Corona: Tusinyoosheane vidole. Kama unaweza kusaidia, please do. Usisubiri uombwe - jitokeze saidia, vinginevyo nyamaza!

This is what is gonna happen within the next month

Paracetamol zitaadimika

Wagonjwa watalalamika

Serikari itasema kawaida huwa wanaoda kutokana na historical data za matumizi na MSD walikuwa na stock ya kutosha.

Lakini wanakubali kuna uhaba umesababishwa na gonjwa la Korona na wameshatoa order zipo njiani (kufika hadi kusambazwa kama mwezi)

A lot of people will suffer kwa muda huo na pengine kupoteza maisha kwa sababu ya uzembe na kukosa mipango.

I take wagers on that occurrence
 
Naweza kusaidia kwa kutangaza kuwa Dar imefungwa rasmi from today,no kuingia no kutoka?
 
bro unaongea ukweli ila wanao laumiwa si wapo? wamejifungia huko mafichoni ? wamekimbia vita na wao walituaminisha corona ni kama wapinzani? kwamba ni kakitu kadogo sana tuchape kazi? sasa watoke huko waje watubu, waongoze mapambano
 

Pascal, Wewe ni culprit No 1, uliyekuwa unabeza COVID -19. Sasa utahukumiwa kwa yote uliyo yaaandika kubeza hii virus. Kuna watu humu ni virus SURVIVORS na effects zake, walionya, na wewe kwa ncha ya peni yako/keyboard na ubongo wake kwa makusudi kabisa ukawa unapotosha. Understand that, wewe ni "Journalist" uliyebobea kwa "standard ya Tanzania", na unao followers wengi sana. Kwa hiyo tu lazima ubebe mzigo wa yote uliyo yaandika, hata baada ya kuonywa.
 
Tusaidie kwanza kujua tunamshauri nani hasa Kati ya waziri wa afya,waziri mkuu au rais? Maana mmoja kati ya hao alishatangaza kabisa kwamba ukimshauri ndo umepoteza,sasa ili tusipoteze muda wetu be specific,TUNA MSHAURI NANI?
 
Mkuu wababa wa aina hiyo huku kwenye nchi ya wadanganyika,wanaitwa wametoka kwa Mungu ili waje kuwakomboa watoto wao walioteswa na Simba kwa muda mrefu
 
Naweza kusaidia kwa kutangaza kuwa Dar imefungwa rasmi from today,no kuingia no kutoka?
Huwezi kusaidia kwa kutangaza hivyo kwasababu wewe huna mamlaka hayo, bali unaweza kusaidia kwa kutoa ushauri kwa wenye mamlaka watangaze kuifunga Dar, kisha unatoa sababu zako za kwanini tuifunge Dar, na kama tukiifunga Dar, hatua hiyo itasaidiaje kupunguza maambukizi, na pia kushauri tukiifunga Dar, hakuna kutoka wala kuingia, pia ushauri wale wote wanaoendesha maisha yao wa kila siku kwa kutoka au kuingia Dar, wataendeshaje maisha yao?.
P
 
Note: ni MS not SM!.
P
 
Hatuwezi kutafuta suluhu ya tatizo hili kwa kutumia akili zile zile zilizotufikisha hapa tena kwa makusudi,Jana nimeona tangazo moja TBC kabla ya habari ya saa mbili rais akihimiza watu kuwa wakati watu wengine kwenye mataifa mengine wamejifungia ndani sababu ya corona basi sisi tuchape
kazi sana
 
Tusaidie kwanza kujua tunamshauri nani hasa Kati ya waziri wa afya,waziri mkuu au rais? Maana mmoja kati ya hao alishatangaza kabisa kwamba ukimshauri ndo umepoteza,sasa ili tusipoteze muda wetu be specific,TUNA MSHAURI NANI?
Mfumo wa utawala wa nchi yetu ni mfumo wa Presidential, rais wetu ni Executive President, rais mtendaji, hivyo watu wengine wote, kila wanachofanya ni kwa niaba ya president. Hivyo ushauri wowote ni kwa president.
P
 
okay nipo tayari kutoa huo ushauri,je naulekeza kwa nani?
 
Sasa Pascal mbona unatuamrisha? Eti vinginevyo nyamaza, who gave you power authority?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mfumo wa utawala wa nchi yetu ni mfumo wa Presidential, rais wetu ni Executive President, rais mtendaji, hivyo watu wengine wote, kila wanachofanya ni kwa niaba ya president. Hivyo ushauri wowote ni kwa president.
P
Sasa umesahau kwamba rais alisema ukimshauri ndio umeharibu? Au unataka tumshauri ili tuharibu zaidi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Vinginevyo nyamaza"
Pasacal, hatuwezi wote kunyamaza, kukosoa nako ni kusaidia pia.
Bila kuangalia tulipojikwaa kukaa kimya hakutasaidia kitu.

Tulikosea pale tulipodhani kwamba corona ni kaugonjwa kadogo tu, ni upepo tu utapita, ni shetani tumkabidhi Mungu amshughulikie.
Sasa tumeona siyo kaugonjwa tena, siyo kacorona bali ni Li-corona, siyo upepo tu wa kawaida bali ni dhoruba. Kwamba bado ni shetani sina ubishi nalo, ila anaweza akawa shetani aliyeruhusiwa na Mungu atushughulikie.
Kumbuka habari ya Ayubu.

Mpaka.sasa hatujawa serious, tunachukulia poa tu. Maambukizi yanaongezeka na vifo vinaongezeka, halafu tukae kimya?
Sasa hivi watu wanakimbia Dar kwenda mikoani, viongozi wetu wanaona na hakuna hatua zinazochukuliwa kuzuia hawa watu, Nani anayejua hawa wanaokimbia Dar wako salama kiasi gani? Zaidi 80% ya maambukizi ya nchi nzima yapo Dar. Ni hatari sasa hivi kuendelea kuruhusu watu kuingia na kutoka Dar.

Mbunge aliyekutwa na virusi ya Corona alitoka Dom kuja Dar na akarudi na maambukizi Dom.
Tutaangamia kwa kukosa maarifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Interested Observer, hiki unachokisema, ndilo lengo haswa la bandiko hili, tusinyoosheane vidole, kwa kulaumiana na kushutumiana bali tusaidiane.

Mimi ni muumini wa karma, malipo ya karma yanalipwa kutokana na nia ovu na jambo ovu. Ukifanya jambo ovu kwa nia njema kama hilo jambo ovu litaisaidia jamii, then kupitia karma, unabarikiwa.

Na ukifanya jambo ovu, ukabaini ulifanya jambo ovu, baada ya kubaini umefanya jambo ovu ukabadilika na kuanza kufanya jambo jema, ukifanya mema mengi makubwa kuliko lile jambo ovu, karma ya mema itakuwa ni kubwa zaidi na itaifuta ile bad karma ya lile jambo ovu moja.

Tangu kuanza kwa janga la Corona, humu jf tuu hili ni bandiko la 15! Dedicated to janga la Corona. Kati ya mabandiko haya 15, ni mabandiko 3 tuu ndio yalisifu Cacorona na kupongeza kujimwambafy dhidi ya Corona, lakini mabandiko 12 ni ya kusaidia jamii, na sikuishia jf tuu, mimi nina co-host a 60 minutes weekly Live TV Program, kwa wiki ya 4 sasa the program is dedicated to Corona to help out Watanzania.

P
Rejea za Mandiko ya The Same Author Kuhusu Janga la Corona
  1. Mtu kama huyu ni binadamu au shetani? Anaombeaje Corona ifike Tanzania. Kuiombea nchi yako majanga, sio zaidi ya uendawazimu? Huu sio ushetani? - JamiiForums
  2. Corona: Japo ni janga, pia ni fursa. Tanzania bado hakuna maambukizi, tupunguze panic, tuongeze Elimu. WB kumwaga mihela, tuchangamkie fursa - JamiiForums
  3. Corona inatufundisha Tanzania tuna tatizo kuchanganya siasa na professionalism. Hongera Prof. Janabi kwa elimu uliyotoa, so far you are the best! - JamiiForums
  4. RC Makonda, Dar ni jiji la wote, vyama vyote. Mbowe sio mwanasiasa uchwara aliyefilisika, Zitto sio mshirikina. Tunakupenda, heshimu wote uheshimiwe - JamiiForums
  5. Je, ni kweli kuna Waziri anaugua Corona inafanywa Siri? Tunaficha nini? Hala hala kisa cha mficha maradhi! Truth & Transparency the only way out! - JamiiForums
  6. Star TV: Msemaji Mkuu wa Serekali, Dr. Hassan Abbas, azungumzia wajibu wa vyombo vya habari kuripoti janga la Corona - JamiiForums
  7. Ama kweli nabii hakubaliki nyumbani!. Je Magufuli ni nabii? Tanzania wanambeza, Afrika wanamlilia! Tanzania yapigiwa mfano Magufuli awe Rais wa Afrika - JamiiForums
  8. Vita Janga la Corona: Msemaji Mkuu wa Serikali, Dr. Hassan Abbas, Naibu Waziri wa Afya, Dr. Faustine Ndungulile, kesho watakuwa live JLNH-Star TV - JamiiForums
  9. Star TV: Msemaji Mkuu wa Serikali, Dr. Hassan Abbas na Naibu Wazuri wa Afya Dr. Faustine Ndungulile, Wanazungumzia Corona - JamiiForums
  10. Mungu ni Omnipresent. Kufuatia Local Transmission ya Corona. Je, Sasa Tushinikize Watu Wasalie Majumbani Mwao, ila Sadaka Ndio Itumwe Kwa M-Pesa? - JamiiForums
  11. Nabii Malisa: Mungu ameniambia Corona ni April tu, May hakuna Corona na hakuna atakayekufa!. - JamiiForums
  12. Kwa Kasi Sasa, Jee Tuendelee Ushujaa wa Ka-Corona, Tusitishane, Tuchape Kazi Tukiteketea, Au Sasa Tubadili Msimamo Tusitisishe Mikusanyiko Tuokoke? - JamiiForums
  13. TBC - Mjadala wa Role of The Media kwenye mapambano ya Corona, Je, Media Inatimiza Wajibu Wake Ipasavyo? - JamiiForums
  14. Live on Star TV: Corona Kushika Kasi Ndio Habari Kubwa Tanzania, Jee Media ya Tanzania, Inatimiza Wajibu Wake Ipasavyo? - JamiiForums
  15. Corona: Tusinyoosheane vidole. Kama unaweza kusaidia, please do. Usisubiri uombwe - jitokeze saidia, vinginevyo nyamaza! - JamiiForums
 
Katiba inavunjwa waziwazi, uonevu kwa wapinzani, kauli ya mkulu kutofautina na vitendo vyake nk.
Inahusiana nini na UZI uliopo?

Kwaiyo katiba sijui uonevu ndio vitasababisha Corona isiwepo?

Jaribu kufikiria nje ya box kumbuka haina dini, kabila, tajiri, masikini wala itikadi ya chama. Chukua hatua Corona inaua.
 
Katiba inavunjwa waziwazi, uonevu kwa wapinzani, kauli ya mkulu kutofautina na vitendo vyake nk.
Inahusiana nini na UZI uliopo?

Kwaiyo katiba sijui uonevu ndio vitasababisha Corona isiwepo?

Jaribu kufikiria nje ya box kumbuka haina dini, kabila, tajiri, masikini wala itikadi ya chama. Chukua hatua Corona inaua.
 
Mfumo wa utawala wa nchi yetu ni mfumo wa Presidential, rais wetu ni Executive President, rais mtendaji, hivyo watu wengine wote, kila wanachofanya ni kwa niaba ya president. Hivyo ushauri wowote ni kwa president.
P
Kitu pekee usichojua ni kwamba huyo executive ndo mwenye kura ya veto na ndo ukimshauri umepoteza unless Kama mdomoni uwe unazungumzia kwenda moro from Dar while in reality wewe unachotaka ni kwenda different direction.Kwa style hiyo utampata
 
Sasa umesahau kwamba rais alisema ukimshauri ndio umeharibu? Au unataka tumshauri ili tuharibu zaidi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Rais Magufuli hajakataa kushauriwa, alichokataa ni kushinikizwa!, kulazimishwa!.
Katiba yetu ya JMT anampa uhuru rais wetu kushauriwa na yoyote na hadi tumemuwekea wasaidizi wataalamu wa washauri na wanampa ushauri wa kitaalamu ila katika kufikia maamuzi, ni katiba hiyo hiyo imempa mamlaka ya kufikia maamuzi yeye kama yeye bila kufuata ushauri wa yeyote usipokuwa katika yale maeneo ambayo katiba inamlazimisha rais kufuata ushauri.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…