Corona; Ufaransa yahodhi shehena ya mask zilizokuwa zipelekwe Italy na Spain

Sikirimimimasikini

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2019
Posts
2,926
Reaction score
15,634
Corona yaendelea kuwatoa utu mabeberu.

Kampuni ya utengenezaji wa vifaa tiba ya Uswizi, imelalamika kuwa Ufaransa imewachezea rafu mbaya mno Italy na Spain baada ya kuhodhi mzigo wa mamilioni ya mask za uso na glovu zilizokuwa zinasafirishwa kwenda kwenda Itali na Spain kupunguza maambukizi ya corona.

Kampuni hiyo imesema hiko kitendo ni cha kuudhi mno na kilichokosa uungwana.

Imesema itasafirisha mzigo mwingine kwenda Italy na Spain ila kupitia Ubelgiji.

Pia imeripotiwa kuwa Ujerumani nayo ilifanya uharamia kama huo wiki iliyopita baada ya kuhodhi shehena ya mask toka China iliyokuwa yasafirishwa kwenda Italy kupitia Ujerumani.


 
Do do mabeberu wanaibiana wao kwa wao
Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]huu mchezo hauhitaji hasira
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa ubabe tu.
Maana dawa hakuna,juzi Trump kafanya haya haya.
Sisi wa Africa tutaendelea kujificha usiku.
 
Apo ndo ujue Mungu ameinusuru Africa maana wazungu wanagombania vitendanishi wenyewe kwa wenyewe,sisi ingekuwaje? Na juzi Marekani imezuia shehena ya vitendanishi vilivyokuwa vinakwenda nchi za Ulaya


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mwenyezimungu hamfichi mnafiki mwaka wao huu kwa wale wenye akili tu ndio wataelewa wazungu ni watu gani Ila kwa wale walishakuwa watumwa wa wazungu toka tumboni wataona kawaida tu maana Kuna watu humu bora umseme vibaya muumba kuliko kumsema mzungu [emoji3][emoji3][emoji40][emoji40][emoji40]
Sent using Jamii Forums mobile app
 
You can imagine wanagombea vifaa tiba na vitendanishi bado chanjo&tiba bado


Sent from my iPhone using JamiiForums
Aisee, Mkuu umewaza mbali sana.

Chanjo/tiba ikipatikana itakuwa ni mchafukoge zaidi!

Masikini sisi waafrika, sijui tutawezaje kupigana nao vikumbo ktk kugombea!
 
Waache wamaindiane wenyewe kwa wenyewe,Washaua sana wasio na hatia,Malipo ni hapa hapa Duniani.
 
Kuna uwezekano baada ya Corona kuisha EU na NATO zitakuwa na hali mbaya itakayopelekea utengano
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…