Cristiano Ronaldo asema Messi anatakiwa kuondoka Spain kuthibitisha ubora wake

brave one

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
4,879
Reaction score
7,386
Mchezaji nguli wa soka duniani Cristiano Ronaldo amemtaka mpinzani wake wa muda mrefu Leonel Messi kukubali challenge yake ya kumtaka kuondoka Spain ili kupata changamoto zingine kuthibitisha ubora.
Ronaldo" nimecheza ureno, uingeleza, uhispania na Sasa Italia liking yeye Messi muda wote yupo Spain, kwangu Mimi maisha ni changamoto, nahisi atakuwa amenimisi, Nampa changamoto akubali aondoke Spain aje Italy japo naheshimu maamuzi yake".
 
Angetaka changamoto angeenda Ac Milan
eti ameenda Juve miaka saba wanabeba kila kombe la ndani
umeenda kupata challange ya nini
kama Messi aende bayern munich kutafuta changamoto au psg

kakaa miaka 9 kachukua la liga mara mbili tu huku mwenzie akichukua mara sita

halafu nimeona kitabia cha kumuongelea messi ili ukae kwenye headlines alianza Maradona kujifananisha na Messi akafata Pele juzi juzi tu hapa sasa ronaldo

cr7 kaona hakuna mwenye shida naye na wakulima wenzie kaamua amuongelee messi
Messi ataongea uwanjani tu hana muda na nyinyi
 
Kama tukitumia kigezo kwamba Messi sio bora sababu tu, amechezea timu moja basi naamini hata Pele hafai kuwa namba moja kwani amechezea Santos miaka 18 na miaka yake miwili ya mwisho kamalizia soka lake Marekani.
 


Mashabiki wa Ronaldo mna tabu sana...alianza Maradona kujifananishanae, kaja Pele and now Ronaldo...since soka lianze kuchezwa hapa duniani mpaka now hakuna kama King Messi.
 
Na Messi naye angetaka tumuone bora angehamia Girona si Barcelona tu kazungukwa na mastaa
 
Maradona alitoka Barcelona akahamia Napoli ikiwa timu ndogo sana, akaipa jina mpaka leo, Messi naye kama kweli ni mfalme wa soka atoke huko mafichoni aende kwenye ligi zingine ili tujue kama Jogoo la shamba linaweza wika mjini
 
CR7 mpaka sasa anaongoza kwa ufungaji kwenye ligi ngeni kwa mwaka wake wa kwanza tu. Ana magoli mengi, asists nyingi na short on target tu ziko karibu mara mbili ya anayemfuata kwa ufungaji. Wale hater wa CR7 waliokuwa wanasema penalti ndio zilikuwa zinambeba wako wapi. Wale waliokuwa wakisema yeye ni mbinafsi, hizo assists nyingi zimewaumbua
Hongera CR7 Mfalme wa soka kwa kizazi hiki, takwimu zinakutetea

  1. Cristiano Ronaldo
    Juventus
    117 per goal
    1635 played
    14 Goals scored
    5 Assists
    51 Short on target
  2. Krzysztof Piatek
    Genoa
    123 per goal
    1594 played
    13 Goals scored
    0 Assists
    31 Short on target
  3. Fabio Quagliarella
    Sampdoria
    129 per goal
    1548 played
    12 Goals scored
    5 Assists
    26 Short on target
 
Na Messi naye angetaka tumuone bora angehamia Girona si Barcelona tu kazungukwa na mastaa


Akili zingine bwana!! Yani hamkosagi maneno...yani atoke club bora duniani inayomlipa pesa nyingi kuliko mchezaji yeyote yule unaemjuwa, alafu wewe unasema aende girona!! Kuweni serious bwana.
 


Ufalme umempachika wewe tu, dunia haitambui hilo.
 



Hahahaa Haters mnapata tabu sana kwa king Messi 🤣🤣🤣 pole sana.

Wewe kama unaujuwa mpira vizuri huwezi ukam-compare striker na attaking midfielder...ni vitu viwili tofauti kamanda.... So huyo striker wako ataachaje kupata goli nyingi! Ebu jiulize tu hiyo nafasi mwanzo si ilikuwa ya HIGUAIN! so higuain alikuwa striker or attaking?? Nyie watu wa ajabu sana. Hata kuwaelewesha ni kazi bure tu.

[/QUOTE]
 
Na Messi naye angetaka tumuone bora angehamia Girona si Barcelona tu kazungukwa na mastaa


King na Barca ni kama baba na mama, so hawezi kuhama hama kama mtoto aliyekosa wazazi....umenipata!!!!
 
Hebu pitia maadnishi yako tena, ni lini Messi amekuwa Attacking Midfielder. Kwa namba ipi
Nafasi zote CR7 anazocheza Messi ndizo Messi anazocheza. False 9 (2012 wakati wa PEP na akavun ja rekodi ya ufungaji), winger wa kulia mara nyingi tu. Tangu enzi za PEP mesi amekuwa akicheza forward akibadilishwa ni winger wa kulia mara chache kushoto. Pole sana naona umechanganywa na uwezo wa Mesi wa ku-drible ukadhani ni MF
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…