Corona virus: Tunajifunza nini toka kwa wengine?

Corona virus: Tunajifunza nini toka kwa wengine?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Moja kwa moja kwenye mada:

Majirani zetu Kenya, Rwanda na DRC tayari wamesha ripoti kuwapo kwa wagonjwa wa corona katika nchi zao.Kwa hali hii ni wazi kuwa hapa kwetu ni suala la muda tu sasa.

Wenzetu, katika nchi nyingi kutegemeana na ukubwa wa tatizo wame kuwa wakichukua hatua kadhaa katika kusaidia udhibiti wa ugonjwa huu. Baadhi ya hatua zilizoishachukuliwa ni:

1. Kuwekwa quarantine kwa wageni wote tokea nchi zenye kufahamika kuwa na wagonjwa kwa takribani siku 14 kabla ya kuruhusiwa kuingia katika nchi nyingine wanakotaka kwenda.

2. Ndege za moja kwa moja tokea nchi zenye wagonjwa zimesitishwa kuelekea nchi zingine.

3. Mikusanyiko ya watu: kwenye mashindano ya mpira, matamasha, makanisani, misikitini nk imesimamishwa.

4. Taratibu za mambo ya kodi kwa wananchi zimecheleweshwa kuwapa wananchi ahueni kwenye kujikimu kuhusiana na mdororo wa uchumi kwani takribani shughuli zote za uzalishaji mali zimesita.

5. Sehemu za wazi kwa ajili kunawa kujiweka salama zimewekwa katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu.

6. Namba za simu za kupiga mtu anapojishuku kuwa na dalili za ugonjwa zimewekwa wazi.

7. Nk

Hapa kwetu ninaamini pamoja na #4 serikali ingepanga kusimamisha kwanza shughuli zote za miradi mikubwa hasa ya SGR na stigglers gorge.

Hatua hii itatupa nafasi kutambua udharura uliopo kuhusiana na ugonjwa huu.

Tuachane na makesi kesi, chuki na magomvi yasiyokuwa na vichwa wala miguu. Tutambue sote kwa umoja wetu sasa tumekabiliwa na adui mmoja hatari mno anayetishia uwepo wetu kama taifa.

Ni heri tukawa hai bila ya SGR au stigglers gorge kuliko kuwa navyo hali tumeangamia sote kwa Corona.

Nawasilisha.
 
Sisi hapa kwetu tumeshaanzisha utaratibu wetu,
MTU akibainika na dalili tu ,tunaenda kumpima, vipimo vikionyesha hana virus basi tunamuacha tu anendelee na maisha yake tu,

Mambo ya kuchunguza siku 14 tumeshawaachia wazungu huko.



Serekali haipo serious na haya mambo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sisi hapa kwetu tumeshaanzisha utaratibu wetu,
MTU akibainika na dalili tu ,tunaenda kumpima, vipimo vikionyesha hana virus basi tunamuacha tu anendelee na maisha yake tu,

Mambo ya kuchunguza siku 14 tumeshawaachia wazungu huko.



Serekali haipo serious na haya mambo

Sent using Jamii Forums mobile app

Ilikuwa heri kuwekwa vilivyo kwenye kujipanga. Kutafuta watu wote waliokutana na mgonjwa kuwa weka kwenye quarantine itakuwa shughuli pevu kweli kweli.
 
Ilikuwa heri kuwekwa vilivyo kwenye kujipanga. Kutafuta watu wote waliokutana na mgonjwa kuwa weka kwenye quarantine itakuwa shughuli pevu kweli kweli.
Hicho kitu viongozi wetu hawatambui mkuu, sasa unadhani tutafanyaje mkuu

Cha msingi ni kuchukua tahadhari binafsi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hicho kitu viongozi wetu hawatambui mkuu, sasa unadhani tutafanyaje mkuu

Cha msingi ni kuchukua tahadhari binafsi

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu la muhimu nionavyo ni kuwapigia kelele hawa serikali kuwajibika.

Corona haina chama.

Wanapaswa serikali watambue kuwa kwa gharama yoyote sisi wananchi hatutaki Corona. Kwa sababu kwenye madaladala mgonjwa mmoja ataambukiza nchi nzima.

Siyo siri tunayo dharura moja tu sasa anayetwambia nyingine hatutakii mema huyo.
 
Rwanda, DRC na Kenya tayari case zinaongezeka. Hawa wanaoongezeka wana wagonjwa wangapi nyuma yao:

Rwanda confirms four more coronavirus cases

Kama ilivyo katika uzi juhudi ilikuwa sasa:

1. Simamisheni mikusanyiko.
2. Tambua ni athari katika mapato ya watu.
3. Ahirisheni deadlines za kodi za mapato.
4. Simamisheni miradi yote mikubwa kwa sasa.

Maisha (uhai) kwanza.
 
Nafuu ipo serikali ya wanyonge imeangazia kutambua majukumu yake kwa raia. Kenya wanasonga mbele:

Safaricom waives M-Pesa fees

Serikali yetu inayo hata dalili ya kujali kweli?
 
Uzi huu uliandikwa March 15 kabla ya corona kuingia nchini.

Hatukufanya lolote. Hatukujifunza toka kwa wenzetu wengine. Hata sasa hatujufunzi hata tumeanza na uorodheshaji wa madereva na makondacta wa madaladala.

Tusidanganyane nyuzi moja baada ya nyingine zitarejeshwa hapa wakati wa kuwajibishana.

Ama kwa hakika hatutaangalia makunyanzi.
 
Kuna uwezekano corona ilikuwepo kabla ya march 15 Kwa sababu kama China ilikuwepo tangu mwaka jana na watu walikuwa wanafanya safari za kwenda na kurudi China
 
Kuna uwezekano corona ilikuwepo kabla ya march 15 Kwa sababu kama China ilikuwepo tangu mwaka jana na watu walikuwa wanafanya safari za kwenda na kurudi China

Yote yanawezekena na hayo sasa ni historia.

Cha msingi sasa ni kuudhibiti maana inafahamika kuwa si ya mchezo mchezo.
 
Sisi hapa kwetu tumeshaanzisha utaratibu wetu,
MTU akibainika na dalili tu ,tunaenda kumpima, vipimo vikionyesha hana virus basi tunamuacha tu anendelee na maisha yake tu,

Mambo ya kuchunguza siku 14 tumeshawaachia wazungu huko.



Serekali haipo serious na haya mambo

Sent using Jamii Forums mobile app
Unakumbuka ilivyokuwa umeandika hapa?

Kuna mwenzio mwingine aliandika kuwa pana dini hamuugui Corona.

Bado hujapanga kufuta bandiko lako tu?
 
Back
Top Bottom