Tetesi: Corona inapukutisha watu Dar. Kuna wanaolalamika ndugu zao kuzikwa kinguvu na Mamlaka Dar huko Bahari Beach, Buza na Mbweni

Tetesi: Corona inapukutisha watu Dar. Kuna wanaolalamika ndugu zao kuzikwa kinguvu na Mamlaka Dar huko Bahari Beach, Buza na Mbweni

Umeandika ki ushabiki sana.
Tena ulicho andika hakiakisi ukweli wowote.


Me ni mkazi wa Buza (kwa mparange ) hata siku moja (tangu janga liingie ) sijawahi shuhudia ambulance ikija na maiti kuzika pale makabulini.

Ama Dar kuna Buza nyingine zaidi ya hii ninayo ishi mimi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Saa tisa usiku unakuwaga macho?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mara ya mwisho lini?

Sent using Jamii Forums mobile app
Siku 4 nyuma. Ila nilikua naongea na mama watoto juu ya hili swala leo akasema Japan kuna watoto 40 wamekutwa na corona wameambukizwa na nesi aliyekua akiwahudumia. Na hao watoto wote ni vichanga.

Sijaprove hii wala sijdoublecheck statistics tena.
 
Watafanya siri lakini wakumbuke NY walikosa sehemu za kuzikia hadi wakawa wanazika watu kwenye parks.
 
Hadi sasa tunatangaziwa kwamba watu 10 pekee ndio waliokwishafariki kutokana na COVID-19; lakini kwa mjibu wa yanayoandikwa kwenye mada hii, kuna watu wengi zaidi ya hao 10 ambao serikali imeamua kuchukua jukumu la kuwazika bila ya kushirikisha ndugu zao, ikiwa na maana kwamba kilichowaua ni COVID-19; lakini serikali haitaki ieleweke hivyo kwa sababu wanazozielewa wenyewe!

Huku kuficha kunaisaidia serikali kwa vipi?
Na hawa raia wanaofichwa taarifa hizi, lakini huko mitaani wanaona hali halisi, waichukulie serikali kivipi? Kwamba inalinda maslahi ya wananchi?

Hizi taarifa zinazofichwa, huko baadae haziwezi kufichuka; na kama zitafichuka na ukweli ukawekwa wazi, tutaendelea kuisifu serikali yetu kwa kusimamia maslahi ya nchi yetu?
Kuna viongozi watakaotakiwa kuwa 'accountable'kwa upuuzi wa aina hii? Sasa hivi wao wanaamini watakuwa kwenye madaraka milele na hata ikilazimu kuondoka, watawaweka wanaowajua kuwa watalinda maslahi yao.

Maswali ni mengi.
Mkuu,hoja yako ingeeleweka sana kama hili jukwaa lingekuwa lile la mwaka 2006-2010.Sahizi Jamiforums watu hawatoi Facts,bali mihemko.HAKUNA ALIYEPINGA KUWA DATA ZIMEFICHWA,BALI UNACHOHITAJI NI USHAHID WA HII HOJA.Bado wanakubishia tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mada kama hii yako ni ngumu mno kuiamini, na wala haiingii kabisa akilini.
Kukiwa na ukweli wowte juu ya haya uliyoandika hapa, basi hakuna serikali iliyowekwa madarakani na wananchi. Badala yake, kutakuwa na kitu kingine kabisa ambacho sina jina la kukipa.

Kuleta mada kama hii, halafu pasiwepo na aina yoyote ya ushahidi unaoipa mada uzito, angalau hata wa kimazingira tu, ni kulifedhehesha hili jamvi la JF.

Hii ni hatari sana kama kuna aina yoyote ya ukweli kwenye mada yako.
Omba Mungu afe ndugu yako kipindi hichi ndipo utaamini anayoyasema mleta Mada, naona unaubishi wa asili, sijui ulitaka akuletee video??
 
Hivi viongozi wetu, Ummy, Majaliwa na Magufuli mnatuchukuliaje sisi wananchi kwa kutudanya na kutupatia takwimu za uongo kiasi hicho?.

Hivi mnadhani mnafanya kazi peke yenu?, mnafikili hao mnaofanyanao kazi ndugu zetu hawatuambii ukweli juu ya yanayoendelea.

Endeleeni kudanganya mchana kweupe ili muendelee kujivua nguo kwa ujinga usiofichika!.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jans nimemuona jamaa ksangika mbele ya kituo cha polisi central na kulikuwa na polisi kama 40 wamemzunguka kwa mbali sana!
 
"Dar es Salaam lazima kuwe na wagonjwa wengi na vifo vingi kutokana statistically kuna Population kubwa".Hii kauli ni ya Mamlaka

Ukweli huogopesha lakini bora usemwe,Corona maeneo ya Dar es Salaam inamaliza watu, Hakuna mwandishi au gazeti ambalo linaweza kuhoji familia hizi zinazolia kila siku kwa kutowaona wapendwa wao wanaozikwa kimya kimya na Mamlaka

Kauli za kupeana Morali kuwa watu wachape kazi waongeze pato la Taifa Dar es Salaam litamsaidia nani? Hizi familia ambazo ndugu zao wanazikwa kwa kuugua corona zina mateso makali sana.

Watu maarufu na wenye ushawishi kwenye mamlaka na jamii ndio hao wanazikwa na watu wasiozidi ishirini au kumi, Je wewe kabwela ambae hutambuliki na mamlaka omba yasikukute

Uchunguzi ufanyike nini kinachoendelea maeneo ya makaburi ya huko Bahari Beach eneo la kondo,Buza na Mbweni

Uchunguzi ufanyike ongezeko la kelele za ambulance kwa wingi maeneo ya Dar es salaam kutoka hospital kuelekea maeneo hayo ni wangapi wanazikwa kwa janga hili

Tunakubaliana vita inahitaji umorali na nguvu lakini hili ni gonjwa sio vita linahitaji tiba tahadhari na ukweli

Leo hii kuna malalamiko makubwa watu wakifuatilia ndugu zao hospitali waliolazwa wanajibiwa alishafariki na kuzikwa na mamlaka kimya kimya,

Mamlaka imeamuru wizara ya afya ijibu kuwa sio kila mgonjwa hufa kwa corona ni kweli.Je kwanini wanazikwa na mamlaka bila hata ndugu kuhusishwa bali hujibiwa ndugu yenu alishazikwa amefariki

Wizara ya afya ni bora mkaongea ukweli ili watu wachukue tahadhari kuliko sasa mnapojaribu kuuma na kupuliza,

Paul Makonda alikuwa anapuliza na kufariji watu wachape kazi lakini visa vya watu kupukutika na corona sasa amebadili kauli na kuamua kuwa mkweli kuwa Dar corona inamaliza watu

Mamlaka kila siku inakuja na kauli kinzani kama corona sio ishu kwanini mnafunga shule Tanzania nzima, Ruhusuni baadhi ya mikoa elimu iendelee isipokuwa Dar na Zanzibar

Wanakijiji wasiojielewa na baadhi ya wapiga pambio wao hawachuji kauli za mamlaka, Hii itapelekea watu kuwa na morali na kupukutika zaidi
Watu wenye midomo mirefu bila kuthibitisha kama wewe hua nawachukulia kama ni WEHU,sijui umetumwa na wanasiasa!!! hv kwa nini waTanzania hua mnapenda kuongea ongea tu?au nyie wengine siyo waTanzania mko huko nje ila mnalipwa na wanasiasa ili mje mropoke chochote kama kuichafua serikali

JAH Rastafari Morning Africa.Trust JAH respect nature
 
Mkuu, watu kama huyu mtoa post ndio Rais Magufuli amewaagiza TCRA na Polisi wawachukulie hatua. Wakikamatwa labda ndio watatuonesha hayo makaburi na hizo familia zinazolia.

Kama huna ndugu au rafiki aliyekufa ni busara kufunga mdomo wako......
Hata kama uko kazini tumia busara ..watu wana machungu....
 
Unajua mkuu 'Chuma cha Mjerumani', sikukatalii kamwe hayo unayosema, kwa sababu sina njia ya kukataa kuwa hayatokei.
Kinachonistua tu ni hicho cha serikali, kama kweli inafanyika hivyo.

Kama haya yaliyoandikwa kwenye mada yanafanyika, tena yakifanywa na serikali na kwa maksudi kabisa serikali hiyo ikificha watu wasijue kuwa yanafanyika..., hilo ndilo linalonitatiza sana mie.

Jana Tena nilipishana na ambulance inaenda maeneo hayo hayo nilikuwa busy sikufwatilia kilicho jiri ila ambulance yenye wahudumu huwa haiendi mahali bila kuitwa na Kama nimtu kaziidiwa huwa magari yapo ata Kama mgonjwa Hana gari jirani anajitolea. Ukiona mtu kwake anayo magari anaumwa anakuja kuchukuliwa na ambulance na week iliyopita wawili walienda eneo Hilo Hilo unajiongeza tuu .
 
"Dar es Salaam lazima kuwe na wagonjwa wengi na vifo vingi kutokana statistically kuna Population kubwa".Hii kauli ni ya Mamlaka

Ukweli huogopesha lakini bora usemwe,Corona maeneo ya Dar es Salaam inamaliza watu, Hakuna mwandishi au gazeti ambalo linaweza kuhoji familia hizi zinazolia kila siku kwa kutowaona wapendwa wao wanaozikwa kimya kimya na Mamlaka

Kauli za kupeana Morali kuwa watu wachape kazi waongeze pato la Taifa Dar es Salaam litamsaidia nani? Hizi familia ambazo ndugu zao wanazikwa kwa kuugua corona zina mateso makali sana.

Watu maarufu na wenye ushawishi kwenye mamlaka na jamii ndio hao wanazikwa na watu wasiozidi ishirini au kumi, Je wewe kabwela ambae hutambuliki na mamlaka omba yasikukute

Uchunguzi ufanyike nini kinachoendelea maeneo ya makaburi ya huko Bahari Beach eneo la kondo,Buza na Mbweni

Uchunguzi ufanyike ongezeko la kelele za ambulance kwa wingi maeneo ya Dar es salaam kutoka hospital kuelekea maeneo hayo ni wangapi wanazikwa kwa janga hili

Tunakubaliana vita inahitaji umorali na nguvu lakini hili ni gonjwa sio vita linahitaji tiba tahadhari na ukweli

Leo hii kuna malalamiko makubwa watu wakifuatilia ndugu zao hospitali waliolazwa wanajibiwa alishafariki na kuzikwa na mamlaka kimya kimya,

Mamlaka imeamuru wizara ya afya ijibu kuwa sio kila mgonjwa hufa kwa corona ni kweli.Je kwanini wanazikwa na mamlaka bila hata ndugu kuhusishwa bali hujibiwa ndugu yenu alishazikwa amefariki

Wizara ya afya ni bora mkaongea ukweli ili watu wachukue tahadhari kuliko sasa mnapojaribu kuuma na kupuliza,

Paul Makonda alikuwa anapuliza na kufariji watu wachape kazi lakini visa vya watu kupukutika na corona sasa amebadili kauli na kuamua kuwa mkweli kuwa Dar corona inamaliza watu

Mamlaka kila siku inakuja na kauli kinzani kama corona sio ishu kwanini mnafunga shule Tanzania nzima, Ruhusuni baadhi ya mikoa elimu iendelee isipokuwa Dar na Zanzibar

Wanakijiji wasiojielewa na baadhi ya wapiga pambio wao hawachuji kauli za mamlaka, Hii itapelekea watu kuwa na morali na kupukutika zaidi

Nimesoma hii post yako..
Wakati nasoma nikategemea utasema familia ya fulani wa sehemu fulani, walikuwa na mgonjwa..fulani.. kwenye hospitali fulani. Amefuatiliwa na taarifa zinaonesha amefariki na kuzikwa katika makaburi unakotaja.

Ni post inasema kitu kikubwa lakini ni hisia tu.
Sasa mkichukuliwa mkathibitishe inakuwa shida baadae, shida ya kutosha tu.
 
Watu wabishi kweli yani. Alichoandika mtoa mada na niliyoshuhudia kuna ukweli 90%.
Sio kilakitu mbishe. Kama mtu hauamini basi unachill tuu. Watakaoconsider hiyo habari then watafikirisha akili zao kujua nn kinachoendelea kuhusiana na huu ugonjwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ukweli inatakiwa uwe 100%.Ukweli hautakiwi kuwa pungufu

Senti bai yuzingi tecno T301
 
Back
Top Bottom