CUF wamtega Kikwete: "Asimamie mazungumzo ya muafaka"

CUF wamtega Kikwete: "Asimamie mazungumzo ya muafaka"

Ni nani aliyekuwa amejitoa ktk muafaka jamani? CCM au CUF? Mnawapa masifa yasiyowastahili hawa jamaa!! JK aaache mambo makubwa ya nchi aende akashughulikie muafaka ? Muafaka wa nini? Kwani kuna watu bado wako Shimoni au? JK komaa na mambo muhimu siasa za Wapemba na Waunguja Mkapa alizimaliza 2001 . Ni nani aliyechinja askari tena tokea 2001? Visima vina kinyesi kama 2001? Hata maalim sasa kanyoa madevu. Muafaka wa nini?

Heshima

mbele mkuu, huko serious au unatania maana naona kama unasema mpaka CUF waue polisi, CCM na CUF waanze kunya kwenye visima ndo CCM ifikirie muhafaka. this will be a great shame on JK ambaye nchi za Africa sasa wanamtegemea kutatua migogoro yao.

Mkuu lazima tukubali hata kama wewe ni mwanachana wa CCM kuwa hamko serious katika ili mnachotaka ni kupitisha muda ili ifie 2010 kwa uchaguzi mwingine muwaibie tena halafu muamze muhafaka mpya, huu ni usanii na ufisadi wa kisisasa.

JK kila alichowaaidi wananchi naona kinagoma kutimia, maisha bora kwa kila mtanzania imekuwa ni maisha bora kwa mafisadi tu, kutatua mgogoro wa Zanzibar naona kumeota mbawa, kama yuko serious na hili hii ni nafasi pekee ya kuwadhibitishia wananchi kuwa anaweza, sijui ajira 1,000,000 zimeshia wapi maana sasa hivi viwanda vingi vinafukuza wafanyakazi kila siku.
 
Nina wasi wasi na uwezo wa JK kwa maswala kama haya pamoja na kuwa mshika dola na kila kitu .Kabla ya kuanza kukata tamaa wacha nimpe muda nione atasemaje .Anaweza kukubalia mwaka 2009 siku chache kabla ya uchaguzi .CUF kaeni macho CCM wanaongea huku wanatafuta namna ya kuwashinda huko Zenji.

JK NI RAIS WANGU NA PIA NI MWANACCM MWENZANGU,LAKINI NADILIKI KUSEMA HUYU BWANA NI MSWAHILI.MSWAHILI KWA MAANA YA KABILA LA WATU WA PWANI NA KUWA MUONGO.HANA UWEZO WA KUWA STRAIGHT NA WALA HAIJUI HISTORIA YA NCHI YAKE NA YA WATU WA ZENJ.NA KAMA ANAIJUA BASI HAJUI NNAMNA YA KUITUMIA KTK KUTEKELEZA MAMBO YAKE..ANALOPOKA TU KUWA ATATATUA MGOGOLO WA ZENJ HUKU HUO UWEZO HANA.NDIO MAANA KARUME AMEACHA KUJA KUHUDHURIA VIKAO VYA BARAZA LA MAWAZIRI ZAIDI YA MWAKA.
 
JK NI RAIS WANGU NA PIA NI MWANACCM MWENZANGU,LAKINI NADILIKI KUSEMA HUYU BWANA NI MSWAHILI.MSWAHILI KWA MAANA YA KABILA LA WATU WA PWANI NA KUWA MUONGO.HANA UWEZO WA KUWA STRAIGHT NA WALA HAIJUI HISTORIA YA NCHI YAKE NA YA WATU WA ZENJ.NA KAMA ANAIJUA BASI HAJUI NNAMNA YA KUITUMIA KTK KUTEKELEZA MAMBO YAKE..ANALOPOKA TU KUWA ATATATUA MGOGOLO WA ZENJ HUKU HUO UWEZO HANA.NDIO MAANA KARUME AMEACHA KUJA KUHUDHURIA VIKAO VYA BARAZA LA MAWAZIRI ZAIDI YA MWAKA.

Heshima mkuu,

Hivi unapokuwa na mshauri wa siasa kama Prof. Mkandala ambaye ameshindwa hata kuongoza watoto 15,000 pale mlimani unategemea nini, utakuwa mbabaishaji tu, hakuna chochote cha kufanya maana kitakachofuatia CUF wakiandamana Mkadara atamshauri awapige mabomu ya machozi.
 
cuf wamejitega, na hawana lolote, si wakati wa kutishiana nyau huu
 
Mimi nafikiri hata huu mseto ni kupotezeana muda tu.


Pia kuna masuala mawili makuu ambayo kama yakizungumzwa basi kidogo patakuwa na maelewano.

1. Suala la kamati ya uchaguzi. Hii ni lazima iwe ni kamati pekee isiyo na nyizi zozote zinazoning'nia kutoka serikalini na CCM. Iwe na kamati yenye watu mbalimbali wanaoteuliwa na vyama vyote vya upinzani katika Tanzania na wanalipwa na fungu maalumu lililotengwa na vyama hivyo.

Kamati hii inakuwa hai pale kunapokuwa na uchaguzi tu, na baada ya uchaguzi inavunjwa.
Kamanda:
Kwa maneno mengine CCM isiwepo kwenye uchaguzi utakaosimamiwa na kamati hiyo ya uchaguzi? Ni uchaguzi gani ambao unaouzungumzia hapo? Na nini faida ya kuwa na kamati hiyo wakati tayali kuna Tume ya Uchaguzi?

Tafadhali naomba ufafanuzi hapo, kwani naona nipo gizani...
 
CUF tangia awali walianza kwa kubofya wrong button, kwani kitendo cha wao kukurupuka na kuanza kufanya maandamano kwenye ngome zao na kuona kuwa kwa sasa wamabakiza ngome moja tuu ya Pemba na kuanza kumtaka JK ni makosa makubwa ya kisiasa na haswa inapokuwa kuwa jambo lenyewe halina masilahi ya moja kwa moja kwa wananchi wa kawaida .

CUF angalieni upya watu ambao ni mastrategist wenu kwani huku ni kufa maji kama mngekuwa smart mlipaswa kwanza mfanye ground work na sio kuamua kuanzisha maandamano ambayo mwisho wake haujulikani na wala hauonekani .

Kuna kila sababu ya kuona hapa kuwa CUF wamekata tamaa na haswa baada ya maandamano ya Tanga juzi, na pia kitendo cha CUF kulifanya suala hili ni la kwao wao binafsi ndio kikubwa ambacho kinawaumiza zaidi kwani walipaswa kulifanaya hili ni jambo la kitaifa na sio la CUF vs CCM .

Shirikisheni vyama vingine ili kuhakikisha kuwa ajenda inabebwa na wananchi na sio viongozi.

Nashauri kuwa CUF rudini na kujipanga upya ,angalieni kesho sio political scores za siku moja.

kusema ukweli sio dhambi hata kama ukweli huo utaniumiza.
 
Kweli CUF kiboko mtu mzima kashikwa sehemu mbaya jamani. Lakini it's very strange JK na mbwembwe zake zote na rungu lake la U-president inakuwaje anapata kigugumizi kwenye hili jambo la Znz?? Huyo huyo tena yuko front kwenda kusuruhisha migogoro kwenye nchi nyingine nadhani hata ho waku wa AU waliompa huo uenyekiti they were completely wrong or they don't know what's happening in Tz?? It's crazy unakaza misuri ya shingi kwenda kuzima moto kwenye nyumba ya mwenzio wakati we kwako bado kunawaka...Kweli dunia ina watu...

Ok let's wait and see hapo napo atapiga chenga ya aina gani??? Akikaa vibaya tunamzomea tu kwani nini???
 
JK knows what is next but ni wao KAFU ndio wasioona ukweli huo, msekwa keshasema kama ni muafaka 2010 na si sasa ,lakini wao wamemng'ang'ania Shamhuna wakati anyefanana na Amani keshasema pengine 2010. Au watuambie kama Msekwa keshakanusha hili? Sisi CCM tunafahamu matatizo ya Unguja na Pemba kwa kina ambacho CUF wanadhania. JK si wa kulaumiwa hapa, Karume ni rais kwa ridhaa yao Wazenj na wao wanalitambua hilo ,kama wasingelitambua wasingeikubali serikali ya Mseto, Raila leo ameapishwa na Kibaki na Seif anataka aapishwe na Karume , Wale washikaji Kenya walikuwa makini lakini wamekubali matokeo ktk meza iliyo mbele ya watu makini, lakini hawa jamaa tangu awali hawakuwa wakweli, 1995-00 waliingia barabarani, misikitini,visimani na diplomasia akaja Anyaouku,what happened. 2000-05 wakarudi visimani na kuchinja polisi ,Benja akaona hapahapa pa kumkoma nyani Giladi mchana peupe ,mwenye sime twende ,risasi twende,mwenye ndevu akanyolewa na ghasia tele mpaka Shimoni Mombasa,ukaja muafaka wa LipuLipu na Benja -Hamad Rashid ndani ya Bunge tukufu na Tume shirikishi -2005 this time hawa jamaa wakapigwa mwereka wakasema wameibiwa tena lakini ushahidi haukutosha wakajifanya wanasubiri JK aseme, muungwana toka Chalinze asiyejua kumung'unya yalo rohoni akapasua kibuyu mbegu hadharani,wakatoka pale kicheko tele na wengine wakahamia Saluni kwa ajili kukarabati videvu vya japo viwiane na muungwana.

Sasa tupo 2008 muafaka aliuanza Mangula then Makamba ndio huu wao hawautaki na wamejitoa,tena wenyewe kwa hiari yao,JK wa nini tena ? Nani kakuondoa mezani / Ni wewe mwenyewe,waache kutusumbua na vijineno vyao,wacha nchi isonge mbele.Wao wamsubirie tu ila CCM iko imara ktk misingi yake.
 
Back
Top Bottom