CRDB Bank jirekebisheni, mikopo ni jambo la dharura

CRDB Bank jirekebisheni, mikopo ni jambo la dharura

Mimi nilikaaga wiki 3 pia ndo nikapata mkopo Yan ukiaza kufuatilia mkopo Crdb Bora ya anayefuatila Kutambulisho Cha Nida au control namba Tanesco lazima utakubali mziki
 
Habari wakuu,

Mimi kama mdau wa bank hii ya CRDB naomba nitoe dukuduku langu na kama yupo mfanyakazi au mtendaji wao tafadhari rekebisheni matatizo yenu, haiwezekani process ya mkopo ikachukua wiki tatu mpaka mwezi na Bado fedha/mkopo hamtoi, hivi hamjui mkopo ni kitu cha dharura?

Naombeni kama mmeshindwa kutoa huduma hii kwa haraka basi muwe wa wazi tu tusipotezeane muda.

Naomba kuwasilisha.

Mhanga hapa, its May 2022, and 45 Days zimepita tangu nianze mchakato wa kufatilia mkopo wa biashara, niko Morogoro, yaani 45 Days tangu siku ambayo wamekuja kunitembelea Ofisi na Dhamana na kwa upande wangu nimefanya process kwa uharaka sana, i.e kupeleka viambatanishi vyote pamoja na kulipia gharama zote za awali (Bima, Ardhi, Official Search etc, keep in mind step hii ni zaidi ya wiki mbili sasa nimeshamaliza) Kupewa form tu za mkataba ilikua mtihani mzito. Pasua kichwa hawa jamaa
 
Mimi nilikaaga wiki 3 pia ndo nikapata mkopo Yan ukiaza kufuatilia mkopo Crdb Bora ya anayefuatila Kutambulisho Cha Nida au control namba Tanesco lazima utakubali mziki

Wiki tatu kutoka Hatua ipi?? Ya kulipia kila kitu gharama za awali na kurudisha form?? Au mchakato mwanzo mpaka mwisho?
 
Habari wakuu,

Mimi kama mdau wa bank hii ya CRDB naomba nitoe dukuduku langu na kama yupo mfanyakazi au mtendaji wao tafadhari rekebisheni matatizo yenu, haiwezekani process ya mkopo ikachukua wiki tatu mpaka mwezi na Bado fedha/mkopo hamtoi, hivi hamjui mkopo ni kitu cha dharura?

Naombeni kama mmeshindwa kutoa huduma hii kwa haraka basi muwe wa wazi tu tusipotezeane muda.

Naomba kuwasilisha.
Wale maana yake wanakuambia usikope
 
Kazi ya kukopesha ni kazi ngumu na inahitaji umakini sana. Huwezi kumkopesha kila mtu mwenye shida. Kinachangaliwa kwenye kukopa ni uwezo wa mkopaji kurudisha. Wabongo ulikiwalegezea baada ya mwaka utakuwa umefunga benki hata kama ilikuwa kubwa kiasi gani. Tuseme kwa ujumla kinachofanya kukopa Tanzania kuwe kugumu ni uhakika wa wakopaji kurudisha walichokopa.
Yaani kuna watu wanaenda kukopa sehemu wanajua kabisa kuwa hawatolipa
 
Yaani ilivyo tu ndugu Watanzania wengi si walipaji wa madeni yawayo yoyote. Ndio maana vikundi vingi vya kukopeshana vinakufa. Ukitaka kujua watanzania 90% sio walipaji wazuri wa madeni,uwe na duka labda la vifaa vya magari hivi, hata yule usiemdhania kwamba anaweza akawa msumbufu atakusumbua mbayaa. Hata kama ana kazi au biashara nzuri tu inayomuingizia hela,lakini wakishakopa akimaliza ile shida yake siku hiyo hataki kabisa kulipa,mtakusukumana sana. Watanzania wengi akimaliza shida yake tu,kulipa anaona tabu kabisa. Na ukitaka kulijua zaidi fuatilia wale wanaokopesha mitaani kwa riba wale unapoenda kukopa aither uache gari au wanashika nyumba,viwanja n.k kulingana na thamani ya pesa unayokopa na inakuwa kwa makubariano ya muda fulani. Wakopaji wengi wanafirisiwa na wakopeshaji. Na sababu kubwa ya kufirisiwa ni ksbb moja Watanzania sio walipaj. Mbili ujanja janja mwingi. Tatu Watanzania wengi wanapoenda kukopa anakuwa hana udhoefu au adea nzuri au hajui kabisa kitu anachoenda kuzalishia hiyo hela anayoenda kukopa. Let say amesikia tu kilimo cha matikiti kwa mtu mmoja,amempa tu hesabu ya kwenye makaratasi kwamba yanalipa,kesho huyo mbio kwenda kukopa. Ndio maana bank unapoenda kukopa lazima wakufuatilie wajiridhishe je kweli unaweza kurejesha hiyo hela. Bank wenyewe huwa wanajisikia vibaya kufikia hatua ya kuuza zamana ya mteja mfano nyumba,ndio maana mpaka kufikia hatua ya kuuza nyumba yako lazima waende na wewe taratibu,wakiona unaendelea kulipa hata kwa kidogo kidogo tofauti na makubariano bado wanaendelea kukuvumilia. Mwisho nikuambie tu Watanzania asilimia kubwa sio walipaji
Umeongea vizuri sana lakini uhalisia hauko hivyo hata ndugu yangu
Benki hawakopeshi wazo kwa beginners
Benki ya biashara sio ya kilimo cha kusikia matikiti yanalipa

Walengwa wa mabenki ni wafanya biashara
Watumishi wa secta za umma na binafsi wenye sifa za kukopesheka

Mfanyabiashara ili akopesheke benki wao hawahitaji aseme kwamba mimi naweza kuwalipa mkinikopesha biashara yenyewe itajiongelea mfano Analipaje kodi za serikali au miamala yake kwenye account zake.

Mtumishi yeye ndio mlipaji mzuri hapo kwa sababu watakata kiasi walichokubaliana kwenye msharaha wake pasipo kuchelewa wala kutaafutana


Makundi yote ya niliyoyataja hapa ndio mojawapo ya watu waaminifu kwenye ulipaji wa madeni kumbuka wewe huwezi tu kwenda bank na kuomba mkopo ukiwa huna kipato chochote cha uhakika kwa waonavyo wao

Hapo sijasemea wenye dhamana pekee bila biashara


Benki wanakuwa hawana haja ya kuchelewesha mikopo wa wateja waliowaamini kuwaruhusu waanze process za kuwapatia mikopo.
 
Hawa watu wanazingua sana kumbe! Kuna mwanangu kajaza mafomi kibao na kusainisha kila sehema. Hajapata pesa na gar inazidi kukaa bandarini
 
Wapumbavu hao crdb
Nmb within 24 hrs unapewa chako.
 
Yaani ilivyo tu ndugu Watanzania wengi si walipaji wa madeni yawayo yoyote. Ndio maana vikundi vingi vya kukopeshana vinakufa. Ukitaka kujua watanzania 90% sio walipaji wazuri wa madeni,uwe na duka labda la vifaa vya magari hivi, hata yule usiemdhania kwamba anaweza akawa msumbufu atakusumbua mbayaa. Hata kama ana kazi au biashara nzuri tu inayomuingizia hela,lakini wakishakopa akimaliza ile shida yake siku hiyo hataki kabisa kulipa,mtakusukumana sana. Watanzania wengi akimaliza shida yake tu,kulipa anaona tabu kabisa. Na ukitaka kulijua zaidi fuatilia wale wanaokopesha mitaani kwa riba wale unapoenda kukopa aither uache gari au wanashika nyumba,viwanja n.k kulingana na thamani ya pesa unayokopa na inakuwa kwa makubariano ya muda fulani. Wakopaji wengi wanafirisiwa na wakopeshaji. Na sababu kubwa ya kufirisiwa ni ksbb moja Watanzania sio walipaj. Mbili ujanja janja mwingi. Tatu Watanzania wengi wanapoenda kukopa anakuwa hana udhoefu au adea nzuri au hajui kabisa kitu anachoenda kuzalishia hiyo hela anayoenda kukopa. Let say amesikia tu kilimo cha matikiti kwa mtu mmoja,amempa tu hesabu ya kwenye makaratasi kwamba yanalipa,kesho huyo mbio kwenda kukopa. Ndio maana bank unapoenda kukopa lazima wakufuatilie wajiridhishe je kweli unaweza kurejesha hiyo hela. Bank wenyewe huwa wanajisikia vibaya kufikia hatua ya kuuza zamana ya mteja mfano nyumba,ndio maana mpaka kufikia hatua ya kuuza nyumba yako lazima waende na wewe taratibu,wakiona unaendelea kulipa hata kwa kidogo kidogo tofauti na makubariano bado wanaendelea kukuvumilia. Mwisho nikuambie tu Watanzania asilimia kubwa sio walipaji
Hii ya kutokulipa kwa Watanzania ni kama hulka. Achilia mbali mikopo, mtanzania hata akiazima chaja tu ya simu HAIRUDISHI KAMWE mpaka wewe uliemuazima uanze kuifuatilia na saa nyingine uzungushwe wee..!
 
CRDBni bank ya ovyo sana kwa wafanyabiashara wadogo na wakati. Mikopo yao kwa kiasi kikubwa inawalenga wafanyakazi hasa wa serikalinj na mashirika makubwa.
Daaaah! Ni kweli nina jamaa yangu yupo mgodini huko Tarime inaelekea mwezi sasa mkopo hawampi wanamzungusha mpaka ameomba asitishe aende NMB sijui ndio tabia ya bank au ya watoa huduma wao.
 
Back
Top Bottom