Csee 2013 examination results ranking & division

Csee 2013 examination results ranking & division

Naomba Niulize Jaman, Kwahiyo Watakao Kwenda Vyuon,polis Na Ualimu Watakaopata Ngapi?
 
A: 75-100, B+:60-74, B:50-59, C:40-49, D:30-39, E:20-29 na F:0-19 kwa sasa

A:80-100, B:65-79, C:50-64, D:35-49 na F: 0-34 kwa zamani

Hapo kwenye red mkuu zama zetu ilikuwa hivi A:81-100 na B:61-79, C:41-60, D:21-40 na F:0-20
 
Sasa inakuaje upangaji Mf. Kuna kijana kapata A moja, B sita, na C tatu lakini wameonesha kapata Div II points 19 naomba mnyumbuliko kwa anaefahamu.

kwa kawaida huwa yanaangaliwa masomo 7 aliofaulu zaidi kwenye upangaji wa madaraja. A=1 na B=3, kwa A moja na B sita ni sawa na (1x1)+(6x3)=19.
Hivyo basi 19 ni daraja la II. Bila shaka umenipata kwa huo mnyumbulisho! Dada Salome
 
Tunaomba kauli ya serikali kuhusu viwango hivyo maana kila mmoja anasema anachojua
 
mimi naomba kujua kwa wale waliopata division four ya point 32,33 na 34 wataenda wapi?.
 
Jamani mi ningependa kujua maana kuna mtoto wa jirani anataka akasomee ualimu hivyo mwakan wanaanza kuchukua kuanzia point ipi? Ile ile ya 27?
 
Kinacho nishangaza kuna watu wana points 41 wana div 0 na kuna wengine wana points 44 wana div 4 yaani hapo ndio nilipo pigwa bumbuwazi
Mimi nimebaki kimya maana wanatuona sisi wajinga wakati walishatuelimisha tukaelimika,tunakoelekea hadi wataweka G na H.
 
Sasa inakuaje upangaji Mf. Kuna kijana kapata A moja, B sita, na C tatu lakini wameonesha kapata Div II points 19 naomba mnyumbuliko kwa anaefahamu.

Hapo iko hivi, wanachukua masomo saba tu aliyofanya vizuri, na kila grade ina point zifuatazo
A = 1, B+=2, B=3, C=4, D=5, E=6, F=7.
kama ana B sita hapo atakua na point 18 jumlisha A moja unapata 19.
 
Jamani mi ningependa kujua maana kuna mtoto wa jirani anataka akasomee ualimu hivyo mwakan wanaanza kuchukua kuanzia point ipi? Ile ile ya 27?

Sio mwakani, kuanzia mwaka huu wanachukua point 27 mwisho
 
Kinacho nishangaza kuna watu wana points 41 wana div 0 na kuna wengine wana points 44 wana div 4 yaani hapo ndio nilipo pigwa bumbuwazi

Wana jamvi naomba mnifuatilie kwa makini juu ya ufafanuzi wa matokeo haya. Naomba nianze upya kuwaelezea jinsi ya upangaji wa madaraja yaani divisions kama ifuatavyo:-
Div. I: Pts 7-17
Div.II: Pts 18-24
Div.III: Pts 25-31
Div.IV: Pts 32-40 + (41,42 43,44,45,46)
Div. O: Pts. + (41,42,43,44,45,46), 47-49
Hizo point zilizopo kwenye mabano zinaingia kotekote kama inavyoonekana yaani ukiwa na moja kati ya point hizo, factor nyingine huangaliwa, factor hizo ni ufaulu katika somo moja moja, yaani kama kuna A moja au B moja au C moja au D mbili, basi hapo daraja la nne yaani Div. IV hutolewa.
Lakini kama hakuna hata A moja, au B moja, au C moja, au D mbili basi daraja O yaani Div. O hutolewa.

Nadhani nimeeleweka.
 
A = 1, B+ = 2, B = 3, C = 4, D = 5, E = 6 na F = 7 kwa hiyo huyo aliyepata A moja na B sita na C tatu... = 1(A) + 6(B) = 19
 
Back
Top Bottom