Congrats Zitto Kabwe!

Congrats Zitto Kabwe!

Invisible

JF Admin
Joined
Feb 26, 2006
Posts
16,286
Reaction score
8,380
cc3b8fc86b.jpg

0326c22955.jpg
 

Attachments

Invisible,
Mkuu hata sielewi mahusiano ya kichwa cha habari na maelezo uloyatoa hapa..Sioni uhusiano wa Zitto na habari hii ikiwa wananchi wenyewe wa Kigoma hawatahusika zaidi ktk mjadala huu. Ni wao wanaofahamu uwakilishi wa Zitto kama mbunge wao na kaweza yepi.
Binafsi Zitto namtazama kama mbunge wangu wa Upinzani hivyo sifa zake zinatokana na uwakilishi wake wa hoja za upinzani ndivyo navitazama zaidi mathlan swala la Buzwagi, na mikataba feki lakini anapokuja kupendekeza tena mkataba feki mwingine inaondoa nguvu kubwa ya sifa alovuta wakati wa Buzwagi. Kwa sababu hata mkataba wa Buzwagi ungetuwezesha kuvuta japo kidogo hizo asilimia 3 na zikapunguza matatizo yetu, pia wakazi wa Buzwagi ambao wanahitaji sana huduma za Shule, Zahanati, Maji safi na Umeme wangeweza kupata japo kiduchu..Barrick wangeweza kuondoa tatizo hilo la wakazi wa Buzwagi nikitumia mtazamo wake ktk swala la Dowans..
 
labda zitto ni mbunge wa "tanzania yote"

btw ... nani kaendesha hii poll?
 
Mkuu Tunaweza kupata report nzima? Maana naona hizo charts peke yake zinaweza zisiseme mengi.

Pamoja na hayo Hongera kwa Zitto na Wabunge wenzake walioonyeshwa kwenye chart, angalau wananchi wanaona michango yao.
 
Invisible,
Mkuu hata sielewi mahusiano ya kichwa cha habari na maelezo uloyatoa hapa..Sioni uhusiano wa Zitto na habari hii ikiwa wananchi wenyewe wa Kigoma hawatahusika zaidi ktk mjadala huu. Ni wao wanaofahamu uwakilishi wa Zitto kama mbunge wao na kaweza yepi.
Binafsi Zitto namtazama kama mbunge wangu wa Upinzani hivyo sifa zake zinatokana na uwakilishi wake wa hoja za upinzani ndivyo navitazama zaidi mathlan swala la Buzwagi, na mikataba feki lakini anapokuja kupendekeza tena mkataba feki mwingine inaondoa nguvu kubwa ya sifa alovuta wakati wa Buzwagi. Kwa sababu hata mkataba wa Buzwagi ungetuwezesha kuvuta japo kidogo hizo asilimia 3 na zikapunguza matatizo yetu, pia wakazi wa Buzwagi ambao wanahitaji sana huduma za Shule, Zahanati, Maji safi na Umeme wangeweza kupata japo kiduchu..Barrick wangeweza kuondoa tatizo hilo la wakazi wa Buzwagi nikitumia mtazamo wake ktk swala la Dowans..
Mkandara,

Nimeambatanisha doc nzima. Well, ni vema kuangalia "Page 36" maana image haionekani vema then utajua naongelea nini.
 
Invisible,
Mkuu, shukran nimekupata sasa hizo asilimia 25 ndio sifa ya mbunge washuhuri wa Kitanzania?..kaazi kweli kweli!. Hizo 25% ya wananchi kukubali uwakilishi wa mtu ni failure kwa Mbunge, mtu kama Zitto anatakiwa kujipima yeye mwenyewe anakubalika vipi na sii kutazama walioko nyuma yake..
Kifupi mkuu wangu ukiwa ktk mtihani uka score asilimia 25% kweli unastahili kupongezwa au ndio kusema shule hiyo haifai kabisa!...mtu wa kwanza kwa aslimia 25% basi hiyo sii shule tena mwondoe mwanao asisome hapo..
Tunachojifunza hapa ni kwamba Bunge letu halkina wabunge kabisa, wananchi hawana imani nalo kabisa iwe mtu kwa mtu.
 
Mkuu Mkandara,

Pamoja na kwamba wananchi wa Kigoma Kaskazini wanaweza wasihusike kutoa maoni yao kwenye huu mjadala, bado ninaona siyo vibaya jamii ikijua ama kusoma report kama hizi just kutufahamisha kwamba wabunge gani wanaowajibika kwa wananchi wao na nchi yao.

Lakini nina tatizo moja kwenye hizo charts, sijajua waliohojiwa ni watanzania wote nchi nzima ama ilikuwaje? Kama ni survey ya nchi nzima then interpretation ya charts inatakiwa ifanywe with caution.

Tunaweza kupima utendaji wa Mbunge kwa njia mbili. Moja, je, wapiga kura wake (jimboni) wana maoni gani kuhusu Mbunge wao. Kuna vipengele vinaongelea ushiriki wa Mbunge kwenye shughuli za maendeleo, sasa kama respondent ni mkazi wa Dar au Mwanza atajuaje yaliyo kwenye ground huko Kigoma Kaskazini ama Same kwa Mama Kilango au Kyela kwa Dr. Mwakyembe? Kwa hiyo charts hizi zingetoa picha halisi kama tungejua Jimboni kwa mbunge husika wananchi wanasemaje? Na hapo inabidi kuwa makini kwamba waliohojiwa ni wa chama gani? Maana wengine ni wakereketwa, hata Mbunge afanye mambo mazuri kiasi gani bado wataona hajafanya kitu kwa kuwa ni si Mbunge wa kutoka chama chao.

Ngazi ya pili ni at a National Level, ambapo sasa akina Mkandara na Keil wanaweza kutoa maoni yao kwamba kwa jinsi tunavyomuona Bungeni akitoa hoja ama kuibana serikali tunaona kwamba anafaa sana. Ingawa kwenye hili kundi maoni yetu hayawezi kuwa na maana sana kwa kuwa sisi sio wapiga kura wa Mbunge husika. Kwa hiyo mimi nikisema Zitto anafaa kurudi Bungeni kwenye uchaguzi wa mwakani, ni utashi wangu lakini siwezi kuchangia chochote kwenye kumrudisha Bungeni. Ningekuwa ni mkazi wa Kigoma Kaskazini, kura yangu moja ina mchango mkubwa sana kumrudisha Bwana Zitto mjengoni na pia hata nikiongea na vijana wenzangu Jimboni ninaweza kuwa-influence wakaona mazuri ya Zitto na wao wakaongezea kura zao.

Ndiyo maana nikamuomba Invisible kama anaweza kutuwekea report yote ili tusome na kuona sample ilipatikana vipi. Tusije tukawamwagia pongezi sisi wakazi wa Dar lakini kwenye majimbo yao kuko hoi bin taaban na wapiga kura wao hawataki hata kuwaona.
 
Kwanza nimpongeze Zito, pamoja na weote walioonekana katika hiyo watatu wanaomfuatia.

Lakini hapa ndipo panapokuwa na matitizo katika design ya utafiti kama huu. Swali, unapolielekeza kutafuta mbunge aliyefanya vyema, halafun ndani yake unchanganya na mawaziri, ni lazima utapata matokeo yanayoegemea upande mmoja (biased). Waziri anawakilisha serikali, na mara nyingi wananchi inawawia vigumu kupima watu hawa 2 katika mizani moja. Ingekuwa ni waziri yupi aliyekonga nyoyo za wananchi, na ni mbunge yupi aliyekonga nyoyo za watu. Vingenevyo ni kutowaweka mawaziri katika mizani wanayostahili.

Jambo jingine, katika hizo kurasa 2 haijaelezwa kuwa watu waliohojiwa walipatikana kwa utaratibu upi, ambayo nayo kitakwimu inaweza kuwa na matatizo kufanya tathmini wakilishi.
 
Kwanza nimpongeze Zito, pamoja na weote walioonekana katika hiyo watatu wanaomfuatia.

Lakini hapa ndipo panapokuwa na matitizo katika design ya utafiti kama huu. Swali, unapolielekeza kutafuta mbunge aliyefanya vyema, halafun ndani yake unchanganya na mawaziri, ni lazima utapata matokeo yanayoegemea upande mmoja (biased). Waziri anawakilisha serikali, na mara nyingi wananchi inawawia vigumu kupima watu hawa 2 katika mizani moja. Ingekuwa ni waziri yupi aliyekonga nyoyo za wananchi, na ni mbunge yupi aliyekonga nyoyo za watu. Vingenevyo ni kutowaweka mawaziri katika mizani wanayostahili.

Jambo jingine, katika hizo kurasa 2 haijaelezwa kuwa watu waliohojiwa walipatikana kwa utaratibu upi, ambayo nayo kitakwimu inaweza kuwa na matatizo kufanya tathmini wakilishi.
Purely UDAKU.
 
Kwenye utafiti kama huu, ni watu wachache tu, sio rahisi uwahusishe watanzania wote, ama sivyo itakuwa uchaguz wa rais.

Pili hii haina ubishi wala hailazimishi kila mtu akubaliane nao.

So, wote mnaopinga, aidha mfanye zenu, kuna mtu anasema bunge la Tanzania halina wabunge kabisa!!!! yet anasema , mbunge Zito ni wa Kigoma!!!!

Kuna ubishi ambao hauna msingi , ili mradi kuonekana unabisha,
 
Kwenye utafiti kama huu, ni watu wachache tu, sio rahisi uwahusishe watanzania wote, ama sivyo itakuwa uchaguz wa rais.

Pili hii haina ubishi wala hailazimishi kila mtu akubaliane nao.

So, wote mnaopinga, aidha mfanye zenu, kuna mtu anasema bunge la Tanzania halina wabunge kabisa!!!! yet anasema , mbunge Zito ni wa Kigoma!!!!

Kuna ubishi ambao hauna msingi , ili mradi kuonekana unabisha,

well said mkuu.Mbona REDET wanaposema JK ni rais bora kabisaaaa toka tanzania ipate uhuru kwani ilihusisha watanzania wote?thinkimng ya miafrika iko biased and one sided sana..
 
Waberoya,
Mkuu punguza jazba hii kitu haikukaa sawa kabisa. Hata Redet wana afadhari mara 10 ya kitu hii maanake hatuwezi kumpongeza Zitto kwa sababu tu yeye ni wa kwanza na amepata kura asilimia 25 yaani kati ya watu 100 ni 24 tu waliompitisha. haya ni matusi makubwa kwa kiongozi huyo.
Na ukitazama mwisho wa hizo kura utaona kisanduku kinachosema DKNone chenye asilimia 24..nikichukulia pengine ndio kusema Hakuna mbora which includes Zitto mwenyewe..hii ni dalilimbaya sana kwa wabunge wetu, labda iwe haina maana hiyo.
Kisha tazama maswali yaliyoulizwa basi, ni vitu ambavyo vinatokana na magazeti yaani sifa ambazo tunaweza kumpa mbunge ni zile tulizozisikia toka magazetini zikilenga umaarufu wa mtu..Wangesema hivyo basi kuwa hapa tunatazama umaarufu wa mtu na sii swala la kuchaguliwa ama kufanya mazuri bungeni wakati hatufahamu kabisa nani kafanya nini bungeni zaidi ya scandals za utawala huu..
Hata hao REDET hutoa takwimu za Umaarufu wa Kikwete na kwa sababu yeye ni rais wa Tanzania nzima binafsi napokea takwimu zao kama somo hata kama kuna makosa ya utekelezaji wake. Labda nikufahamishe kidogo nilichoelewa mimi upate kuona wapi nazungumzia..
Kwanza, sifa za mbunge kulingana na point walizo score.. Ya kwanza ambayo imepata kura nyingi inasema nini?..I am not keen on the issue or the name of the minister! hii wamevote kwa asilimia 19...ipo juu kabisa ya kura zote na sijui kuna ubora gani wa kiongozi yeyote zaidi ya kutupoteza kabisa..ya pili inayofuata inasema He fights for the poor!- kivipi mkuu wangu and who are the poor! Je, ni Wananchi, Walalahoi au wanatafuta mbunge mwenye mtazamo wa siasa za Kijamaa kugawana umaskini.
Hilo tuachane nalo twende mbele zaidi..

Shuka chini ktk hesabu ya Wabunge wanaotegemewa kurudi bungeni utakuta ni asilimia 42 swali la kwanza linasema - Careless in his work, hapo wame vote kwa asilimia 22 juu ya kila kipengele cha uchaguzi wa wabunge hao watakao rudi bungeni. Mimi mkuu wangu sielewi hapa wanaposema Careless on his work, wana maana gani kiasi kwamba iwe sifa ya kwanza kumrudisha mbunge..laa sivyo ni ashirio tosha kwamba hatuna wabunge wa maana (the are all negligent) kwa asilimia hiyo 19, hii sio sifa hata kidogo..

Hata hivyo naomba darasa mkuu wangu ikiwa mimi ndio sikuelewa... karibu
 
Hiyo page iko wapi mbona siioni zaidi ya hapo juu bwana invisible ?
 
Waberoya,
Mkuu punguza jazba hii kitu haikukaa sawa kabisa. Hata Redet wana afadhari mara 10 ya kitu hii maanake hatuwezi kumpongeza Zitto kwa sababu tu yeye ni wa kwanza na amepata kura asilimia 25 yaani kati ya watu 100 ni 24 tu waliompitisha. haya ni matusi makubwa kwa kiongozi huyo.
Na ukitazama mwisho wa hizo kura utaona kisanduku kinachosema DKNone chenye asilimia 24..nikichukulia pengine ndio kusema Hakuna mbora which includes Zitto mwenyewe..hii ni dalilimbaya sana kwa wabunge wetu, labda iwe haina maana hiyo.
Kisha tazama maswali yaliyoulizwa basi, ni vitu ambavyo vinatokana na magazeti yaani sifa ambazo tunaweza kumpa mbunge ni zile tulizozisikia toka magazetini zikilenga umaarufu wa mtu..Wangesema hivyo basi kuwa hapa tunatazama umaarufu wa mtu na sii swala la kuchaguliwa ama kufanya mazuri bungeni wakati hatufahamu kabisa nani kafanya nini bungeni zaidi ya scandals za utawala huu..
Hata hao REDET hutoa takwimu za Umaarufu wa Kikwete na kwa sababu yeye ni rais wa Tanzania nzima binafsi napokea takwimu zao kama somo hata kama kuna makosa ya utekelezaji wake. Labda nikufahamishe kidogo nilichoelewa mimi upate kuona wapi nazungumzia..
Kwanza, sifa za mbunge kulingana na point walizo score.. Ya kwanza ambayo imepata kura nyingi inasema nini?..I am not keen on the issue or the name of the minister! hii wamevote kwa asilimia 19...ipo juu kabisa ya kura zote na sijui kuna ubora gani wa kiongozi yeyote zaidi ya kutupoteza kabisa..ya pili inayofuata inasema He fights for the poor!- kivipi mkuu wangu and who are the poor! Je, ni Wananchi, Walalahoi au wanatafuta mbunge mwenye mtazamo wa siasa za Kijamaa kugawana umaskini.
Hilo tuachane nalo twende mbele zaidi..

Shuka chini ktk hesabu ya Wabunge wanaotegemewa kurudi bungeni utakuta ni asilimia 42 swali la kwanza linasema - Careless in his work, hapo wame vote kwa asilimia 22 juu ya kila kipengele cha uchaguzi wa wabunge hao watakao rudi bungeni. Mimi mkuu wangu sielewi hapa wanaposema Careless on his work, wana maana gani kiasi kwamba iwe sifa ya kwanza kumrudisha mbunge..laa sivyo ni ashirio tosha kwamba hatuna wabunge wa maana (the are all negligent) kwa asilimia hiyo 19, hii sio sifa hata kidogo..

Hata hivyo naomba darasa mkuu wangu ikiwa mimi ndio sikuelewa... karibu

Mkandara,
Inawezekana unapoint lakini unashindwa kuchallenge hiyo ripoti kwa hoja kama zilivyotumika humo. Kumbuka kuwa huu ni utafiti na wala siyo hisia za mtu, kwa hiyo basi ninakushauri go back na kuchambua vianzilishi, viashiria nk vya utafiti ili ujenge hoja zenye nguvu. Kukataa utafiti bila ya kufanya utafiti sidhani kama ni sahihi.
 
wakuu sijaelewa hapa nini kinaendelea CONGRATS ZITTO KABWE for what??????/ !!!!!!!!
 
Back
Top Bottom