapishwa kuwa Rais akiwa na miaka 29 tu. Joseph akafanya jitihada mbalimbali za kukomesha vita kwa kushirikisha Jumuiya ya kimataifa.

Julai 30, 2002, ukasainiwa Mkataba wa Pretoria (The Pretoria Agreement) uliotaka pande zote kusitisha mapigano. Desemba 17, 2002, ukasainiwa Mkataba mwingine ulioitwa Global &Inclusive Agreement (maarufu kama 2003 Peace Deal). Na hatimaye, Aprili 2, 2003, ukasainiwa Mkataba Maarufu wa Sun City Peace Agreement uliomaliza kabisa vita ya Congo.

Pamoja na mambo mengine, mkataba huo ulitaka kuondolewa kwa majeshi yote ya kigeni nchini Congo, kuwepo na utaratibu wa uchaguzi wa kidemokrasia, na kuwaingiza jeshini askari wa vikundi vya waasi. Mkataba huo ulihitimisha Vita vya Pili vya Congo. Vita mbaya mno katika historia. Vita hivi vilibatizwa jina "The Great war of Africa" kwa jinsi vilivyoshirikisha mataifa mengi, na jinsi vilivyoleta madhara makubwa kwa watu ikiwemo vifo vya zaidi ya watu 500,000.

Baada ya kumalizika kwa vita hivyo, Congo ikarudi kwenye amani, japokuwa kulikuwa na vikundi vidogo vya wanamgambo katika maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo, hasa eneo la Kivu lakini makundi makubwa yote ya Waasi yalikubali kuweka silaha chini. Kuanzia mwaka 2003 hadi 2006 hali ikatulia kabisa. Kwa mara ya kwanza raia wa Congo wakalala pasi na kusikia milio ya risasi.!

Inaendelea ....
 
CONGO CRISIS - PART 3

Baada ya miaka mitatu ya utulivu, ghafla 2006 Jenerali Laurent Nkunda, aliasi jeshi kwa madai serikali imeshindwa kutekeleza Mkataba wa Amani wa SunCity. Ikumbukwe kabla ya kujiunga na Jeshi, alikua mpiganaji wa RCD - Goma, kundi lililoungwa mkono na Rwanda. Baada ya mkataba wa Suncity waasi wote waliingizwa jeshini akiwemo Nkunda.

Lakini Juni 29, 2006, Nkunda akaasi jeshi na kuunda kundi la Congrès National pour la Défense du Peuple (CNDP). Madai yake:
  • Askari wa vikundi vya waasi walioingizwa jeshini hawakupewa vyeo.
  • Serikali ya Congo kushindwa kuwatanbua Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo kama raia wa Congo.
  • Serikali ya Congo kushindwa kuwakamata wanamgambo wa kihutu wa FDLR (Intarahanwe) waliojificha Congo baada ya kufanya mauaji ya kimbari Rwanda 1994.

Nkunda akasema lengo la kuanzisha kundi la waasi la CNDP ni kupigania haki za Watutsi waishio mashariki mwa Congo (Banyamulenge) na kukabiliana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR. Nkunda akaungwa mkono na Rwanda na Uganda, akapewa silaha, vita ikaanza upyaaaaa (tamka kwa sauti ya mbunge Bwege).

CNDP ikaua raia wengi wenye asili ya Kihutu ikiwatumu kuwa wafuasi wa FDLR. Serikali ya Burundi ikiongozwa na Piere Nkurunzinza (Mhutu) ikaingiza jeshi Congo kupambana na CNDP ili kulinda raia wake waliokua Congo. Kwa miaka mitatu kukawa na mapigano makali sana mashariki mwa Congo.

January 2009 Waasi wa CNDP wakazidiwa. Laurent Nkunda akakimbilia Rwanda. Alipofika akakamatwa na kuwekwa kizuizini. Mpaka leo, bado anashikiliwa bila kufikishwa mahakamani. Jenerali Bosco Ntaganda, Mtutsi, mzaliwa wa Kinigi, jimbo la Musanze nchini Rwanda akateuliwa kuongoza CNDP. Akafanya vitendo vingi vya kikatili kwa raia kuliko mtangulizi wake, kama ubakaji, mauaji ya halaiki, na kutumikisha watoto jeshini.

Machi 23, 2009 serikali ya Congo na CNDP wakasaini Mkataba wa Amani, ulioitwao "March 23 Agreement" wenye masharti yafuatayo:
  • Kusitisha mapigano kwa pande zote.
  • Kuingiza askari wa CNDP kwenye jeshi la Congo.
  • Kutowashtaki askari wa CNDP kwa makosa waliyofanya wakati wa vita.
  • Wananchi wa Kivu wanufaike na rasilimali zao
  • Kulinda haki za binadamu Kivu.

March 23, 2009 Mkataba ukasainiwa huko Goma, kati ya serikali ya Congo na Waasi wa CNDP, wasuluhishi wakiwa mzee Mkapa na mzee Obasanjo. Mapigano yakasitishwa.

Ntaganda na askari wa CNDP wakaingizwa kwenye jeshi la Congo (FARDC). Kukawepo na miaka mitatu ya amani, vita ikakoma kabisa. Lakini ghafla, April 04, mwaka 2012 Bosco Ntaganda alitangaza kujitoa kwenye jeshi la Congo (FARDC) pamoja na baadhi ya askari waliokuwa wanamgambo wa CNDP. Ntaganda alidai Serikali ya Congo imeshindwa kutekeleza mkataba wa amani wa Machi 23, 2009.

Alisema Makataba huo uliweka masharti ya kutowabughudhi askari 600 wa CNDP waliokataa kujiunga na jeshi la Congo. Lakini serikali ya Congo iliwashughulikia. Baadhi walikamatwa na wengine kuuawa. Pia alidai serikali ya Congo imeshindwa kuwalinda Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo.

Ntaganda akatangaza kuanzisha kikundi kipya cha waasi kiitwacho M23. Alidai kutumia jina hilo ili kuikumbusha serikali ya Congo kuheshimu mkataba wa amani wa Machi 23, 2009. Kundi la M23 likapata wafuasi wengi hasa askari wa zamani wa CNDP na Banyamulenge wa Kivu. Mapigano yakaanza upya.

Rwanda na Uganda zikashutumiwa kuunga mkono waasi hao, lakini zikakataa. Hata hivyo Rwanda ililaumiwa kwa kuruhusu M23 kuwa na kambi za kijeshi katika miji ya Gisenyi na Rusizi. Pia Rwanda ilihusishwa na mgogoro huo kwa sababu Ntaganda hakuwa Mkongomani, bali Mnyarwanda aliyezaliwa na kukulia Rwanda. Ametumikia jeshi la Rwanda kwa miaka mingi, kabla ya kuhamia Congo kupigania haki za Banyamulenge.

Baada ya mwaka mmoja wa mapigano makali, vikosi vya M23 vikazidiwa nguvu na jeshi la serikali. Machi 18, 2013, Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda na akaenda mwenyewe kujisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani mjini Kigali. Akasafirishwa kwenda The Heague kwenye mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai (ICC).

Mwaka 2015 kesi yake ikaanza kusikilizwa, na mwaka 2019 akapatikana na hatia katika makosa 18, yakiwemo ubakaji, mauaji ya raia wasio na hatia, na kutumikisha watoto jeshini. Akahukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, adhabu ambayo anaitumikia hadi sasa.
 
Uchafu huu hakuna la maana

USSR
 
CONGO CRISIS - PART 3

Baada ya miaka mitatu ya utulivu, ghafla 2006 Jenerali Laurent Nkunda, aliasi jeshi kwa madai serikali imeshindwa kutekeleza Mkataba wa Amani wa SunCity. Ikumbukwe kabla ya kujiunga na Jeshi, alikua mpiganaji wa RCD - Goma, kundi lililoungwa mkono na Rwanda. Baada ya mkataba wa Suncity waasi wote waliingizwa jeshini akiwemo Nkunda.

Lakini Juni 29, 2006, Nkunda akaasi jeshi na kuunda kundi la Congrès National pour la Défense du Peuple (CNDP). Madai yake:
  • Askari wa vikundi vya waasi walioingizwa jeshini hawakupewa vyeo.
  • Serikali ya Congo kushindwa kuwatanbua Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo kama raia wa Congo.
  • Serikali ya Congo kushindwa kuwakamata wanamgambo wa kihutu wa FDLR (Intarahanwe) waliojificha Congo baada ya kufanya mauaji ya kimbari Rwanda 1994.

Nkunda akasema lengo la kuanzisha kundi la waasi la CNDP ni kupigania haki za Watutsi waishio mashariki mwa Congo (Banyamulenge) na kukabiliana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR. Nkunda akaungwa mkono na Rwanda na Uganda, akapewa silaha, vita ikaanza upyaaaaa (tamka kwa sauti ya mbunge Bwege).

CNDP ikaua raia wengi wenye asili ya Kihutu ikiwatumu kuwa wafuasi wa FDLR. Serikali ya Burundi ikiongozwa na Piere Nkurunzinza (Mhutu) ikaingiza jeshi Congo kupambana na CNDP ili kulinda raia wake waliokua Congo. Kwa miaka mitatu kukawa na mapigano makali sana mashariki mwa Congo.

January 2009 Waasi wa CNDP wakazidiwa. Laurent Nkunda akakimbilia Rwanda. Alipofika akakamatwa na kuwekwa kizuizini. Mpaka leo, bado anashikiliwa bila kufikishwa mahakamani. Jenerali Bosco Ntaganda, Mtutsi, mzaliwa wa Kinigi, jimbo la Musanze nchini Rwanda akateuliwa kuongoza CNDP. Akafanya vitendo vingi vya kikatili kwa raia kuliko mtangulizi wake, kama ubakaji, mauaji ya halaiki, na kutumikisha watoto jeshini.

Machi 23, 2009 serikali ya Congo na CNDP wakasaini Mkataba wa Amani, ulioitwao "March 23 Agreement" wenye masharti yafuatayo:
  • Kusitisha mapigano kwa pande zote.
  • Kuingiza askari wa CNDP kwenye jeshi la Congo.
  • Kutowashtaki askari wa CNDP kwa makosa waliyofanya wakati wa vita.
  • Wananchi wa Kivu wanufaike na rasilimali zao
  • Kulinda haki za binadamu Kivu.

March 23, 2009 Mkataba ukasainiwa huko Goma, kati ya serikali ya Congo na Waasi wa CNDP, wasuluhishi wakiwa mzee Mkapa na mzee Obasanjo. Mapigano yakasitishwa.

Ntaganda na askari wa CNDP wakaingizwa kwenye jeshi la Congo (FARDC). Kukawepo na miaka mitatu ya amani, vita ikakoma kabisa. Lakini ghafla, April 04, mwaka 2012 Bosco Ntaganda alitangaza kujitoa kwenye jeshi la Congo (FARDC) pamoja na baadhi ya askari waliokuwa wanamgambo wa CNDP. Ntaganda alidai Serikali ya Congo imeshindwa kutekeleza mkataba wa amani wa Machi 23, 2009.

Alisema Makataba huo uliweka masharti ya kutowabughudhi askari 600 wa CNDP waliokataa kujiunga na jeshi la Congo. Lakini serikali ya Congo iliwashughulikia. Baadhi walikamatwa na wengine kuuawa. Pia alidai serikali ya Congo imeshindwa kuwalinda Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo.

Ntaganda akatangaza kuanzisha kikundi kipya cha waasi kiitwacho M23. Alidai kutumia jina hilo ili kuikumbusha serikali ya Congo kuheshimu mkataba wa amani wa Machi 23, 2009. Kundi la M23 likapata wafuasi wengi hasa askari wa zamani wa CNDP na Banyamulenge wa Kivu. Mapigano yakaanza upya.

Rwanda na Uganda zikashutumiwa kuunga mkono waasi hao, lakini zikakataa. Hata hivyo Rwanda ililaumiwa kwa kuruhusu M23 kuwa na kambi za kijeshi katika miji ya Gisenyi na Rusizi. Pia Rwanda ilihusishwa na mgogoro huo kwa sababu Ntaganda hakuwa Mkongomani, bali Mnyarwanda aliyezaliwa na kukulia Rwanda. Ametumikia jeshi la Rwanda kwa miaka mingi, kabla ya kuhamia Congo kupigania haki za Banyamulenge.

Baada ya mwaka mmoja wa mapigano makali, vikosi vya M23 vikazidiwa nguvu na jeshi la serikali. Machi 18, 2013, Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda na akaenda mwenyewe kujisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani mjini Kigali. Akasafirishwa kwenda The Heague kwenye mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai (ICC).

Mwaka 2015 kesi yake ikaanza kusikilizwa, na mwaka 2019 akapatikana na hatia katika makosa 18, yakiwemo ubakaji, mauaji ya raia wasio na hatia, na kutumikisha watoto jeshini. Akahukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, adhabu ambayo anaitumikia hadi sasa.
NAAPA!! KAGAME mwaka huu atakimbia nchi!!
 
  • Kicheko
Reactions: rr4
Nkunda anazuiliwa Rwanda,Bosco Ntaganda anatumikia kifungo the gauge
Kwamba mwisho wa siku Pk anashindwa kuwasaidia watu wanaompasupport kupgana na Congo
 
Nkunda anazuiliwa Rwanda,Bosco Ntaganda anatumikia kifungo the gauge
Kwamba mwisho wa siku Pk anashindwa kuwasaidia watu wanaompasupport kupgana na Congo
Huelewi wazungu wanavyocheza game zao. Karata zinachangwa mpaka unakubali hapa hakuna mchezo mchafu.
Huyo Yuko The Hague kwa maelezo ya wakubwa, lazima kuwe na lab rat mmoja, space goat wa kufanyiwa mfano kuwa huu mgogoro haukuandaliwa na mtu so kwa makubaliano au pasina makubaliano unawekwa ndani.
Nkunda Yuko kizuizini lakini unakuta anakula maisha TU.
Miaka ya zamani Gereza la Karanga Moshi, Kuna wafungwa matajiri walikuwa hawalali magereza. Anatoka usiku saa mbili anaenda nyumbani. Saa kumi na Moja anakuwa amesharudi ngome.
Sio Kila ukionacho duniani kipo kama kinavyoonekana. There is a lot of things that are going on behind the scene hadi mlaji apate final product.
 
Niko upande wa Banyamulenge, Due to respect His Excellency Gen Paul Kagame ataniteua kuongoza M23, 2nd in command atakua Capt Ibrahim Traore
 
haaaaaaa pandora box hiii ....huu mgogoro ni mkubwa sana damu za watu zilizwamwagwa hapa hii nchii haiwezi tulia labda ikatwe iwe ndogo ndogo ila kwa ukubwa huo haiwezi tawalika
 
Halafu anakuja mtu ameshiba makande anakwambia Kagame hahusiki. Nimempuuza sana PLO Lumumba
Kagame anatetea ndugu zake watutsi. Mimi naona tatizo la huo mgogoro upo sehemu mbili:
1. Watutsi/Banyamulenge wa Kongo kutopewa haki zao kama raia halali wa DRC
2. Maslahi binafsi ya nchi na makundi mbalimbali ktk eneo la Kongo mashariki mahali ambapo kuna rasilimali nyingi. Hivyo, Serikali ya Kongo isaidiwe kuunda Serikali yenye nguvu na itakayohusisha makundi yote nchini humo.
 
Back
Top Bottom