CP Awadhi afunga mafunzo ya Wakuu wa Polisi Wilaya - Moshi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Kamishna wa Operesheni Mafunzo wa Jeahi la Polisi CP Awadhi Juma Haji Leo Novemba 8,2024 amefunga mafunzo ya siku tano kwa Wakuu wa Polisi Wilaya zote Tanzania Bara na Visiwani. Mafunzo hayo yamefanyika katika Shule ya Polisi Tanzania Moshi Mkoani Kilimanjaro.

Wakati akifunga Mafunzo hayo CP Awadhi amewataka Wakuu hao wa Polisi Wilaya waende kutumia elimu waliyoipata kuweka mipango kazi shirikishi ya kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27,2024 ili uweze kufanyika katika mazingira ya amani,utulivu na usalama kulingana na imani na matarajio ya Watanzania.


 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…