Coronavirus: Wauguzi wa wagonjwa wa corona Kenya waanza mgomo baridi

Coronavirus: Wauguzi wa wagonjwa wa corona Kenya waanza mgomo baridi

Bishop Hiluka

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2011
Posts
7,147
Reaction score
14,699
wauguzi.jpg

Wauguzi wanaofanya kazi katika wodi iliyotengwa kwa watu walioambukizwa virusi vya corona nchini Kenya wameanza mgomo baridi kulalamikia kile wanachodai kuwa ukosefu wa vifaa vya kujikinga na mafunzo ya kutosha.

Hospitali ya Mbagathi katika mji mkuu wa Nairobi, ni moja ya hospitali zilizo na wodi ya kutibu wagonjwa waliombukizwa virusi hivyo hatari.

Katibu mkuu wa muungano wa wauguzi nchini Kenya, Seth Panyako ameiambia BBC kwamba wauguzi watarejea kazini ikiwa watapewa mavazi maalum na mafunzo ya jinsi ya kuwashughulikia wagonjwa.

"Wahudumu wa afya wako katika hatari ya kupata maambukizi katika mazingira yao ya kazi," alisema Bw. Panyako.

"Bila ya kuwa na vifaa maalum,wanatarajiwa kujilinda vipiwakiwa kazini na wanaporejea nyumbani kutangamana na familia zao?"

Hospitali ya ya Mbagathi inawazuilia watu 22 ambao walitangamana na mgonjwa wa kwanza aliyeambukizwa virusi vya corona.

Watu wengine wawili walioambukizwa virusi hivyo wamepelekwa katika hospitali ya ya kitaifa wa Kenyatta - ambako mgonjwa wa kwanza aliyethibitishwa kuambukizwa anapewa matibabu.

Chanzo: BBC Swahili
 
Ninatumaini wizara ya afya imesikia hili ili matukio ya hivyo yasijitokeze hapa kwetu.
 
Tanzania pia kimewaka, corona imeshaingia. Mtu mmoja amethibitishwa...
 
e706321e-f11f-49df-8e4b-23dc13ebd19d.jpg

Kenyan nurses at a coronavirus isolation ward have started a go-slow to protest against what they say is a lack of protective gear and poor training. Mbagathi Hospital in the capital, Nairobi, is one of the facilities with isolation wards for treatment of patients infected with the virus.

The Kenya National Union of Nurses Secretary General Seth Panyako has told the BBC that the nurses will only report back to work once they've had training on how to handle patients and received protective gear. "Nurses are the most exposed workers in hospitals," Mr Panyako said. "With no protective equipment gear, how are they supposed to protect themselves at the workplace and their families too when they go back home?"

The hospital is holding 22 people who came into contact with the first confirmed case. Two of the contacts, who tested positive, have since been moved to Kenyatta National Hospital - the country's top referral hospital - where the first confirmed patient is being treated.

SOURCE: BBC
 
Back
Top Bottom