Contradictions zilizopo kwenye Biblia

Contradictions zilizopo kwenye Biblia

A Peculiar people

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
612
Reaction score
773
Naam natumai mu wazima.

Wengine wanaweza wakaona ni upuuzi nashauri tu ukiona huu ni upuuzi usicomment. Bila kupoteza muda ninawashirikisha katika mdajala huu unahusu Contradiction zilizopo kwenye Biblia.

Contradiction kwenye biblia inawezekana (japo binafsi sijaona) lengo langu haswa ni tuzungumze jambo hili..

Ukisoma injili zote (Mathayo, Marko, Luka na Yohana) utaona mambo haya matatu nayo ni KUZALIWA, KUFA NA KUFUFUKA kwa Yesu kristo yakiwa yamelandanda kwa asilimia zote.

Itakuwa najiuliza nataka kuzungumza nini. Ni hivi Agano la kale (kwa wale wasomaji wa biblia wataelewa) ni kivuli tu cha Agano jipya.. Na msingi mzima wa Agano jipya unajengwa katika KUZALIWA, KUFA NA KUFUFUKA kwa Yesu Kristo.Hiyo ndio injili halisi ambayo watu wanapaswa kuifahamu na kuijua. Ndio uhalisia na kweli.

Mitume walipotumwa walitumwa kuhubiri kuhusu hilo na hata leo watu wanapaswa kuifahamu. Zile ishara na maajabu hazikufanyika maajabu bila hivyo vitu vitatu. Na tunaviona katika biblia vyote vikiwa sawa.

Contradiction ambazo watu wanaziona ni zipo katika akili zao na kukosa ufahamu wa kwel.

Hivyo ningependa kushauri wote wanaopenda kuitafta kweli, muombe Mungu akusaidie kuelewa na jaribu kujiuliza haya kwanini Yesu, kwanini alikuja, kwanini afe na kwanini afufuke.
 
Back
Top Bottom