ningekushauri tu ufuatilie kwenye mtandao wako badala ya kuanza kelele kwa vitu vya ajabu, mimi natumia iyo huduma ya iyo benki na watu wengi tu wanatumia iyo kitu ivyo ingefaa ungeomba ushauri badala ya kukimbilia kuleta mada. Ivi ni lini hao CRDB wakamiliki mtandao wa simu?yani unataka Vodacom au tigo au airtel wakikugomea kupata huduma kwao ambayo iko kwa third party wewe unamlaumu thirdy party? Sasa ulitaka CRDB wamlazimishe service provide akuruhusu uweze ku access akaunti? yaani uko kwenye foleni toka ubungo kwenda Ikulu magogoni, ukutane na Traffic pale mataa ya magomeni akuzuie kwa muda then ulaumu ikulu kwa kutomwambia traffic akupitiushe kwa lazima?does it make sense???
Binafsi uwa sipendi kuharibu public image au business za watu kama ivi, inafaa uende kwa Voda/airtel/tigo wakupe jibu KAMA HAUKURIDHIKA then uende CRDB wakakupe majibu ya uhakika, kama wakikujibu ovyo apo uje kwetu Jf tulalamike kwa pamoja kwa kampuni inayotoa huduma mbovu ila ili la kuamua umrushie nani tuhuma limekaa ovyo!
Mtu hauna salio la kutuma sms voda/tigo/airtel kualert kuwa unahitaji huduma flani toka kampuni flani eg CRDB...then wewe unataka utumie bure huduma ya mtandao wa simu kupata huduma kwa kampuni nyingine bureee!!inaleta mantiki?au unadhani mtandao wa simu upo kuisaidia iyo CRDB kupata faida?? Ukitaka huduma CRDB then nenda uko CRDB kama ukitaka huduma ya CRDB kwa kupitia mtu mwingine/Mtandao wa simu, lazima umpe gharama za kupeleka request yako uko ulikomtuma/CRDB , tofauti na hapo tunataka tu vya bure/dezo kitu ambacho mtandao wa simu hautakubali, yani kutuma sms alert/request bure kwa kampuni yako unayotaka ikuhudumie!! kwa ivi wengi tutabaki kuwa walalamikaji milele katika kulazimisha free service!