Credibility Check: SBT Japan Kampuni ya Kuuza Magari

Credibility Check: SBT Japan Kampuni ya Kuuza Magari

Wapendwa wana Jamvi,

Niko kwenye mawasiliano na hii kampuni inayojishughulisha na kuuza magari yaliyotumika huko Japan. Wenye hii kampuni ama ni wahindi au Wapakistani. Nimeongea nao kwa simu na kupitia skype pia. Wanataka kuniuzia gari na makubaliano yapo katika hatua za mwisho. Sijawahi kufanya biashara na hawa watu, hii itakuwa ni mara yangu ya kwanza.

Kwa kuwa pesa itakayotumika kwenye manunuzi ni kubwa, nimeogopa kuendelea na hii deal bila kutafuta ushauri. Je kuna mtu amewahi kufanya nao biashara hawa jamaa? Wako genuine kiasi gani?

Naogopa kuuvaa mkenge mchana kweupeee!!!!!.

Tiba

Mi nishafanya nao tena mzigo nimeupata November niliagiza October. Cjaona kama ni wajanja wajanja na kwa kweli gari niloipata iko vizuri saana. Nakushauri endelea nao tu cóż uzuri SBT hii ni site Yap tofauti na Bfoward na Car trade view ambazo ni free site. So u receive what u ordered.
 
Mbona utaji haina ya gari mkuu?au itakua hiyo tu Tanzania mzima
 
Nipitiamichango ya wadau katika hii topic wengi wanakushauri usiitumie hii kampuni. Sababu kubwa ni magari kusafirishwa kabla hayajanunuliwa na wengine wanasema ucheleweshaji. Mimi nimenunua magari mawili moja mwaka jana na lingine 2009 toka katika kampuni hii bila matatizo yoyote. Hivi karibuni wameanza kusafirisha magari kabla hayajanunuliwa nahisi kama walikuwa wanafanya majaribio. Cha kufanya pitia zile email zao zenye attachment list ya magari waliyotuma hakikisha hilo halimo halafu ndio uliagize. Kuhusu ucheleweshaji wa kusafirisha sikupata usumbufu hata kidogo tarehe nilizotajiwa ndio meli ilifika bongo. Kabla ya kununua uliza ni Meli gani watatumia nawe fanya reseach kujua hiyo meli iko wapi tumia google. Kumbuka kuna Meli zinazunguka kupitia Singapore, South, Msumbiji to Dar zinatumia muda wa kama mwezi na siku 10 na zile za moja kwa moja kama mwezi hivi yote kwa yote gari inafika.
Ushauri wangu:
Usinunue gari kwa kampuni ambayo hata nembo yao hujawahi kuiona katika gari lolote hapa bongo.
Kama una uwoga mkubwa tumia Tradecarview kwani huo ni mnada wa magari na hela inatumwa kwa account ya Carview sio kwa muuzaji. Muuzaji hupewa pesa yake pale atakapokuwa amekutumia BL.
Binafsi nimenunua gari hivi karibuni kupitia Carview (muuzaji alikuwa RealmotorJapanJR) CIF ilikuwa USD 4000 na Carview wao USD kama 200 hivi.
SBT, Beforward & Carview ni wazuri tu inabidi uwe good communicator usiwe internet shy.
Goodluck

Mkuu nakushukuru kwa mchango wako. Nitafuata ushauri wako kwa karibu.

Tiba
 
Mbona utaji haina ya gari mkuu?au itakua hiyo tu Tanzania mzima

Mkuu unataka nikutajie aina ya gari ninalolitaka wewe ni supplier inawezekana unalo?

Tiba
 
Mi nishafanya nao tena mzigo nimeupata November niliagiza October. Cjaona kama ni wajanja wajanja na kwa kweli gari niloipata iko vizuri saana. Nakushauri endelea nao tu cóż uzuri SBT hii ni site Yap tofauti na Bfoward na Car trade view ambazo ni free site. So u receive what u ordered.

Asantr mkuu kwa ushauri.

Tiba
 
Huko tradecarview kuna makampuni elfu kidogo, hata sbt na beforward wapo pia humo tradecarview kwa sababu wenyewe ni kama platform tu. BTW, sbt nimewahi kufanya nao kazi mara mbili, mara ya kwanza ilienda vizuri, japo gari ilikaa miezi miwili ndiyo ikafika bongo (ni kawaida hata beforward huwa inatokea, kuna gari nimeagiza toka dec lakini haijaingia mpaka leo, sina shaka nao). Gari ya pili sbt ilikuwa Disco III, kwanza wakaniambia ipo watanitumia picha, nikakaa wiki nzima bila picha, baadaye wakanipigia wakasema "you know the car is in uk"...sawa nataka picha.."will send"...wiki nyingine, baadaye wakatuma picha moja tu!!! rangi tofauti na niliyokuwa nataka, wakati huo wananiambia nitume pesa haina shida gari nyeupe ipo!!!! Nikasource kwingine nikapata nyeupe ikaja faster tu, nikauza nikatia mpunga wangu mfukoni. Hawa jamaa wanatuma tu migari yao bongo mi nilidhani wana bonded warehouse kumbe hamna, magari yanakaa bandarini mpaka yanapigwa mnada na TRA, kwa hiyo unaweza ukaagiza gari uliyoiona kwenye site yao, bahati mbaya ukakuta wana gari ya aina hiyohiyo ambayo tayari iko bandarini dar wanakushikisha hiyohiyo!! kikubwa kaka Tiba sijajua hiyo gari unayotaka ni gari gani, kukuliza pesa sijawahi kuskia wameliza mtu pesa zaidi ya kubadili gari, kama unaamua kudeal nao wakuhakikishie kwanza gari iliko, isije kuwa either liko bongo linahesabu storage au liko mbali zaidi kiasi mpaka wafanye utaratibu wa kukutumia ni mbinde. Ungetaja aina ya gari au ukatuma picha au stock namba ningekusaidia kufanya research kujua liko wapi.

Mkuu nitakuPm nikupatie stock number ya hilo gari. Asante kwa kujitokeza kunisaidia.

Tiba
 
Last edited by a moderator:
SBT wako poa niliagiza gari kwao.....lilikuja bila shida yoyote kwa muda ule ule. Tatizo lao wako aggressive sana kwenye mawasiliano........utakuta kwenye simu, email, Skype, Sms etc. Mimi nilikuwa nadeal na Mohamed Afraz.

Mkuu asante kwa mchango wako na ushauri.

Tiba
 
Hawa jama wa SBT ninamiaka karibu 2 nafanya nao kazi mimi huwa nawapa credit kubwa kwasababu wanajua biashara wanaku upadte kila hatua pia hata kama huna haja na gari watakukumbusha tu so wako serious na kazi sio tatizo letu huwa tuanjaribishiwa kufanya biashara kama wewe hapo sasa hivi unapresha kubwa wewe tuma hiyo pesa halafu huyo peter wa SBT ndo manager wao kwa tanzania ndo maana wameona unataka kununua lakini unawasiwasi na hao sales account wako ndo maana anapewa boss wao ajaribu kuzungumuza na wewe pia swala ya kuwa ni wapakstani is not an issue kwasababu mbona afraz nimefanya naye pia kuna dada wa indonesia pia anaitwa Maricon Bais pia anashingilia account za watu hapa tanzania bishara ni matanganzo kama unaogopa kupingiwa simu so watajuaje au watafanyaje biashara you have to know also they doing business sio wanakaa kama sisi hapa bongo unasubiria wateja na biashara yako ya nyanya(Prof muhongo said).
ni pm nikupe direction it so easy to do business online nowdays.
 
SBT ni kampuni nzuri na ya mda mrefu sana,naona kuna bwana hapo juu aliogopa kidogo uliposema uliongea na mpakistani,biashara ya magari Japan na Dubai imeshikiliwa na wa Pakistan hivyo usishtuke,75% ya used car dealers Japani ni wapakistani ukiongea na Mjapani wengi wameajiriwa tu,Dubai AL AWEER ndio sehemu kubwa duniani inayouza magari used ya mkono wa kulia na almost 90%ya showroom ni za wapakistani,kuna siku nilimwuliza jamaa mmoja Dubai kwanini showrooms nyingi ni za wapakistani akaniambia hawa jamaa wanapesa nyingi sana za unga hivyo wengi wao wanaamua waziweke kwenye magari kama biashara(sina uhakika).
Turudi kwenye mada hiyo kampuni ipo na ni nzuri lakini wauza magari wanatabia ya kuchukua order na baada ya hapo wanakutafutia gari wanazunguka minadani mpaka watalipata, na wakilipata watachezea odometer na kusoma KM zozote ambazo mteja anataka.Kuna bwana mmoja hapo juu alisema aliagiza gari wakamwambia lipo UK ni kweli wanafanya hivyo gari linawezakuwa lefthand drive wakabadili likawa righthand drive ndivyo biashara hii ilivyo(sio wote).
Wasiliana nao usiogope kwamba ni wa Pakistani,matatizo ya used cars yapo kwa dealer wengi sana,maana gari zao nyingi ni za ukarabati,niliwashanunua Rav 4 toka kwenye kampuni kubwa sana walisema ni 2004 model lakini baada ya kuikagua chasis nikagundua ni 2002,niliwainunua hiace ikasumbua gearbox baada ya kuifungua nikakuta ilikuwa ya kichina!!!matatizo kwenye used cars yapo,ndio maana njia nzuri ya kununua used car ni kuliona na kulichambua otherwise ni gamble tu.
 
Wapendwa wana Jamvi,

Niko kwenye mawasiliano na hii kampuni inayojishughulisha na kuuza magari yaliyotumika huko Japan. Wenye hii kampuni ama ni wahindi au Wapakistani. Nimeongea nao kwa simu na kupitia skype pia. Wanataka kuniuzia gari na makubaliano yapo katika hatua za mwisho. Sijawahi kufanya biashara na hawa watu, hii itakuwa ni mara yangu ya kwanza.

Kwa kuwa pesa itakayotumika kwenye manunuzi ni kubwa, nimeogopa kuendelea na hii deal bila kutafuta ushauri. Je kuna mtu amewahi kufanya nao biashara hawa jamaa? Wako genuine kiasi gani?

Naogopa kuuvaa mkenge mchana kweupeee!!!!!.

Tiba

Habari, yeah ni vizuri kuondoa kupata ushauri ili uwe na uhakika ya unachoenda kukifanya. Binafsi hawa jamaa nilikaribia kufanya nao biashara miezi michache iliopita, baadae nilisita baada ya kuona wao wananisumbua sana kwa kunipigia pigia simu kila wakati kama vile wananilazimisha tufikie mwafaka. Sina hakika sana juu ya uaminifu wao lakini sina imani nao kabisa.
Binafsi nimeshanunua gari kwenye kampuni mbili tofauti; ilionivutia zaidi ingawa bei zao ni kama ziko juu ni kampuni ya AUTOREC. Gari zao ni kama mpya, lakini pia wanatoa waranti. Ushauri: Pesa mama ikishakutoka ndio basi tena ni kama maji, kama utaipata basi itakuwa sio ile tena; vizuri uwe na uhakika wa 100% ya unachokwenda kukinunua, rahisi mara nyingi huwa garama zake baadae.
 
Hawa jama wa SBT ninamiaka karibu 2 nafanya nao kazi mimi huwa nawapa credit kubwa kwasababu wanajua biashara wanaku upadte kila hatua pia hata kama huna haja na gari watakukumbusha tu so wako serious na kazi sio tatizo letu huwa tuanjaribishiwa kufanya biashara kama wewe hapo sasa hivi unapresha kubwa wewe tuma hiyo pesa halafu huyo peter wa SBT ndo manager wao kwa tanzania ndo maana wameona unataka kununua lakini unawasiwasi na hao sales account wako ndo maana anapewa boss wao ajaribu kuzungumuza na wewe pia swala ya kuwa ni wapakstani is not an issue kwasababu mbona afraz nimefanya naye pia kuna dada wa indonesia pia anaitwa Maricon Bais pia anashingilia account za watu hapa tanzania bishara ni matanganzo kama unaogopa kupingiwa simu so watajuaje au watafanyaje biashara you have to know also they doing business sio wanakaa kama sisi hapa bongo unasubiria wateja na biashara yako ya nyanya(Prof muhongo said).
ni pm nikupe direction it so easy to do business online nowdays.

Mkuu kwa kauli ya huyo ninaye wasiliana naye hawana agent hapa Tanzania kwa sasa ila wako mbioni kuwa na ofisi. Hata hivyo tumezungumza na kufikia hatua nzuri. Tumekubaliana nitume 50% ya gharama ya gari halafu wao wafanye shipping arrangements. Wakimaliza watanitumia scanned copy ya bill of landing. Nikiishapata hiyo bill of landing na kuhakikisha kwamba gari iliyokuwa shipped ndio hiyo niliyokubaliana nao kununua nitume 50% iliyobaki na wao wanitumie Orginal bill of lading.

Ila jamaa wako aggressive sana katika biashara.

Tiba
 
Mkuu kwa kauli ya huyo ninaye wasiliana naye hawana agent hapa Tanzania kwa sasa ila wako mbioni kuwa na ofisi. Hata hivyo tumezungumza na kufikia hatua nzuri. Tumekubaliana nitume 50% ya gharama ya gari halafu wao wafanye shipping arrangements. Wakimaliza watanitumia scanned copy ya bill of landing. Nikiishapata hiyo bill of landing na kuhakikisha kwamba gari iliyokuwa shipped ndio hiyo niliyokubaliana nao kununua nitume 50% iliyobaki na wao wanitumie Orginal bill of lading.

Ila jamaa wako aggressive sana katika biashara.

Tiba

Yap Tiba, unatoa nusu gari ikifika Dar port unamalizia. Mimi mwenyewe walinifanyia hvo. Pia huwa wananipigia cm kuulizia kama nataka kununua tena. Wako Very serious kufanyafolloup.
 
SBT sio wabaya, sio matapeli pia.
Ila wasumbufu kwenye mawasiliano, wanaweza wakakupigia hata mara 10 kwa siku so inakua kero.
 
Mi nishafanya nao tena mzigo nimeupata November niliagiza October. Cjaona kama ni wajanja wajanja na kwa kweli gari niloipata iko vizuri saana. Nakushauri endelea nao tu cóż uzuri SBT hii ni site Yap tofauti na Bfoward na Car trade view ambazo ni free site. So u receive what u ordered.

Unmaanisha nini hapo kwenye red?
 
Hata mimi niliwakimbia. Hiyo marketing strategy inaleta wasiwasi sana. Nilichagua gari na tukakubaliana. Ikawa simu,email kila siku. Siku nakwenda kudeposit wakapiga simu nipo benki somebody Sande, roho yangu ikaghairi nikaacha.
 
Unmaanisha nini hapo kwenye red?

Namaanisha kuwa, SBT wanauza magari yao kwa kutumia site yao(webpage), wakati Befoward na Car trade view ni free site. Wao wanauza magari ya wateja na wanachukua commission.
 
Namaanisha kuwa, SBT wanauza magari yao kwa kutumia site yao(webpage), wakati Befoward na Car trade view ni free site. Wao wanauza magari ya wateja na wanachukua commission.

be foward sio free site
 
Namaanisha kuwa, SBT wanauza magari yao kwa kutumia site yao(webpage), wakati Befoward na Car trade view ni free site. Wao wanauza magari ya wateja na wanachukua commission.

Ni tradecarview pekee ndiyo hawauzi magari, beforward wanauza magari na ndiyo kampuni inayoongoza kuuza magari used africa kwa sasa, nao pia unaweza kuwapata kwenye website yao Japanese Used Cars | BE FORWARD, ni kampuni kama sbt, na hata sbt nao pia wanauzia tradecarview, autotrader na kwingineko. Ni chaguo la mnunuzi tu, unakoona gari zuri kwa bei umeipenda unanunua kokote.
 
Hata mimi niliwakimbia. Hiyo marketing strategy inaleta wasiwasi sana. Nilichagua gari na tukakubaliana. Ikawa simu,email kila siku. Siku nakwenda kudeposit wakapiga simu nipo benki somebody Sande, roho yangu ikaghairi nikaacha.

Hahahaa, ukaona kama wanakuvuta wakulize?..sbt sijawahi kuskia wameliza mtu pesa, lakini wana mambo yao ambayo yanakera wakati mwingine utafikiri unadeal na kanjanja flani mwenye njaa!
 
Hata mimi niliwakimbia. Hiyo marketing strategy inaleta wasiwasi sana. Nilichagua gari na tukakubaliana. Ikawa simu,email kila siku. Siku nakwenda kudeposit wakapiga simu nipo benki somebody Sande, roho yangu ikaghairi nikaacha.

Customer Service kwenye nchi yetu ipo chini sana,ukiingia dukani mwenye duka anakukodolea macho kama vile umepotea njia,sometime anakuwa busy na game kwenye simu yake,ukitoa pesa bila aibu anakwambia hana chenji!!!wenzetu wanajua umuhimu wa mteja,wanajua bila wewe wao si kitu ata ukienda kwenye malls zao hawatazami una simu gani au umeshuka kwenye gari gani wataonyesha kukujali sana.Ni kweli hao jamaa wanafuatilia sana mteja kwa simu,mails nk.Kwa sisi ambao hatujazoea tunajua tunaibiwa.
 
Back
Top Bottom