CRDB yaamuriwa kumlipa Zawadi Bahenge milioni 300 kwa kutumia picha yake kwenye matangazo bila ridhaa

Huyo dada aliwahi jitangaza miaka flani kuwa ni muathirika.
Picha zake zilikuwa zikitumika kama namna ya kuhamasisha jamii.
 
Hiyo hela ni nyingi sana! Milioni 20 au 30 ingetosha. CRDB wakate rufaa kiasi cha pesa kipunguzwe. Sijui vigezo gani vilitumika hadi Mahakama iamue huyu mama ntilie alipwe milioni 300. Halafu kumbe ndiyo mchezo wake. Lione linavyochekelea. Hakuna mtu anayemjua huyu kibibi. Hana brand name au brand recognizance kama Alikiba au Diamond Platnumz na hajapata madhara yoyote hadi alipwe fidia ya milioni 300.
 
Tukiwambia hamna akili mnachukia.
 
Kwanini ni yeye tu dhidi ya makampuni makubwa nchini?
Makosa kama haya yanafanywa na makampuni mengi mno hata dakika hii tunavojadili hapa. Unakuta mfanyakazi kaajiriwa kazi ya mapokezi anapigwa picha na kampuni iliyomuajiri kisha kuitumia katika matangazo ya biashara bila ridhaa yake. Sema wabongo wengi tuna ile kusema sina muda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…