CP Hamduni Salum imulike Tanga inanuka rushwa,TAKUKURU wamekuwa mawakala wa wahalifu

CP Hamduni Salum imulike Tanga inanuka rushwa,TAKUKURU wamekuwa mawakala wa wahalifu

Afrikasana

JF-Expert Member
Joined
Oct 27, 2021
Posts
320
Reaction score
288
Kamanda wa kupambana na rushwa Hamduni Salum wasaidie sana watu wa Tanga.

Ofisi za TAKUKURU jiji la Tanga wamekua watu wasiotenda haki kwa kutofuata miiko ya kazi.

Wanakua watoa siri hata ukiwaeleza juu ya viongozi wala rushwa wao wanakua washanunuliwa na hao viongozi. Ukitokatu ofisi za TAKUKURU utashangaa kuambiwa na mtuhumiwa habari zote ulizopeleka huko nimeshazipewa.

Ingawa aliondolewa kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga tangia mwaka jana lakini bado hakuna jipya ameacha masalia yaliyokomaa hapo

TAKUKURU Tanga imekua wapowapotu,maeneo ya watu yanauzwa mara mbilimbili na watu wa ardhi lakini wakipewa taarifa hakuna linalofanyika.

Ukweli nikwamba matapeli wa ardhi bado wapo wanatishia watu mtaani kuuza maeneo yao,tena wanatembea na polisi eti ni watu wa mipango miji na TAKUKURU wamelala fofofo kama wamedungwa sindano kali za usingizi hawachunguzi wanasubiri wapelekewe taarifa na wakipelekewa wanaona imejitokeza fursa kwao na sio kazi

Kwabahati mbaya sana Tanga haijapata viongozi wanaotatua migogoro ya ardhi,kusimamia utekelezaji wa maagizo ya Mh. Rais. Bado wanyonge wanaporwa haki zao na wahusika wanapeperushatu bendera kwenye magari.

Ili kujua kama Tanga rushwa imekomaa hata waandishi wa habari Tanga mjini hawapo na mkiwaita kutoka wilayani huko nakuwapa habari wakitoka hapo wanalala nazo mbeleee.

Kama wakija kwenye mikutano ya hadhara hata baada ya wananchi kuwaita kutoka maeneo mengine wanakuja na hao viongozi kwenye magari yao. Halafu angalia sasa kitakachoripotiwa

Eti Tanga ni jiji lakini hakuna mwandishi wa ITV, Star TV,TBC,Channel Ten nk katikati ya jiji badala yake eti Channel Ten wanaripoti zaidi Handeni na Lushoto kisa walishaona labda mazingira sio rafiki kwao ila harufu ya rushwa ipo.

Waletwe watumishi waadilifu kwani watanzania wanaoweza hiyo kazi niwengi.

Ni bora ofisi za TAKUKURU Tanga zikafungwa maana hazina tija kwa wananchi wa Tanga. Zipo kesi zenye zaidi ya mwaka lakini TAKUKURU hawayang'azi

CP Hamduni anza na Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga akiondoka na watumishi wala rushwa walioachwa na yule aliyesimamishwa mwaka jana ndio labda ofisi itatenda haki.
 
Hapo kwa waandishi wa habari nakukatalia..kuna William Mngazija wa ITV na Bertha Mwambela..wa TBC hao ni kwa uchache tu..shida nini mkuu..?
 
Hapo kwa waandishi wa habari nakukatalia..kuna William Mngazija wa ITV na Bertha Mwambela..wa TBC hao ni kwa uchache tu..shida nini mkuu..?
Ofisi zao zipo wapi kwa hapo Tanga jiji mkuu,naomba nielekeze.

Mngazija yule sio Mngazija huyu. Hatuoni habari zake kwasasa
 
Mkuu kiongoz wa takukuru tanga anaitwa Nani?? Tuanzie hapo Kwanza na kitu gani ameshindwa kukishughulikia maana umekuwa too general, ungeenda specific, wapi ka kwama??

Ni nini alitakiwa afanye, na walao ungekuja na ushuhuda wako binafsi, au wa mtu wa karb kujustfy kuwa Takukuru wamefel,

Ikiwa utashindwa maana yake kunasehema hujajipanga, au unamasilahi yako binafsi...
 
Kujua au kutojua jina la mkuu wa taasisi hakuondoi uhalali wa raia kulalamika

Nimetaja mfano mmoja wa tatizo la ardhi na watu wa mipango miji kuuza viwanja vya watu,unataka niwe specific kivipi yani

Mkurugenzi aliyetenguliwa alisharipotiwa kwa kudhulumu na kukandamiza watu,hajawahi hata kuchukuliwa hatua

Unataka ushuhuda gani
 
Hapo kwa waandishi wa habari nakukatalia..kuna William Mngazija wa ITV na Bertha Mwambela..wa TBC hao ni kwa uchache tu..shida nini mkuu..?
Mkuu huyo jamaa nimemuelewa, anaposema waandishi wanakuja na viongozi kwenye magari yao ona maana hii hapa ambayo ni ukweli mtupu....

Mwandishi anapokuja na mtoa habari ya upande wa kwanza ambaye ndiye aliyempa (tip) na atampa bahasha ya kaki, kwenye kubalance story kutoka kwa mtu wa pili lazima iwe ya kulinda mtoa tip si kumuumiza 😃!.

Ndiyo maana anasema,
"... hata baada ya wananchi kuwaita kutoka maeneo mengine wanakuja na hao viongozi kwenye magari yao" maana yake ndiyo hiyo mkuu!.
 
Hapo kwa waandishi wa habari nakukatalia..kuna William Mngazija wa ITV na Bertha Mwambela..wa TBC hao ni kwa uchache tu..shida nini mkuu..?
Duh ati Betha Mwambela sasa anapatikana wapi huyo.

Bora hata akina Millard Ayo wafungue ofisi Tanga kuliko hayo ma TBC na ITV. Hawana jipya
 
Mkuu huyo jamaa nimemuelewa, anaposema waandishi wanakuja na viongozi kwenye magari yao ona maana hii hapa ambayo ni ukweli mtupu....

Mwandishi anapokuja na mtoa habari ya upande wa kwanza na ambaye ndiye aliyempa (tip) na atampa bahasha ya kaki, kwenye kubalance story kutoka kwa mtu wa piliazima iwe ya kulinda mtoa tip si kumuumiza 😃!.

Ndiyo maana anasema,
"... hata baada ya wananchi kuwaita kutoka maeneo mengine wanakuja na hao viongozi kwenye magari yao" maana yake ndiyo hiyo mkuu!.
Asante kwa kunielewa mkuu.
Kwanza baadhi ya waandishi wakiitwa wanadai hawana mafuta kisha wanakuja na hao viongozi maana yake nikwamba wameshanunuliwa jumla
 
Mkuu huyo jamaa nimemuelewa, anaposema waandishi wanakuja na viongozi kwenye magari yao ona maana hii hapa ambayo ni ukweli mtupu....

Mwandishi anapokuja na mtoa habari ya upande wa kwanza ambaye ndiye aliyempa (tip) na atampa bahasha ya kaki, kwenye kubalance story kutoka kwa mtu wa pili lazima iwe ya kulinda mtoa tip si kumuumiza [emoji2]!.

Ndiyo maana anasema,
"... hata baada ya wananchi kuwaita kutoka maeneo mengine wanakuja na hao viongozi kwenye magari yao" maana yake ndiyo hiyo mkuu!.
Mkuu unahoja ya msingi ila mafikr hujaipika vzr, au huwezi kujieleza vzr, ila ukiweka vzr kidg tu hii habar yako Ni vyeti mno, pokea ushauri mkuu
 
Niiwekeje mkuu. Naomba ushauri
Kanuni ya jamii forum Ni speak openly, na ambacho ungeIngatia(kwa maoni yangu) ungetoa ushuhuda wa moja kwa moja not general, kwamba ulikuwa mhanga au mtu wako wa karibu, ukamtaja aliehusika na hlo Jambo hyo wa takukuru, then ukawasaidia watakofuatilia sos ya taarifa yako, ili wanapoanza wajue wanaanzia wapi,

Habar Kama hzi za idara nyeti huja na unyeti wake, mfano nikitoa taarifa kwa nlipo(geita) naeleza imenitokea/ au mtu wa karbu, natoa taarifa hata nliempatia taarifa(mkurugenzi wa takukuru) naenda mbali mpka police, baada ya ushahidi na utable hum Sasa, wajib wangu unakuwa umeisha... So utawasaidia wanaofuatilia kujua pakuazia kuliko kuwapa kazi tena...

Anyway Ni maoni. Yangu..
 
Kanuni ya jamii forum Ni speak openly, na ambacho ungeIngatia(kwa maoni yangu) ungetoa ushuhuda wa moja kwa moja not general, kwamba ulikuwa mhanga au mtu wako wa karibu, ukamtaja aliehusika na hlo Jambo hyo wa takukuru, then ukawasaidia watakofuatilia sos ya taarifa yako, ili wanapoanza wajue wanaanzia wapi,

Habar Kama hzi za idara nyeti huja na unyeti wake, mfano nikitoa taarifa kwa nlipo(geita) naeleza imenitokea/ au mtu wa karbu, natoa taarifa hata nliempatia taarifa(mkurugenzi wa takukuru) naenda mbali mpka police, baada ya ushahidi na utable hum Sasa, wajib wangu unakuwa umeisha... So utawasaidia wanaofuatilia kujua pakuazia kuliko kuwapa kazi tena...

Anyway Ni maoni. Yangu..
Asante mkuu kwa ushauri. Eneo lengwa ni rushwa kwa watu wa ardhi.

Mkurugenzi aliyemaliza muda wake na mkuu wa mkoa ambaye kwasasa yupo Morogoro ndio waasisi wa huu mgogoro.

Aliyekua mkuu wa wilaya bwana Mwilapo nae aliunda kamati yake lakini akazidiwa nguvu na mabingwa wa mbinumbinu.

TAKUKURU wanajua kama ardhi imeuzwa na watu wa mipango miji isivyohalali.

Tatizo Tanga hawana mtu wa kuwasemea usije ukaona watu ukasifia kama kuna wachapakazi Tanga.

Masuala ya ardhi na rushwa Tanga bado sana
 
Mkuu unahoja ya msingi ila mafikr hujaipika vzr, au huwezi kujieleza vzr, ila ukiweka vzr kidg tu hii habar yako Ni vyeti mno, pokea ushauri mkuu
Nimetoa ufafanuzi kidogo mkuu kulingana na mtu ambaye hajaelewa kontenti ya mtoa mada, so nianze kuandika mada ndani ya mada haiwezekani hasilani!.

Note from the early comment has replied!.
 
Kweli suala la ardh tanga rushwa imetawala sana! Ofisi za tbc zipo bandar pale unaweza kwenda ila kama ulivyosema mwandish pekee hawezi kukutatulia tatizo lako maana hao viongozi ndiyo wanaowaweka mjini sasa usitegemee atakitia kitumbua chake mchanga!

Siku moja mie nilipata kesi pale tanga kuna watu walitaka kunilipua wakaita waandishi..kabla mwandishi hajaenda kwao akanipigia akaniekeza nikamwambia usiende nikamtumia elf hamsini na ile kesi nikaizima kimyakimya wakabak tu na maumivu yao moyoni..

Ili ufanikiwa changamka..panda gar nenda dodoma kwa waziri au nenda mosh kwa kamishna wa ardh vinginevyo utalalamika hadi yesu arudi
 
Kweli suala la ardh tanga rushwa imetawala sana! Ofisi za tbc zipo bandar pale unaweza kwenda ila kama ulivyosema mwandish pekee hawezi kukutatulia tatizo lako maana hao viongozi ndiyo wanaowaweka mjini sasa usitegemee atakitia kitumbua chake mchanga!

Siku moja mie nilipata kesi pale tanga kuna watu walitaka kunilipua wakaita waandishi..kabla mwandishi hajaenda kwao akanipigia akaniekeza nikamwambia usiende nikamtumia elf hamsini na ile kesi nikaizima kimyakimya wakabak tu na maumivu yao moyoni..

Ili ufanikiwa changamka..panda gar nenda dodoma kwa waziri au nenda mosh kwa kamishna wa ardh vinginevyo utalalamika hadi yesu arudi
Huyo waziri mwenyewe alishapotoshwa na Martin Shigela na mkurugenzi aliye tupiwa virago vyake bwana Daudi Mayeji.
Watu hao wawili ni maadui wa vyombo vya habari na ndio wamekoleza mgogoro wa ardhi.
 
Huyo waziri mwenyewe alishapotoshwa na Martin Shigela na mkurugenzi aliye tupiwa virago vyake bwana Daudi Mayeji.
Watu hao wawili ni maadui wa vyombo vya habari na ndio wamekoleza mgogoro wa ardhi.
Sasa ndugu yangu..huko ni kukata tamaa! Fuata taratibu na kanuni au nenda kwa waziri au nenda mahakaman lakini ukibak kusema kila mtu anakasoro utaambulia maumivu
 
Sasa ndugu yangu..huko ni kukata tamaa! Fuata taratibu na kanuni au nenda kwa waziri au nenda mahakaman lakini ukibak kusema kila mtu anakasoro utaambulia maumivu
Labda mahakamani maana waziri alipofika walijifungia nae ndani wakampotosha.
Mbunge nae hajasomeka msimamo wake
 
Back
Top Bottom