CUF wanatumiaje ruzuku yao bara?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027


mambo ya kuzingatia:

a. Baada ya CCM, CUF ni chama cha pili kinachopokea ruzuku nyingi toka serikalini.

b. Pesa hizo ni nje ya wanazopata kupitia wafadhili, miradi yao mbalimbali (kama wanayo), uwekezaji benki (kama wanafanya) na michango ya wanachama (kama ipo)

c. ni nje ya fedha za mishara ya wabunge na wawakilishi wake

Nitaendelea kuwaletea taarifa za vyama vingine vikuu vinavyopokea ruzuku ya fedha za walipa kodi wa Tanzania kwa kadiri siku zinavyokwenda na kwa kadiri zinavyopatikana
 
Last edited by a moderator:
Ni vema pia ikawekwa na ya CCM na CHADEMA ili discussion iwe fair..tusijeelemea upande mmoja tu wa CUF!

CUF walipata 2.6 bln 2008 kuna mtu anajua CCM 2008 walipata kiasi gani??
 
Kwa sasa tunaangalia CUF tu kwani kupatwa kwao fedha hakutegemei chama kingine kinapata kiasi gani. Ikifika zamu ya CUF na wengine tutaangalia hivyo.
 
Kwa sasa tunaangalia CUF tu kwani kupatwa kwao fedha hakutegemei chama kingine kinapata kiasi gani. Ikifika zamu ya CUF na wengine tutaangalia hivyo.

yes ni muhimu kujua wamezitumia vipi hizo pesa kwani ukishindwa kutumia kidogo utawezaje kutumia kikubwa?
 
Je kiasi hicho kinatumika kwa kiasi gani huku bara katika kujiimarisha kisiasa?
 
Haa, yaani fedha zote hizo wanafanyia kitu gani ?mbona hawaonekani kuwa na mkakati maalumu ama programm ya chama?

CUF ni lazima wajitokeze na kueleza fedha hizo zaidi ya bilioni mbili walizopata kwa kipindi cha mwaka jana zinatumika kufanya kazi gani na wapi?

Kuna jambo la kujifunza hapa na yeyote anayeweza kuleta pia za CHADEMA na CCM afanye hivyo ili kujua hawa jamaa wa vyama wanapata kiasi gani na wanazifanyia nini hizo fedha wanazozipata.
 
Nadhani Mwiba atatuambia jinsi zinavyotumika Bara!

Naona nyingi zinatumika kuiangamiza CCM Pemba na kusaidia mikutano ya vile vijembe vya Seif kule Kibandamaiti!

Ni vema pia kujua ktk 2.6 billlions ni ngapi zilitumika bara na ngapi kule Visiwani!
 
Haya masuala ya ruzuku kusema ukweli yanatakiwa kuondolewa, ni upotevu wa fedha za walipa kodi bure. Hizo mnazoona za CUF, ikitolewa wanayopata CCM ni balaa. Manake ruzuku hutolewa kwa kufuata uwiano wa wabunge wa chama husika.

Vyama kwa kuwa vina wanachama, viachwe vijihudumie vyenyewe, TANU ama ASP (nisisahau na Hizbu, Mwiba akanibana) zilipata wapi fedha, ilikuwa ni kutoka kwa wanachama na wapenzi. Kwa nini sasa tupoteze fedha zote hizo kwa sababu ya vyama badala ya kusaidia miundo mbinu yetu. Na hili la ruzuku ndio kimekuwa kikwazo kwa vyama pinzani kushirikiana pale ambapo kuna kila dalili kuwa kama vitashirikiana vyaweza kuishinda CCM, kila chama kinataka kipate Wabunge wengi ili na ruzuku iwe kubwa. Wizi mtupu!.
 
Pamoja na kuwa CCM wanapata mara nyingi zaid ya CUF, lakini kama CUF wangekuwa na moyo wa maendeleo then hicho kidogo kingeonekana kinafanya nini, wajitolee waonyeshe mfano kwa kujenga shule moja wa wazazi wa CUF na kuindesha kwa gharama nafuu kwa ajiri ya wanachama wao, au wachangie ujenzi wa madarasa ya shule za serikali badala ya kuendelea kukamua wananchi
 
Kwa sasa tunaangalia CUF tu kwani kupatwa kwao fedha hakutegemei chama kingine kinapata kiasi gani. Ikifika zamu ya CUF na wengine tutaangalia hivyo.


Iliuweze ku-analys hii issue, weka Financial report ya vyama vyengine kama CCM, Chadema ndo to compare.
 

Kwanini Fedha za shughuli nyengine hatuulizi kiasi gani kinakwenda Zanzibar?

Kama Bara wanaumwa na fedha yao (fedha yote hii karibu 90% inatoka bara) wangeacha vile visiwa vijiamulie mambo yao. Nikifikiria na 7,000,000 za kila mwezi kwa Wabunge wa visiwani wasiopunguwa 60,135,000 kwa wajumbe hao kwa kuja na kusikiliza mipango ya kuiendeleza Tanganyika na kukaa kwenye kamati na kujadili mambo yasiyo wahusu ndio naona hasara ya huu unganganizi.
 

TANU na ASP walishikilia madaraka ya nchi na hakukuwa na tofauti kati ya serikali na Chama. Wakati huo wakijichotea watakavyo. Ama hayo ya HIZBU Mwiba ndiye atakaetusaidia.
 

Kwa hilo haliwezekani kule visiwani. Kuna wakati kulitokea maradhi kule Pemba na serikali ilikataa dawa zilizotolewa na CUF. Hata kada Mohamedi Raza alikwishakataliwa kutowa msaada Hospitali. Muulize KIbunango pengine alikwishahamia Unguja wakati huo.
 
TANU na ASP walishikilia madaraka ya nchi na hakukuwa na tofauti kati ya serikali na Chama. Wakati huo wakijichotea watakavyo. Ama hayo ya HIZBU Mwiba ndiye atakaetusaidia.

Mkuu Ngekewa nilikuwa nazungumzia wakati kabla ya Uhuru, hivi vyama vilipata fedha toka kwa wanachama wao. Ndio nikaandika sioni sababu sasa hivi vyama vya siasa kupewa fedha yote hiyo ya walipa kodi.
 
Ngekewa,

1. Kwa nini SMZ ikatae dawa zilizotolewa na CUF?

2. Hiyo ya Mbunge Bunge la Muungano toka Visiwani kulipwa 7,000,000 kwa mwezi si wanazungumzia kule mambo ya Muungano pia?

Sasa unasema Bara waache visiwa vile vijitawle vyenyewe sii watauna wenyewe kwa wenyewe kama wakati wa Mapinduzi??

Kumbuka Sambe wa Komoro ameonyesha nia na ombi la kujiunga na Bara!

Uko hapo??
 
Last edited:
Kwa kiasi ambacho CUF wanapokea inakuwaje hawana mbunge Tanzania bara? au kushindwa vibaya kama kule Mbeya au Tarime? Kwanini hata maeneo ya pwani ambapo naweza kusema ni ngome yao (Tanga, Dar, Pwani) hawana mbunge hata mmoja!
 
Kwa kiasi ambacho CUF wanapokea inakuwaje hawana mbunge Tanzania bara? au kushindwa vibaya kama kule Mbeya au Tarime? Kwanini hata maeneo ya pwani ambapo naweza kusema ni ngome yao (Tanga, Dar, Pwani) hawana mbunge hata mmoja!
Unaweza kuwa na mtaji mkubwa ukashindwa kuutumia.Maximo anakula mshahara mkubwa hawezi kuleta kombe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…