Congo crisis. Imeandikwa na Malisa GJ

Congo crisis. Imeandikwa na Malisa GJ

#PART4

Baada ya Ntaganda kupelekwa The Heague, M23 iliongozwa na Sultan Makenga, Mtutsi wa Rutshuru huko Kivu Kaskazini. Mwaka 1990 Makenga akiwa na miaka 17 tu alienda Rwanda kujiunga na kikundi cha waasi RPF kilichokuwa kinaongozwa na Jenerali Fredy Rwigyema. Sultan Makenga akiwa askari wa RPF alipigana msituni dhidi ya serikali ya kihutu ya Juvenile Habyarimana.

Baada RPF ilishika dola, Askari wote wa RPF waliingizwa katika jeshi la Rwanda akiwemo Sultan Makenga. Alihudumu katika jeshi hilo kwa muda mrefu hadi kufikia cheo cha Kanali kabla ya kurudi "nyumbani" Congo, kujiunga na kikundi cha waasi cha CNDP. Baada ya mkataba wa amani wa March 23, 2009 Sultan Makenga alikuwa miongoni mwa askari 600 wa CNDP waliokataa kujiunga na jeshi la Congo (FARDC).

Mwaka 2012 Bosco Ntaganda alipojitoa kwenye jeshi la Congo na kuunga kikundi cha waasi cha M23, Sultan Makenga alikua wa kwanza kujiunga. Baada ya Ntaganda kujisalimisha, Makenga akapewa uongozi wa M23. Akaongoza kuanzia 2013 hadi 2016 kisha akaachia uongozi na kuhamia uhamishoni nchini Rwanda. July 2024 Makenga alizungunza na media kwa mara ya kwanza akiwa Kigali na kueleza bado ana azma ya kuikomboa DRC.

Baada ya Makenga, M23 ikapata viongozi ambao hawakuwa mashuhuri hadi 2022 ilipompata Corneille Nangaa, aliyekua Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi (CENI) na ndiye aliyemtangaza Tshikeshedi kuwa mshindi wa kiti cha Urais kwenye uchaguzi wa December 30 mwaka 2018.

Katika mambo yanayoshangaza na kufanya vita ya Congo kuonekana ngumu, ni jinsi Nangaa alivyotoka kuwa Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, hadi kuanzisha coalition ya vikundi vya waasi, Congo River Alliance (CRA) na kuingiza M23. Nangaa ndiye ameongoza M23 kuutwaa mji wa Goma January 2025, na kuyafurusha majeshi ya serikali. Nangaa ametangaza nia ya kumuondoa madarakani Rais Tshisekedi, ambaye mwaka 2018 alimtangaza kuwa Rais.

August 2024 Mahakama ya kijeshi mjini Kinshasa ilimhukumu Nangaa adhabu ya kunyongwa hadi kufa kwa kosa la uhaini. Hukumu hiyo ilitolewa bila yeye kuwepo mahakamani (death sentence in absentia). Nangaa amesema ikiwa M23 itashika dola, wale waliomhukumu ndio watanyongwa kwa niaba yake.!

Itaendelea.... (popcorn zisiishe).!
 
Mapatano alikuwa anasema mpiganaji mmoja juzi ni kwamba kwa kumuondoa Mobutu Rwanda itapewa North and South Kivu na Uganda itapewa Ituri..
Lakini kama watu wandaiana malipo kama hayo,it is something that can be estimated and calculated.
Nakumbuka wakati ule Tony Blair alipokuwa Waziri Mkuu siku moja ilitangazwa," Leo Uingereza imelipa installment ya mwisho ya deni lake kwa USA kwa msaada iliopata WW2"
 
#PART4

Baada ya Ntaganda kupelekwa The Heague, M23 iliongozwa na Sultan Makenga, Mtutsi wa Rutshuru huko Kivu Kaskazini. Mwaka 1990 Makenga akiwa na miaka 17 tu alienda Rwanda kujiunga na kikundi cha waasi RPF kilichokuwa kinaongozwa na Jenerali Fredy Rwigyema. Sultan Makenga akiwa askari wa RPF alipigana msituni dhidi ya serikali ya kihutu ya Juvenile Habyarimana.

Baada RPF ilishika dola, Askari wote wa RPF waliingizwa katika jeshi la Rwanda akiwemo Sultan Makenga. Alihudumu katika jeshi hilo kwa muda mrefu hadi kufikia cheo cha Kanali kabla ya kurudi "nyumbani" Congo, kujiunga na kikundi cha waasi cha CNDP. Baada ya mkataba wa amani wa March 23, 2009 Sultan Makenga alikuwa miongoni mwa askari 600 wa CNDP waliokataa kujiunga na jeshi la Congo (FARDC).

Mwaka 2012 Bosco Ntaganda alipojitoa kwenye jeshi la Congo na kuunga kikundi cha waasi cha M23, Sultan Makenga alikua wa kwanza kujiunga. Baada ya Ntaganda kujisalimisha, Makenga akapewa uongozi wa M23. Akaongoza kuanzia 2013 hadi 2016 kisha akaachia uongozi na kuhamia uhamishoni nchini Rwanda. July 2024 Makenga alizungunza na media kwa mara ya kwanza akiwa Kigali na kueleza bado ana azma ya kuikomboa DRC.

Baada ya Makenga, M23 ikapata viongozi ambao hawakuwa mashuhuri hadi 2022 ilipompata Corneille Nangaa, aliyekua Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi (CENI) na ndiye aliyemtangaza Tshikeshedi kuwa mshindi wa kiti cha Urais kwenye uchaguzi wa December 30 mwaka 2018.

Katika mambo yanayoshangaza na kufanya vita ya Congo kuonekana ngumu, ni jinsi Nangaa alivyotoka kuwa Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, hadi kuanzisha coalition ya vikundi vya waasi, Congo River Alliance (CRA) na kuingiza M23. Nangaa ndiye ameongoza M23 kuutwaa mji wa Goma January 2025, na kuyafurusha majeshi ya serikali. Nangaa ametangaza nia ya kumuondoa madarakani Rais Tshisekedi, ambaye mwaka 2018 alimtangaza kuwa Rais.

August 2024 Mahakama ya kijeshi mjini Kinshasa ilimhukumu Nangaa adhabu ya kunyongwa hadi kufa kwa kosa la uhaini. Hukumu hiyo ilitolewa bila yeye kuwepo mahakamani (death sentence in absentia). Nangaa amesema ikiwa M23 itashika dola, wale waliomhukumu ndio watanyongwa kwa niaba yake.!

Itaendelea.... (popcorn zisiishe).!
Good luck
 
haaaaaaa pandora box hiii ....huu mgogoro ni mkubwa sana damu za watu zilizwamwagwa hapa hii nchii haiwezi tulia labda ikatwe iwe ndogo ndogo ila kwa ukubwa huo haiwezi tawalika
Damu inamwagika ili familiya za kagame na mseven ziishi Kama peponi...hao wanajeshi nao NI wajinga wanashindwa kumtwanga kagame warudi kwao Rwanda Kama anawapenda kwa Nini haearudiahi nyumbani Kigali..wanataka Kongo isiyo yao...
 
Damu inamwagika ili familiya za kagame na mseven ziishi Kama peponi...hao wanajeshi nao NI wajinga wanashindwa kumtwanga kagame warudi kwao Rwanda Kama anawapenda kwa Nini haearudiahi nyumbani Kigali..wanataka Kongo isiyo yao...
kagame ni moja ya matatizo hata yeye akifa sasa hivi hii vita haiwezi isha miaka 1000.....kuna vikundi vidogo zaidi ya 100 na nchi ni kubwa sana na maliasili ni nyingi na dunia nzima inafaidika ila wakongo ndo wanapata hasara maamuzi yafanyike kwa maslahi ya wakongo
 
Kagame anatetea ndugu zake watutsi. Mimi naona tatizo la huo mgogoro upo sehemu mbili:
1. Watutsi/Banyamulenge wa Kongo kutopewa haki zao kama raia halali wa DRC
2. Maslahi binafsi ya nchi na makundi mbalimbali ktk eneo la Kongo mashariki mahali ambapo kuna rasilimali nyingi. Hivyo, Serikali ya Kongo isaidiwe kuunda Serikali yenye nguvu na itakayohusisha makundi yote nchini humo.
Survival for the fitness

Ova
 
Mapatano alikuwa anasema mpiganaji mmoja juzi ni kwamba kwa kumuondoa Mobutu Rwanda itapewa North and South Kivu na Uganda itapewa Ituri..
Lakini kama watu wandaiana malipo kama hayo,it is something that can be estimated and calculated.
Nakumbuka wakati ule Tony Blair alipokuwa Waziri Mkuu siku moja ilitangazwa," Leo Uingereza imelipa installment ya mwisho ya deni lake kwa USA kwa msaada iliopata WW2"
Hivi haikuwa kipindi Cha Donald Cameroon
 
#PART5

Baada ya M23 kuitwaa Goma walidai hawana mpango wa kuchukua miji mingine. Jeshi la Congo (FARDC) likarelax. Kumbe ilikua mbinu ya kivita. Ghafla M23 wakavamia na kuuteka mji wa Rutshuru wenye utajiri wa dhahabu, tin na Tungsten na mji wa Masisi wenye utajiri wa dhahabu na cassiterite.

Mpango wa M23 ni kufika Kinshasa na kuuangusha utawala wa Rais Felix Tshisekedi. Madai ya M23 ni yaleyale ya siku zote, ambayo ni kulinda maslahi ya Watutsi waishio mashariki mwa nchi hiyo, kupambana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR (Interahamwe), na kutaka Banyamulenge watambuliwe kama raia halali wa Congo.

Mzozo wa mashariki mwa Congo umegharimu maisha ya mamilioni ya watu toka ulipoanza. Umoja wa Mataifa (UN) na Umoja wa Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umepeleka askari wa kulinda amani. Ikumbukwe askari hao hawapigani upande wa serikali wala wa waasi. Kuna watu wanadhani askari wetu wa JWTZ walioko Congo wanapigana upande wa jeshi la serikali (FARDC). Hapana. Hawapigani upande wowote. Wanalinda amani. Lakini ikitokea kuna upande unahatarisha amani utapewa haki yake ya kikatiba.

Kwa mfano, mwaka 2012 Umoja wa mataifa uliunda jeshi la kulinda amani Congo (MONUSCO). Ndani yake kulikua na brigedi maalumu ya kunyang'anya silaha makundi ya wapiganaji - Force Intervention Bregade (FIB). Brigedi hiyo iliundwa na askari kutoka Tanzania, Malawi, Afrika Kusini na Uruguay.

April 2012, M23 wakashambulia kambi ya FIB iliyokua Rutshuru na kuua askari watatu. Aliyekua Mkuu FIB, Jenerali James Mwakibolwa alipanga vikosi vyake kujibu mapigo. M23 walichakazwa vibaya na zaidi ya askari 600 wa M23 waliuawa na wengi kujeruhiwa. Walipigwa bila huruma na kuachia miji yote waliyokua wameishikilia ikiwemo Rubaya, Kitchanga na Rutshuru. Askari 16 wa FIB nao walipoteza maisha.

Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda kujisalimisha ubalozi wa Marekani. Alipelekwa ICC akahukumiwa miaka 30 na sasa anatumikia adhabu gereza Leuze-en-Hainaut huko Ubelgiji. Sultan Makenga alirithi mikoba ya Ntaganda lakini nae alitandikwa na ilipofika March 2013, M23 walisalimu amri. Moja ya makosa ambayo Makenga anayajutia hadi leo ni kuingia kwenye 18 za FIB iliyokua inaongozwa na Jenerali James Aloizi Mwakibolwa.

Kumekua na jitihada mbalimbali za kumaliza mgogoro wa DRC kwa njia za kidiplomasia ikiwemo mkutano wa viongozi wakuu wa SADC na EAC uliofanyika leo jijini Dar.

#MyaTake:
1. Congo imeponzwa na ukarimu wake. Wakati wa vita vya Rwanda, Congo ilipokea Watutsi wengi na kuwapa hifadhi, akiwemo Kagame. Baada ya utawala wa Habyarimana kuangushwa Wahutu nao wakakimbilia Congo na kupewa hifadhi. Sasa hicho kimekua kigezo cha Rwanda kuingiza majeshi Congo kila mara kwa madai ya kuwatafuta Wahutu wa FDLR. Kwa lugha rahisi vita ya ndugu wawili (Wahutu na Watutsi) iliyopaswa kupiganwa Rwanda sasa inapiganwa Congo.

2. Congo inateswa na mipaka ya kikoloni. Laiti wakati wa kuchora mipaka jamii yote ya Watutsi ingewekwa Rwanda, leo kusingekuwa na Banyamulenge Congo, kwahiyo Watutsi wasingepata sababu ya kuishi Congo na kujifanya raia. Ni sawa na kukuta Wamasai 1,000 pale Longido, halafu uambiwe kati yao wapo wa Kenya. Utawajuaje? Utawatofautishaje?

3. Congo inateswa na rasilimali zake. Kama eneo la Kivu lisingekuwa na utajiri, mgogoro usingekuwa mkubwa kama ulivyo. Rejea #Part1 kujua utajiri uliopo Kivu. Kumbuka bila Kivu dunia haina laptop wala smartphones kwa sababu 80% ya coltan yote duniani inatoka Kivu.

4. Rwanda na Uganda ni Keyplayers kwenye mgogoro wa Congo. Kwa miaka mingi majeshi yao yameigeuza Congo shamba la bibi. Waondoe majeshi yao Congo.

5. Viongozi wengi wa M23 ni Wanyarwanda. Huu ni udhibitisho kuwa Rwanda ni kinara kwenye mgogoro huu.

6. Congo ni kubwa sana na hivyo inakosa jeshi imara la kutosha kulinda mipaka yake yote. Congo ni kubwa mara 90 ya Rwanda. Wapo wanaoshauri igawanywe kama njia ya kutatua mgogoro. Kama ambavyo Yugoslavia iligawanywa na kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe.

7. Kiongozi wa sasa wa M23 Corneille Nangaa alikua Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi 2019 na ndiye aliyemtangaza Tshisekedi kuwa Rais kwa ushindi wa 38%. Lakini alilaumiwa kupunguza kura za Martin Fayulu aliyepata 34%. Huenda kuna ahadi alipewa haikutimizwa ndio maana akaungana na Waasi.

Sababu hizo hapo juu zikifanyiwa kazi, mgogoro wa Congo unaweza kupungua kwa kiasi kikubwa. Mnaopenda kujifunza zaidi, naandika Kitabu. Get ready to have your copy. MWISHO.!
 
Malisa ni mwandishi mzuri sio kama chawa wa Mbowe ndugu Yericko. Yeye kitu kikitokea anadai tayari alishaelezea kwenye kitabu chake cha ujasusi.
 
Halafu anakuja mtu ameshiba makande anakwambia Kagame hahusiki. Nimempuuza sana PLO Lumumba
Kwa hisia rahisi tu, Kagame anahusika kwa sababu asipofanya hivyo, walw Banyaamulenge wakifurushwa huko Mashariki ya DRC watarudi Rwanda wakati ardhi ni ndogo. Kagame anaendelea kuwapambania wabaki huko huko DRC ili angalau hata awe anawatumia kupata chochote kitu madini
 
CONGO CRISIS - PART 3

Baada ya miaka mitatu ya utulivu, ghafla 2006 Jenerali Laurent Nkunda, aliasi jeshi kwa madai serikali imeshindwa kutekeleza Mkataba wa Amani wa SunCity. Ikumbukwe kabla ya kujiunga na Jeshi, alikua mpiganaji wa RCD - Goma, kundi lililoungwa mkono na Rwanda. Baada ya mkataba wa Suncity waasi wote waliingizwa jeshini akiwemo Nkunda.

Lakini Juni 29, 2006, Nkunda akaasi jeshi na kuunda kundi la Congrès National pour la Défense du Peuple (CNDP). Madai yake:
  • Askari wa vikundi vya waasi walioingizwa jeshini hawakupewa vyeo.
  • Serikali ya Congo kushindwa kuwatanbua Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo kama raia wa Congo.
  • Serikali ya Congo kushindwa kuwakamata wanamgambo wa kihutu wa FDLR (Intarahanwe) waliojificha Congo baada ya kufanya mauaji ya kimbari Rwanda 1994.

Nkunda akasema lengo la kuanzisha kundi la waasi la CNDP ni kupigania haki za Watutsi waishio mashariki mwa Congo (Banyamulenge) na kukabiliana na wanamgambo wa Kihutu wa FDLR. Nkunda akaungwa mkono na Rwanda na Uganda, akapewa silaha, vita ikaanza upyaaaaa (tamka kwa sauti ya mbunge Bwege).

CNDP ikaua raia wengi wenye asili ya Kihutu ikiwatumu kuwa wafuasi wa FDLR. Serikali ya Burundi ikiongozwa na Piere Nkurunzinza (Mhutu) ikaingiza jeshi Congo kupambana na CNDP ili kulinda raia wake waliokua Congo. Kwa miaka mitatu kukawa na mapigano makali sana mashariki mwa Congo.

January 2009 Waasi wa CNDP wakazidiwa. Laurent Nkunda akakimbilia Rwanda. Alipofika akakamatwa na kuwekwa kizuizini. Mpaka leo, bado anashikiliwa bila kufikishwa mahakamani. Jenerali Bosco Ntaganda, Mtutsi, mzaliwa wa Kinigi, jimbo la Musanze nchini Rwanda akateuliwa kuongoza CNDP. Akafanya vitendo vingi vya kikatili kwa raia kuliko mtangulizi wake, kama ubakaji, mauaji ya halaiki, na kutumikisha watoto jeshini.

Machi 23, 2009 serikali ya Congo na CNDP wakasaini Mkataba wa Amani, ulioitwao "March 23 Agreement" wenye masharti yafuatayo:
  • Kusitisha mapigano kwa pande zote.
  • Kuingiza askari wa CNDP kwenye jeshi la Congo.
  • Kutowashtaki askari wa CNDP kwa makosa waliyofanya wakati wa vita.
  • Wananchi wa Kivu wanufaike na rasilimali zao
  • Kulinda haki za binadamu Kivu.

March 23, 2009 Mkataba ukasainiwa huko Goma, kati ya serikali ya Congo na Waasi wa CNDP, wasuluhishi wakiwa mzee Mkapa na mzee Obasanjo. Mapigano yakasitishwa.

Ntaganda na askari wa CNDP wakaingizwa kwenye jeshi la Congo (FARDC). Kukawepo na miaka mitatu ya amani, vita ikakoma kabisa. Lakini ghafla, April 04, mwaka 2012 Bosco Ntaganda alitangaza kujitoa kwenye jeshi la Congo (FARDC) pamoja na baadhi ya askari waliokuwa wanamgambo wa CNDP. Ntaganda alidai Serikali ya Congo imeshindwa kutekeleza mkataba wa amani wa Machi 23, 2009.

Alisema Makataba huo uliweka masharti ya kutowabughudhi askari 600 wa CNDP waliokataa kujiunga na jeshi la Congo. Lakini serikali ya Congo iliwashughulikia. Baadhi walikamatwa na wengine kuuawa. Pia alidai serikali ya Congo imeshindwa kuwalinda Watutsi (Banyamulenge) waishio mashariki mwa nchi hiyo.

Ntaganda akatangaza kuanzisha kikundi kipya cha waasi kiitwacho M23. Alidai kutumia jina hilo ili kuikumbusha serikali ya Congo kuheshimu mkataba wa amani wa Machi 23, 2009. Kundi la M23 likapata wafuasi wengi hasa askari wa zamani wa CNDP na Banyamulenge wa Kivu. Mapigano yakaanza upya.

Rwanda na Uganda zikashutumiwa kuunga mkono waasi hao, lakini zikakataa. Hata hivyo Rwanda ililaumiwa kwa kuruhusu M23 kuwa na kambi za kijeshi katika miji ya Gisenyi na Rusizi. Pia Rwanda ilihusishwa na mgogoro huo kwa sababu Ntaganda hakuwa Mkongomani, bali Mnyarwanda aliyezaliwa na kukulia Rwanda. Ametumikia jeshi la Rwanda kwa miaka mingi, kabla ya kuhamia Congo kupigania haki za Banyamulenge.

Baada ya mwaka mmoja wa mapigano makali, vikosi vya M23 vikazidiwa nguvu na jeshi la serikali. Machi 18, 2013, Bosco Ntaganda akakimbilia Rwanda na akaenda mwenyewe kujisalimisha kwenye ubalozi wa Marekani mjini Kigali. Akasafirishwa kwenda The Heague kwenye mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai (ICC).

Mwaka 2015 kesi yake ikaanza kusikilizwa, na mwaka 2019 akapatikana na hatia katika makosa 18, yakiwemo ubakaji, mauaji ya raia wasio na hatia, na kutumikisha watoto jeshini. Akahukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, adhabu ambayo anaitumikia hadi sasa.
Noma sana
 
Back
Top Bottom