Tetesi: CUF: Lipumba kuwafuta uanachama wabunge wote wa kuchaguliwa majimbo yote ya Bara

Tetesi: CUF: Lipumba kuwafuta uanachama wabunge wote wa kuchaguliwa majimbo yote ya Bara

TangataUnyakeWasu

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2016
Posts
1,268
Reaction score
1,611
CUF HAITAKUWA IMARA TENA! MISSION IMEKAMILIKA KWA 80+℅

CUF sasa inaishilia, ni kama mpango unakamilika, mpango mkakati umetengenezwa kimkakati zaidi, kuhakikisha CUF haina nguvu tena, ili kuleta unafuu visiwani. Wabunge wa majimbo wakishavuliwa uanachama, majimbo yao yatakuwa wazi, uchaguzi utarudiwa, kama hujui ni mpango,: kumbuka kauli ya juzi ya mkurugenzi wa tume ya uchaguzi, pale aliposema' ikiwa wabunge wa CUF watavuliwa uanachama, tume imejiandaa kwa dharula yoyote na bajeti ipo! Akili kumkichwa' mkurugenzi wa tume anazungumzia uchaguzi mdogo kwenye majimbo ambayo bado yana wabunge! MISSION

Lipumba sasa anatambuliwa na kila taasisi ya sirikali, anatambuliwa na Bunge, anatambuliwa na Msajili, anatambuliwa mpaka na taasisi ya jikoni! MISSION

Kete kwa upande wa CUF Halisi ilikuwa imebaki moja tu (MAHAKAMA) baada ya makosa kufanyika nyuma! Ndiyo makosa yalifanyika mwanzo kabisa kwa upande wa Maalim Seif kumdharau Lipumba na kumuona ni mtu mmoja tu anayetapatapa kisha atatulia, hawakumuona mapema aliyekuwa nyuma ya Lipumba! Hili lilikuwa Kosa kubwa! Wamekuja kushituka na kuiona nguvu yake kipindi ameingilia bodi ya wadhamini ya CUF! Hapo ndo walishituka na kumbe tayari walikuwa wamechelewa! Walipaswa kumshughulikia mapema!
Sasa kete ya mahakamani nayo inaanza kufeli, kwa nini nasema inafeli?

1😛amoja na kesi ya kutomtambua Lipumba na kauli ya Msajili kuwa mahakamani! Bado Lipumba ameendelea na shughuli za chama kwa kujitanua hadi kufukuza wabunge bila woga na hakuna mhimili unaohoji!

2: Kutupiliwa mbali kwa mapingamizi ya wabunge wa CUF waliovuliwa uanachama, ni pigo kubwa kwa upande wa Maalim Seif! Hata wakirekebisha vifungu walivyotakiwa kuvirekebisha, wao wako mahakamani, Lipumba anaendelea na shuguli za chama huku akijipanga kuwaita na kuwahoji wabunge wa majimbo!

3: Kutotambulika kwa maazimio ya CUF upande wa Maalim wa kuwavua ubunge wabunge wawili ni pigo kubwa pia.

NANI ALAUMIWE

1. Mtatiro;
Ndiyo, huyu ni mtu wa kwanza kabisa kulaumiwa na wana CUF' atanisamehe. Yeye alipewa jukumu kuwa mwenyekiti wa kamati ya uongozi ya CUF, Lakini amekuwa akifanya siasa za mtandaoni zaidi, kila Lipumba akifanya jambo, yeye huja kulalamika mtandaoni na hukomea kuandika tu bila ya kuelezea njia mbadala ( rejea post zake kwenye plofile yake) Sasa kama yeye kiongozi analalamika na kujibu mapigo ya Lipumba mtandaoni, wengine watafanyeje? Yeye huiongelea CUF baada tu ya Lipumba kufanya kisanga, Lipumba akiwa kimya' na yeye yuko kimya. Kwa hiyo amekuwa akicheza ngoma ya Lipumba!

2. Maalim Seif
Yeye namlaumu kwa kutochukua hatua mapema, Lipumba hakupaswa kupewa nafasi mapema, naye sasa amekuwa akijibu mapigo ya Lipumba tu badala ya Lipumba kujibu mapigo yake! Lipumba akiita Baraza lake, naye anaita lake, Lipumba akifukuza wabunge, naye anafukuza! Amechelewa sana!

NINI CUF YA MAALIM IFANYE?
Kwa sasa CUF ya Maalim imebanwa sana na Lipumba, na naona imebakiwa na option mbili tu!

1. Mahakama;
Mahakama pekee kwa sasa ndo imebaki kuweza kuamua kama CUF iwe ya Lipumba au ya Maalim. Na ikitokea mahakama ikaamua kuwa CUF iwe ya Lipumba, Maalim atabaki na option mbili tu, mosi kuungana na Lipumba au

2. Kuongeza nguvu CHADEMA.
Option ya mwisho kabisa kwa Seif ni kutangaza kuachana na siasa za CUF ya Lipumba na kuongeza nguvu upande wa CHADEMA. Faida kubwa kwa upande wa CHADEMA ikiwa hili litatokea, ni kupata wafuasi wengi Zanzibar bila chenga! Na hapo ndipo msemo usemao "Waliokuwa nyuma ya Lipumba waliruka mkojo wakakanyaga kinyesi" utatimia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unapaswa kwanza ujue lengo la walio nyuma ya Lipumba.
Walio nyuma ya Lipumba wanataka Kumfuta Maalim uanachama ili;
☞ kumkosesha platform ya kuongelea mambo ya CUF
☞Kudhoofisha madai yake ya urais wa Zanzibar ambayo yamefikia mahali pazuri kwenye jumuiya za Kimataifa.

Ili kujua Maalim afanye nini lazima kujiuliza kwanza ;
Je, walioko nyuma ya Lipumba wakifanikiwa kumfutia Maalim uanachama (Kitu ambacho watafanikiwa ) , Madai ya urais wa Zanzibar ya Maalim kwenye jumuiya za Kimataifa yataathirika kiasi gani?

Kama hayataathirika basi Maalim apractice kile wazungu wanasema -Stop, look, listen, think and wait .

Kama yataathirika basi Maalim anaweza kuchukua ushauri wako hapo juu.
 
new era is coming,2020 ndio mwisho wa cuf kama jina, upinzani ni watu sio chama,upinzani hauwezi kufa, kinachoendelea saivi ni hasara kubwa kwa watawala,wanatumia mbinu zao nyingi sana kwa wakati mmoja ili kupambana na upinzani,

wanachofanya bila ya kujijua ni kujenga nguvu kubwa sana ya upinzani na sio kuua,binadam tulivyo tunajifunza kutokana na makosa,kila ujanja wanaotumia kukandamiza watu,unatafutiwa ufumbuzi, mbinu zao zikishamalizika nao wao watamaliza pia
 
Ni kawaida kiongozi kua na watu watakaoendana na mkakati wako.

Anachofanya lipumba sio kigeni na ni cha kawaida kama mwenyekiti WA CUF.

Japo nia yake in OVU tangu mwanzo kwakua anatumika.

Ila yeye lipumba hataki chama chake kitumike na cdm, anataka kitumike na ccm.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siasa sipendi ila Lipumba anavyowafanyia Wapinzani sio sawa alijiondoa ili kudhoofisha upinzani na ameamua kuja kuua kabisa upinzani haswa chama kilichomkaribisha... kama hawataki tena akae tu pembeni kuugua ukimwi sio lazima uambukize na wengine ili mfe wote
 
Kumuunganisha Maalim Chadema litakuwa kosa kubwa kuliko yote la kimkakati alilofanya Sizonje.
WE WILL BE A LEGION AND NOTHING CAN STOP US!

You never want your enemy to be united against you , Sizonje makes us more than united, he makes us strong.
 
Ukimlaumu Mtatiro utakuwa unamwonea tu. Kambi ya Maalim Seif ilifanya kosa kuchelewa kuziba nafasi ya Lipumba alipojiuzulu mwaka 2015. Kitendo cha kukaa mwaka mzima bila kuziba ile nafasi lilikuwa kosa kubwa linalotumiwa kuwavuruga.
Mtatiro alipewa uongozi mwaka 2016 na bado anategemea sana maelekezo ya Maalim Seif

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama ni kweli, Lipumba anaiua CUF kwa mikono yake na njaa zake.

Damu na Jasho la waliopigania CUF wakati wa uchaguzi wakati yeye akiwa mapumzikoni vitamuandama maisha yake yote.

Dhambi mbaya sana hii..

We umeiona CUF wakati wa uchaguzi juzi tu? Unajua bara CUF imejengwa na nani? Unakumbuka container la visu wewe? Unakumbuka Ngangari na Ngunguli ya inspector Omari Mahita?
 
Ukimlaumu Mtatiro utakuwa unamwonea tu. Kambi ya Maalim Seif ilifanya kosa kuchelewa kuziba nafasi ya Lipumba alipojiuzulu mwaka 2015. Kitendo cha kukaa mwaka mzima bila kuziba ile nafasi lilikuwa kosa kubwa linalotumiwa kuwavuruga.
Mtatiro alipewa uongozi mwaka 2016 na bado anategemea sana maelekezo ya Maalim Seif

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwa maana hiyo lipumba yupo sahihi si ndio?
 
Uchambuzi wa mleta uzi uko sawa kabisa.

Kwangu mm, option ya pili ndiyo yenye mashiko kumwezesha Seif kuendelea kuwa juu kisiasa hasa uchaguzi wa 2020. Lakini hofu yangu ni je jumuiya za kimataifa na madai ya Urais Zanzibar yatakuwa na impact ipi (positive or negative) maana tayari amehama chama ???

Hongera kwa uchambuzi mzuri...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CUF HAITAKUWA IMARA TENA! MISSION IMEKAMILIKA KWA 80+℅

CUF sasa inaishilia, ni kama mpango unakamilika, mpango mkakati umetengenezwa kimkakati zaidi, kuhakikisha CUF haina nguvu tena, ili kuleta unafuu visiwani. Wabunge wa majimbo wakishavuliwa uanachama, majimbo yao yatakuwa wazi, uchaguzi utarudiwa, kama hujui ni mpango,: kumbuka kauli ya juzi ya mkurugenzi wa tume ya uchaguzi, pale aliposema' ikiwa wabunge wa CUF watavuliwa uanachama, tume imejiandaa kwa dharula yoyote na bajeti ipo! Akili kumkichwa' mkurugenzi wa tume anazungumzia uchaguzi mdogo kwenye majimbo ambayo bado yana wabunge! MISSION

Lipumba sasa anatambuliwa na kila taasisi ya sirikali, anatambuliwa na Bunge, anatambuliwa na Msajili, anatambuliwa mpaka na taasisi ya jikoni! MISSION

Kete kwa upande wa CUF Halisi ilikuwa imebaki moja tu (MAHAKAMA) baada ya makosa kufanyika nyuma! Ndiyo makosa yalifanyika mwanzo kabisa kwa upande wa Maalim Seif kumdharau Lipumba na kumuona ni mtu mmoja tu anayetapatapa kisha atatulia, hawakumuona mapema aliyekuwa nyuma ya Lipumba! Hili lilikuwa Kosa kubwa! Wamekuja kushituka na kuiona nguvu yake kipindi ameingilia bodi ya wadhamini ya CUF! Hapo ndo walishituka na kumbe tayari walikuwa wamechelewa! Walipaswa kumshughulikia mapema!
Sasa kete ya mahakamani nayo inaanza kufeli, kwa nini nasema inafeli?

1😛amoja na kesi ya kutomtambua Lipumba na kauli ya Msajili kuwa mahakamani! Bado Lipumba ameendelea na shughuli za chama kwa kujitanua hadi kufukuza wabunge bila woga na hakuna mhimili unaohoji!

2: Kutupiliwa mbali kwa mapingamizi ya wabunge wa CUF waliovuliwa uanachama, ni pigo kubwa kwa upande wa Maalim Seif! Hata wakirekebisha vifungu walivyotakiwa kuvirekebisha, wao wako mahakamani, Lipumba anaendelea na shuguli za chama huku akijipanga kuwaita na kuwahoji wabunge wa majimbo!

3: Kutotambulika kwa maazimio ya CUF upande wa Maalim wa kuwavua ubunge wabunge wawili ni pigo kubwa pia.

NANI ALAUMIWE

1. Mtatiro;
Ndiyo, huyu ni mtu wa kwanza kabisa kulaumiwa na wana CUF' atanisamehe. Yeye alipewa jukumu kuwa mwenyekiti wa kamati ya uongozi ya CUF, Lakini amekuwa akifanya siasa za mtandaoni zaidi, kila Lipumba akifanya jambo, yeye huja kulalamika mtandaoni na hukomea kuandika tu bila ya kuelezea njia mbadala ( rejea post zake kwenye plofile yake) Sasa kama yeye kiongozi analalamika na kujibu mapigo ya Lipumba mtandaoni, wengine watafanyeje? Yeye huiongelea CUF baada tu ya Lipumba kufanya kisanga, Lipumba akiwa kimya' na yeye yuko kimya. Kwa hiyo amekuwa akicheza ngoma ya Lipumba!

2. Maalim Seif
Yeye namlaumu kwa kutochukua hatua mapema, Lipumba hakupaswa kupewa nafasi mapema, naye sasa amekuwa akijibu mapigo ya Lipumba tu badala ya Lipumba kujibu mapigo yake! Lipumba akiita Baraza lake, naye anaita lake, Lipumba akifukuza wabunge, naye anafukuza! Amechelewa sana!

NINI CUF YA MAALIM IFANYE?
Kwa sasa CUF ya Maalim imebanwa sana na Lipumba, na naona imebakiwa na option mbili tu!

1. Mahakama;
Mahakama pekee kwa sasa ndo imebaki kuweza kuamua kama CUF iwe ya Lipumba au ya Maalim. Na ikitokea mahakama ikaamua kuwa CUF iwe ya Lipumba, Maalim atabaki na option mbili tu, mosi kuungana na Lipumba au

2. Kuongeza nguvu CHADEMA.
Option ya mwisho kabisa kwa Seif ni kutangaza kuachana na siasa za CUF ya Lipumba na kuongeza nguvu upande wa CHADEMA. Faida kubwa kwa upande wa CHADEMA ikiwa hili litatokea, ni kupata wafuasi wengi Zanzibar bila chenga! Na hapo ndipo msemo usemao "Waliokuwa nyuma ya Lipumba waliruka mkojo wakakanyaga kinyesi" utatimia.

Sent using Jamii Forums mobile app
umenena vyema.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hio option namba 2 nimeipenda sana na ndilo linalotakiwa kutekelezwa na cuf maalim
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Back
Top Bottom