Corona: Mapungufu na madhahifu ya Magufuli katika Mapambano dhidi ya Corona

Corona: Mapungufu na madhahifu ya Magufuli katika Mapambano dhidi ya Corona

joto la jiwe

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2017
Posts
26,117
Reaction score
46,617
Ni ukweli kwamba jina la Magufuli limezidi kufahamika zaidi duniani tangu ulipozuka ugonjwa wa Corona na kuingia hapa Africa na hususan Tanzania. Magufuli aligonga vichwa vya habari duniani kwa uzuri na ubaya katika viwango vyenye kukaribiana.

Mwanzoni tu ugonjwa ulipoingia Tanzania, Magufuli alianza kupata shutuma na kurushiwa kila aina ya kebehi na matusi pale alipoamua kuruhusu ibada na kukataa kufunga mipaka ya ndani na nje ya nchi yake.

Kikomo cha kukashifiwa kilifika kileleni pale Magufuli alipokwenda kanisani na kurudia kusema kwamba, hatozuia wala kufunga nyumba za ibada kwa sababu anaamini virusi haviwezi kuishi na kuwadhuru watu Mungu.

Mara tu ya kumaliza kusema hivyo, dunia nzima ilimshukia na kumlaani Magufuli kwa kuchukua misimamo tofauti na nchi zote duniani, kwa kweli haikua rahisi sana kuvumilia kwa jinsi dunia ilivyomgeukia Magufuli, inahitaji mtu mwenye ujasiri wa pekee kuvuka bila kubadilisha msimamo baada ya kulaaniwa na dunia nzima.

Wakati dunia haijamaliza kulaani misimamo ya Magufuli ya kuruhusu nyumba za ibada na kutofunga mipaka ya nchi, Magufuli akaibuka na hili la kutilia shaka kuhusu vipimo vya Corona, ghafla jina lake likazidi kuwa gumzo duniani kote, ila safari hii sio kwa kukashifiwa na kukejeliwa, ila kwa kusifiwa na kupongezwa, sasa nchi, watu na makundi mbalimbali yamesahau jinsi yalivyomkashifu na kumuona mtu wa ajabu, sasa wanamuita ni mtu jasiri, makini na mwenye misimamo isiyoyumbishwa.

"Negative Energy"

Vyovyote vile iwavyo, ama kwa kusifiwa au kwa kupongezwa, kwangu ninahisi hayo yote aliyofanya Magufuli ni Mapungufu zaidi katika mapambano dhidi ya Corona kuliko kuimarisha na kuboresha mapambano.

1)Kuwaruhusu watu kuendelea kukusanyika katika Nyumba za ibada bila kutoa maelekezo na mifumo ya kufuatilia kuhakikisha kwamba maelekezo yanafuatwa, huo ni upungufu mkubwa has a ikizingatiwa kwamba, huko Rome na Makka kwenye vitovu vya dini hizi mbili, wamesitisha ibada baada ya kupoteza waumini wao.

2)Kitendo cha kuweka nguvu kubwa katika imani ya dini na dawa za asili na kutotilia mkazo katika maelekezo ya kitaalamu ya kuzuia maambukizi, ni kosa na Mapungufu makubwa.

3)Kuzuia na kukejeli unyunyiziaji wa dawa mijini na sehemu mbalimbali zenye mikudanyiko kwa madai ya kwamba haziui Corona, sio sawa kwa sababu zilisaidia kuua Mbu wanaosababisha Malaria na Dengue, alipaswa kuwashauri waongeze dawa yenye kujua virusi vya Corona (Sabuni au Alcohol).

4)Kutafuta na kujua ukweli dhidi ya Mapungufu ya vipimo vinavyotumika kupima Corona bila kutoa maelekezo ya nini kifanyike katika hiki kipindi ambacho vyombo mbalimbali vinachunguza, ni kuiacha nchi hewani huku wananchi wakiwa hawaelewi hali ya maambukizi inavyokwenda nchini.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku zote si rahisi kumuelewa mtu aliye tofauti. Ukweli ni kwamba tunahitaji watu kama hawa ili tuweze kuwa na maendeleo ya kweli, lakini si viongozi wanaonata na beat, yaani wale wanaoenda na upepo unavyoenda.

Binafsi huwa nawapenda watu wanao challenge
 
Siku zote si rahisi kumuelewa mtu aliye tofauti..ukweli ni kwamba tunahitaji watu kama hawa ili tuweze kuwa na maendeleo ya kweli,lakini si viongozi wanaonata na beat,yaani wale wanaoenda na upepo unavyoenda

Binafsi huwa nawapenda watu wanao challenge
Challenge sio mbaya ila iwe na mantik sio kuchallenge ili mradi huku ukihatarisha maisha ya wengine wewe ukiwa mafichoni.
 
Challenge sio mbaya ila iwe na mantik sio kuchallenge ili mradi huku ukihatarisha maisha ya wengine wewe ukiwa mafichoni.
We unaleta siasa hapa. Ni kitu cha ajab Watanzania woooote wamekuwa wana siasa!!!
Magufuli pia ni mtanzania kama wewe,hata wewe pia ulikuwa na uwezo wa kukimbilia kwenu njilinji!!!!.
Serikali yake pia imetoa nafasi kwa wenye uwezo wa kujifungia ndani,wajifungie...wasio na uwezo waendelee na mishe zao,simple tu,serikali inajua hali za wananchi wake,kwa uhalisia! na si kwa kufuata mkumbo..ni mtu asiyekuwa na akli timamu anayeweza kushangilia lockdown

Pia unasema challenge ya magufuli haina mantiki!! Fuatilia mambo; usiingie kwenye mkumbo wa siasa uchwala, testing kits are now questionable all over the world!
 
joto la jiwe,

Mzee suala la kunyunyizia dawa alipinga the use of chlorine kupunguza maambukizi! Mimi binafsi naona alikuwa sawa maana kupigana na coronavirus inahitaji science approach chlorine haiui virus wa aina yeyote ile! Na kama ingekuwa any sort of alcohol disinfectant spraying asingepinga! Maamuzi yake yalikuwa ku-save already meager resources from misappropriation.

Pili amekuwa akisema hazuii shuguli za uzalishaji mali kipindi cha maambukizi coronavirus lakini amekuwa akisisitiza social distancing, hand washing and masks! Mzee usijidanganye hata nchi zilizoendelea hazijaweza kuepuka hilo yaani kuhimiza kazi ziendelee, maana huu ugonjwa haijulikani lini utaisha, some darwinism scientific theories claim of natural selection until after people build natural immunity! Tatizo lake kubwa Mkulu ni utashi wa kisiasa na linaonekana kwa kutoweza kuzuia mikusanyiko nyumba za Ibada out of imani of which inaeleweka haswa pale mtu anapohepa kukataza shuguli za kupata kipato halafu akazuia mikusanyiko nyumba za ibada. Ila still hata huko kuna msisitizo wa social distancing, hand washing and masks. BTW kumbuka uchaguzi ni hapo October.

Tatu, kuhusu testing kits mi binafsi nimeona confusion, japokuwa tests kits za kutoka Uchina ziko proven kuwa na defaults, approach aliyotumia is too shallow and revealed of politics at play kulinda serikali yake. Kama unafuata scientific protocols katika kufanya any test analysis basi methods na procedure alizotumia, pili investigation/evaluation ya Result na mwisho conclusion yake would have counted him out.Truth to be told, they had to be more scientific explanation out those tests he conducted n he should have used experts at his disposal before coming out in the media like that! In science false positives are always possible in any laboratory test/experiment depending on methods/procedures used, a reason there r always written procedures/methods/guidelines to test anything in labs short of that the results though positive/negative will turn out to be invalid!

Mwisho, i would be happy kama angepunguza mihemko na tabia ya ku-discredit vitu out of no valid basis! Kwa mfano kutumia cheap jabs kama kutumwa na mabeberu inamfanya kuonekana yupo undiplomati, shallow na hana exposure. Pili sihafiki kusimamishwa ama kufukuzwa kazi kwa Dr. Nyambura Moremi, she more than qualified kuendelea kuongoza taasisi ile na kama kuna matatizo na kits basi makose ni ya waliozinunua (i guess MSD). Na kwa namna alivyo-deal na Dr. Nyambura sidhani kama anayemfuata atatoa matokeo halali, in short she has been treated unfairly and Magufuli decision lacks merit and is unethical one!
 
We unaleta siasa hapa...ni kitu cha ajab watanzania woooote wamekuwa wana siasa!!!
Magufuli pia ni mtanzania kama wewe,hata wewe pia ulikuwa na uwezo wa kukimbilia kwenu njilinji!!!!.
Serikali yake pia imetoa nafasi kwa wenye uwezo wa kujifungia ndani,wajifungie...wasio na uwezo waendelee na mishe zao,simple tu,serikali inajua hali za wananchi wake,kwa uhalisia! na si kwa kufuata mkumbo..ni mtu asiyekuwa na akli timamu anayeweza kushangilia lockdown
Kumbe ni praise team.
Huwezi kuambia watu ni kaugonjwa kadogo wakati wewe umejidicha. Kama magonjwa mengine tushayazoea na saivi tunaishi nayo, basi lead by example, toka mafichoni! Vinginevyo nyie praise team ndo mnaleta siasa.
Pia unasema challenge ya magufuli haina mantiki!!???..fuatilia mambo kijana usiingie kwenye mkumbo wa siasa uchwala,testing kits are now questionable all over the world!
Unaniambia nifatilie mambo wakati wewe mwenyewe umeshindwa. Ukifatilia hao wanaolalamikia test kits, wanacholalamikia ni low sensitivity ya hizo kits kwa maana nyingine zinatoa negative kwa wenye positive. Ukisikilizahotuba yake, alicholalamikia ni positive kua nyingi! Angekua objective angehoji zaidi hata negatives.
 
Mzee suala la kunyunyizia dawa alipinga the use of chlorine kupunguza maambukizi! Mimi binafsi naona alikuwa sawa maana kupigana na coronavirus inahitaji science approach chlorine haiui virus wa aina yeyote ile! Na kama ingekuwa any sort of alcohol disinfenctant asingepinga! Maamuzi yake yalikuwa ku-save resources.
Kiongozi ni mtu wa kutoa solutions sio kupoint out shortfalls. Sawa chlorine ni upuuzi mtupu basi avail resources za kutumia hiyo alcohol.

Kwa mfano kwenye vituo vya mwendokasi, waliokua wananawisha kwenye vituo vidogo wengi wameacha kazi coz kazi ya kufata ndoo za maji na kunawisha kwa sabuni ni kazi kubwa kulingana na malipo. Kinachoendelea saivi watu wananawa kwenye vituo vikubwa tu kama kimara, ubungo na fire. Wanaopandia vituo vidogo hawanawi. Makes no sense!
 
Katika unyunyizaji wa dawa mijini kosa alilofanya ni kukebehi lile zoezi na kuliita ni upuuzi mtupu, hilo alifanya kosa kubwa kwa sababu ya

1) Unyunyizaji wa dawa pamoja na kwamba alisema hauna uwezo wa kuuwa virusi(Japo sina uhakika kama ni kweli), lakini lilikua linaua Mbu na wadudu wengine wenye kusababisha vifo na magonjwa mengi zaidi kuliko Corona, yeye mwenyewe alikiri kwamba bado Malaria inaendelea kuua watanzania wengi kuliko Corona, vipi unasema zoezi la kuua Mbu ni upuuzi?

2)Alipaswa kutumia hili zoezi la kunyunyiza dawa ambalo lilianza kwa kasi sana, kama "stepping stone" kwa kuwaambie watafute dawa inayouwa virusi, kama vile sabuni ya maji iwe ni miongoni mwa dawa zinazotumika ili tuweze kupambana na magonjwa mengi kwa wakati mmoja, ikiwezekana, hata baada ya kumalizika kwa Corona, unyunyizaji wa dawa mijini uendelee, kumbuka tunasumbuliwa sana na Malaria, Dengue, na Inzi.

Kwa ufupi lile zoezi halikua la kipuuzi lenye kustahili kudhalilishwa kwa wahusika waliolibuni na kulisimamia, Aliwadhalilisha sana na kuwavunja nguvu. Huko Wuhan ambako wamefanikiwa kumaliza maambukizi, walikua wakinyunyuza dawa mitaa yote, ninauhakika walikua wakinyunyiza kwa lengo la kuua virusi vya Corona, kwanini asiulize na kuagiza hiyo dawa waliyotumia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiongozi ni mtu wa kutoa solutions sio kupoint out shortfalls. Sawa chlorine ni upuuzi mtupu basi avail resources za kutumia hiyo alcohol.
Kwa mfano kwenye vituo vya mwendokasi, waliokua wananawisha kwenye vituo vidogo wengi wameacha kazi coz kazi ya kufata ndoo za maji na kunawisha kwa sabuni ni kazi kubwa kulingana na malipo. Kinachoendelea saivi watu wananawa kwenye vituo vikubwa tu kama kimara, ubungo na fire. Wanaopandia vituo vidogo hawanawi. Makes no sense!
Kwa hiyo kwa upumbavu wako tuendelee kutumia chlorine (isiyosaidia) kwa vile hamna alternative ya kusi-disinfect mitaa at whose cost? BTW kunawa haimaanishi a sure way na si lazima kunawishwa mikono it has to be everyone's personal responsibility! a behavioral approach! Kwani mbona huko kwenye maambukizi madogo hamna watu kwa ajili ya kunawisha mikono wengine? Kwangu mimi hii si valid excuse ya ku-blame serikali!
 
Kwa hiyo kwa upumbavu wako tuendelee kutumia chlorine (isiyosaidia) kwa vile hamna alternative ya kusi-disinfect mitaa at whose cost? BTW kunawa haimaanishi a sure way na si lazima kunawishwa mikono it has to be everyone's personal responsibility! Kwani mbna huko kwenye maambukizi madogo hamna watu kwa ajili ya kunawisha mikono wengine? Kwangu mimi hii si valid excuse ya ku-blame serikali!
Let me assume hujanielewa.
 
Let me assume hujanielewa....
Nimekuelewa sana kule Dubai walipopuliza alcohol disinfectanct what's the result? To fight huu ugonjwa, it has to do with behavioral approaches! Short of that hamna kitu!
 
Kumbe ni praise team.

Huwezi kuambia watu ni kaugonjwa kadogo wakati wewe umejidicha. Kama magonjwa mengine tushayazoea na saivi tunaishi nayo, basi lead by example, toka mafichoni! Vinginevyo nyie praise team ndo mnaleta siasa.

Unaniambia nifatilie mambo wakati wewe mwenyewe umeshindwa. Ukifatilia hao wanaolalamikia test kits, wanacholalamikia ni low sensitivity ya hizo kits kwa maana nyingine zinatoa negative kwa wenye positive. Ukisikilizahotuba yake, alicholalamikia ni positive kua nyingi! Angekua objective angehoji zaidi hata negatives.
We hujitambui
Jibu positive kwa oil ya gari inashindikana vipi kuwa positive kwenye sample ambayo ni negative?

Bado hatujawa na hoja ya msingi ya kuita corona ni ugonjwa mkubwa kwa afrika,labda ulaya huko,napo kwa sasa si tishio tena,kila mmoja anatamani mipaka ifunguliwe waishi kama awali yaani kama alivyofanya magufuli tu, kwa sababu mmekuwa mkitupa wiki 2 tangu mwezi wa tatu,na hadi leo ni wiki takribani 5 ile idadi yenu ya vifo mlivyokadiria hamjaipata hata robo,ni kiasi gani mmekosa weredi kama hivyo vifaa vyenu,kwa bahati mbaya mko mnakosoa mtu aliye sahihi,poleni sana!ukweli haufichiki,unajidhihirisha wenyewe


Au mnatupa wiki 2 nyingine?
 
Nimekuelewa sana kule Dubai walipopuliza alcohol disinfectanct what's the result? To fight huu ugonjwa, it has to do with behavioral approaches! Short of that hamna kitu!
Mkuu behavioral approaches ni long term strategies, ambazo hazisaidii sana katika "acute diseases" kama Corona. Hapa ni lazima kufanyike " short and intensive strategies hata kama ni gharama kubwa ili mradi ziwe zinaleta matokeo chanya.

Walichofanya Uganda kimewasaidia sana, japo walipoteza pesa nyingi sana kwa kununua na kusambaza chakula, kusimamisha uchumi kwa siku 21, lakini imeokoa maisha mengi ya waganda, sasa hivi Uganda ndio ipo katika position nzuri ya kuanza " behavioral approaches", wameshapita katika "acute stage of the disease".

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee suala la kunyunyizia dawa alipinga the use of chlorine kupunguza maambukizi! Mimi binafsi naona alikuwa sawa maana kupigana na coronavirus inahitaji science approach chlorine haiui virus wa aina yeyote ile! Na kama ingekuwa any sort of alcohol disinfenctant spraying asingepinga! Maamuzi yake yalikuwa ku-save already meager resources from misappropriation.

Pili amekuwa akisema hazuii shuguli za uzalishaji mali kipindi cha maambukizi coronavirus lakini amekuwa akisisitiza social distancing, hand washing and masks! Mzee usijidanganye hata nchi zilizoendelea hazijaweza kuepuka hilo yaani kuhimiza kazi ziendelee, maana huu ugonjwa haijulikani lini utaisha, some darwinism scientific theories claim of natural selection until after people build natural immunity! Tatizo lake kubwa Mkulu ni utashi wa kisiasa na linaonekana kwa kutoweza kuzuia mikusanyiko nyumba za Ibada out of imani of which inaeleweka haswa pale mtu anapohepa kukataza shuguli za kupata kipato halafu akazuia mikusanyiko nyumba za ibada. Ila still hata huko kuna msisitizo wa social distancing, hand washing and masks. BTW kumbuka uchaguzi ni hapo October.

Tatu, kuhusu testing kits mi binafsi nimeona confusion, japokuwa tests kits za kutoka Uchina ziko proven kuwa na defaults, approach aliyotumia is too shallow and revealed of politics at play kulinda serikali yake. Kama unafuata scientific protocols katika kufanya any test analysis basi methods na procedure alizotumia, pili investigation/evaluation ya Result na mwisho conclusion yake would have counted him out.Truth to be told, they had to be more scientific explanation out those tests he conducted n he should have used experts at his disposal before coming out in the media like that! In science false positives are always possible in any laboratory test/experiment depending on methods/procedures used, a reason there r always written procedures/methods/guidelines to test anything in labs short of that the results though positive/negative will turn out to be invalid!

Mwisho, i would be happy kama angepunguza mihemko na tabia ya ku-discredit vitu out of no valid basis! Kwa mfano kutumia cheap jabs kama kutumwa na mabeberu inamfanya kuonekana yupo undiplomati, shallow na hana exposure. Pili sihafiki kusimamishwa ama kufukuzwa kazi kwa Dr. Nyambura Moremi, she more than qualified kuendelea kuongoza taasisi ile na kama kuna matatizo na kits basi makose ni ya waliozinunua (i guess MSD). Na kwa namna alivyo-deal na Dr. Nyambura sidhani kama anayemfuata atatoa matokeo halali, in short she has been treated unfairly and Magufuli decision lacks merit and is unethical one!


Geza, we ni mwanangu wa siku nyingi sana. Ukweli usemwe, wewe ulikua ki-aina ukimpigia debe Lowassa.

Pili, Unampinga sana Magufuli kwenye maamuzi yake mengi na hasa anayotoa public.

Ukumbuke, Makinikia yalipozuiliwa kulikua na timu kubwa ya wataalam walio chunguza mzigo ule, halikua jambo la kujifanyia.

Sasa, most of the time, usiitaji watu wafanye or kutoa maelezo vile yatakonga nyoyo yako. Wewe ni msomi, kama alivyo yeye pia.
 
Geza, we ni mwanangu wa siku nyingi sana. Ukweli usemwe, wewe ulikua ki-aina ukimpigia debe Lowassa.

Pili, Unampinga sana Magufuli kwenye maamuzi yake mengi na hasa anayotoa public.

Ukumbuke, Makinikia yalipozuiliwa kulikua na timu kubwa ya wataalam walio chunguza mzigo ule, halikua jambo la kujifanyia.

Sasa, most of the time, usiitaji watu wafanye or kutoa maelezo vile yatakonga nyoyo yako. Wewe ni msomi, kama alivyo yeye pia.
Ngoja tuone mzee! Ila sikuwa upande wa Lowassa mie! Magufuli mropokaji na hilo linaleta maadui wengi!
 
ngoja tuone mzee! Ila sikuwa upanda wa Lowassa mie! Magufuli mropokaji na inaleta maadui wengi!

Maadui ni lazima hasa kwenye sistim ambayo ilikua ya upigaji.

Kwenye taasisi ya urais, mtu mwenye kupata all sort of inteligensia ripoti kila kukicha, kumuita mropokaji sidhani ni sahihi.

Naamini, yapo mengi sana nyuma ya pazia ambayo hayawezi semwa hadharani.

Kwamfano: Rais ana maongezi ya ana-kwa-ana na Rais wa China inayoshutumiwa vikali. Unajua maongezi ya kiintelijensia kati ta serikali hizi, nini China inasema kuhusu huu ugonjwa na misimamo yake?

USA wamekazana kua huu ugonjwa umetoka Laboratory China, yes or not - ila huu ni ugonjwa wa kupika.

Kuna mengi nyuma ya pazia.
 
Maadui ni lazima hasa kwenye sistim ambayo ilikua ya upigaji.

Kwenye taasisi ya urais, mtu mwenye kupata all sort of inteligensia ripoti kila kukicha, kumuita mropokaji sidhani ni sahihi.

Naamini, yapo mengi sana nyuma ya pazia ambayo hayawezi semwa hadharani.

Kwamfano: Rais ana maongezi ya ana-kwa-ana na Rais wa China inayoshutumiwa vikali. Unajua maongezi ya kiintelijensia kati ta serikali hizi, nini China inasema kuhusu huu ugonjwa na misimamo yake?

USA wamekazana kua huu ugonjwa umetoka Laboratory China, yes or not - ila huu ni ugonjwa wa kupika.

Kuna mengi nyuma ya pazia.
Mimi ninadhani tusiumize vichwa kwa kujadili kuhusu USA au China, sisi tumjadili Magufuli kwa anayefanya hapa nyumbani katika kukabiliana na Corona, tujadili yale tunayoyaona, kuyasikia na kuona yanayotokea, je tunadhani ni muafaka na sahihi?, kwasababu ndio yatakayotuokoa ama kutuangamiza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ninadhani tusiumize vichwa kwa kujadili kuhusu USA au China, sisi tumjadili Magufuli kwa anayefanya hapa nyumbani katika kukabiliana na Corona, tujadili yale tunayoyaona, kuyasikia na kuona yanayotokea, je tunadhani ni muafaka na sahihi?, kwasababu ndio yatakayotuokoa ama kutuangamiza.

Sent using Jamii Forums mobile app


Wakati tukijadili hayo, ni ngumu kutojadili hayo mengine (China-USA) kwa sababu, ni mambo ambayo yanainfluensi maamuxi mengi yanayochukuliwa chini kwa chini.
 
Mimi ninadhani tusiumize vichwa kwa kujadili kuhusu USA au China, sisi tumjadili Magufuli kwa anayefanya hapa nyumbani katika kukabiliana na Corona, tujadili yale tunayoyaona, kuyasikia na kuona yanayotokea, je tunadhani ni muafaka na sahihi?, kwasababu ndio yatakayotuokoa ama kutuangamiza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Magufuli ako sawa, full stop

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati tukijadili hayo, ni ngumu kutojadili hayo mengine (China-USA) kwa sababu, ni mambo ambayo yanainfluensi maamuxi mengi yanayochukuliwa chini kwa chini.
Ukishaingiza neno la chini kwa chini, unatoa nafasi ya mtu kuzungumza lolote na utashindwa kumuomba akupe ushahidi, kwa sababu atakimbilia kujificha katika kichaka cha "chini kwa chini".

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom