Mchana huwa rahisi kwa polisi kufuatilia nani hajavaa barakoa, anakuona hata kwa mbali huko na kukujia, ila usiku unajimwayamwaya bila libarakoa kwa raha zako haujali kitu.
Niwe mkweli, sio asili yetu Waafrika kwenye kuchukua tahadhari, mimi binafsi nachukia sana barakoa, inanifanya nijihisi kama zuzu hivi, ila ndio sayansi hiyo na siibishii, isingekua kwa mapolisi sidhani kama ningevaa barakoa, ila tu basi inabidi maana kwa uzembe wetu Waafrika lazima tulazimishwe hata kwenye kuchukua tahadhari.
Barakoa inasaidia kwa asilimia fulani, kwanza kwa namna Watanzania husongamana, mna bahati sana corona haijawa na hasira dhidi ya Waafrika, mngepukutika kama kondoo na mbuzi.... huwa mnasongamana kwenye midaladala na kupumuliana humo balaa.