Cristiano Ronaldo aendelea kutisha ndani na nje ya uwanja anunua gari la bei kubwa katika historia ya dunia bilioni 43 hakuna mwingine atakayelinunua

Cristiano Ronaldo aendelea kutisha ndani na nje ya uwanja anunua gari la bei kubwa katika historia ya dunia bilioni 43 hakuna mwingine atakayelinunua

Utakuta billget na jeff bozzes wanatembelea range
 
Acha uzushi uo. Sasa kwanini wengine washindwe kununua? Je hao wanaomfadhili na kumlipa mshahara watashindwaje wao wakiamua kununua?

Ronaldo bado hajawa Tajiri kwenye wanaoitwa matajiri huko ulaya. Ni tajari kwa maskini tu.
 
Acha uzushi uo. Sasa kwanini wengine washindwe kununua? Je hao wanaomfadhili na kumlipa mshahara watashindwaje wao wakiamua kununua?

Ronaldo bado hajawa Tajiri kwenye wanaoitwa matajiri huko ulaya. Ni tajari kwa maskini tu.
Mkuu gari hilo limetengenezwa moja tu ...hivo hakuna gari lingine la namna hiyo litakalotengenezwa tena.
 
Mkuu gari hilo limetengenezwa moja tu ...hivo hakuna gari lingine la namna hiyo litakalotengenezwa tena.

Mkuu hilo si jambo la ajabu kwa Majuu. Matajiri wanatengenezesha magari kwa design wanavotaka wao. So sio big deal kabisa.

Yeye Ronaldo amejipiga kabisa na kutumia karibu robo 3 ya mshahara wake kulinunua. Wengine kwao bado zinahisabika ni vijicent tu.
 
Duh!! Lijamaa Lina nunua Gari Kama Lina Nunua Kitumbua vile.[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Dah mashabiki wa ronado, kichwa cha habari na taarifa yenyewe zinakinzana.

Ni tetec tu mjomba.
 
Lijue Gari ghali zaidi duniani, Cristiano Ronaldo atajwa kulinunua

Hili gari, Bugatti La Voiture Noire ndilo gari ghali zaidi katika historia ya dunia, likiwa linagharimu US Dollar Milioni 18.7 sawa na Tsh. Bilioni 43.1.

Gari hili lilizinduliwa Machi 5 mwaka huu kwenye maonyesho ya magari ya kimataifa, Geneva International Motor Show kuadhimisha miaka 100 tangu kuanzishwa kwa kampuni ya Bugatti.

Wakati wa uzinduzi wake, gari hili tayari lilikuwa limelipiwa na mnunuzi ambaye hakutaka kujulikana. Bwana huyo alilipia gari hilo hata kabla kutengenezwa kwenye kiwanda.

Kuna fununu ambazo zingali hazijathibitishwa kwamba gari hilo lilinunuliwa na nyota wa soka Cristiano Ronaldo.

Gari hili ambalo lina injini yenye ukubwa wa 8,000cc na turbo nne, linabeba abiria wawili na linaweza kuenda kasi ya kilomita 465 kwa saa. Kampuni ya Bugatti ilitengeneza toleo moja pekee ya La Voiture Noire. Hivyo basi hakuna mwingine atakayekuwa na gari sawa isipokuwa aliyenunua hili toleo.

Watu wana hela ila hela hazina watu...mwandae mwanao awe mcheza soka akishindwa masumbwi pesa zipo nje nje.
Kampuni inatimiza miaka mia.......afrika hatupo duniani tunaishi mwezini kuwasindikiza wa duniani
 
43.1 Bilion Tshs.napigia hesabu ya bus za Yutong hapa,unapata kama basi 215,ngoja nilale tu kwanza sitaki hata kuwaza...
Kwa kila moja bei gani ambalo limekamilika mpaka kuingia barabarani
 
Back
Top Bottom