Currency swap kati ya Tanzania na China, India, Turkey kukabiliana na uhaba wa Dola

Currency swap kati ya Tanzania na China, India, Turkey kukabiliana na uhaba wa Dola

mwanamichakato

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2015
Posts
1,188
Reaction score
1,090
Kuna biashara kubwa sana (inayohusisha mabilioni ya fedha) baina ya nchi yetu na China, India, Uturuki, Afrika Kusini n.k.

Taifa letu bado ni tegemezi katika kuagiza vitu, vifaa, chakula, nguo na mengine toka katika nchi mbalimbali. Hili linafanya wafanyabiashara wanaoagiza kuhitaji na kutafuta fedha za kigeni haswa Dola ya Marekani kila leo. Bidhaa zinaagizwa kwa dola na kisha kuuzwa kwa fedha ya Tanzania (madafu) na hivyo kulazimu wafanyabiashara kununua dola kwa bei ya soko ili kuagiza bidhaa.

Tatizo linakuja kwenye mfumuko wa bei, uhaba wa dola. Bei ya kununua Dola ya Marekani kupanda kila leo hivyo kuleta usumbufu mkubwa sana kwa wafanyabiashara na mwisho walaji wa mwisho wa bidhaa. Hivi sasa kupata (kununua)dola 10000;20000;100,000;300,000;600,000;1000,000 n.k si jambo rahisi kupitia benki.

Kwa mujibu wa sheria za fedha kimataifa inawezekana kufanya currency SWAP baina ya nchi na nchi. Hili hufanyika kwa Benki kuu za nchi husika kukubaliana kila nchi kufanya manunuzi katika nchi ya mwenzie Kwa kutumia fedha yake.

Mathalani tunanunua nondo China, invoice inakuja katika Yuan na wafanyabiashara kufanya malipo kwa kutumia shilingi sawa na thamani ya Yuan, vivo hivyo Kwa rupees na zingine.

Hili litaondoa utegemezi wa Dola ya Marekani lakini mfumuko mkubwa wa bei unaotokana na fedha yetu kushuka thamani pia fluctuations.

Yawezekana IMF na World Bank wakawa Kikwazo katika kufanikisha hili lakini naamini watendaji na viongozi wetu wakiwa shupavu tunaweza.

Uimara wa biashara na wafanyabiashara ndio uti wa mgongo katika maendeleo ya nchi pamoja na ustawi.

Heri ya Miaka 60 ya Muungano kati ya TANGANYIKA na Zanzibar (Unguja na Pemba).
 
naamini watendaji na viongozi wetu wakiwa shupavu tunaweza.
Kwa mara ya kwanza,niipongeze CCM Kwa hili.
JamiiForums914827189.jpeg
 
Mkuu tunafanya trade kutokana na international trade law, usione tunafanya biashara na china ukajua tunaweza tu kukutana na china tukaongea tue tunalipina vipi mchezo ukaishia hapo, hapana, kuna sheria za kimataifa zinatubana sisi na hao wachina pia


Unadhani mchina nae anapenda ku trade kwa Dola? China ndo nchi inaongoza duniani kuuza bidhaa za viwandani, lakini malipo yote anapokea kwa USD, unadhani ye hapendi kuuza kwa yuan ili apromote currency yake? Marekani ilishaongozwa na watu wazalendo sana yani wameweka Mikataba karibu Dunia yote kuipendelea nchi Yao kuanzia miaka hio


Unachoshauri hakiwezekani, dollar bado ipo sana sio rahisi kuikwepa kiivyo
 
Mleta mada, moja ya sheria kwenye biashara yoyote ni muhimu kuwepo na standardization

Sarafu zingine tofauti na dola sio imara na zinabadilika kila wakati kutokana na sababu mbalimbali hasa mfumuko wa bei kwenye nchi husika

Mfano Uturuki, Safaru ya Uturuki kati ya 2016 na leo imeanguka kwa zaidi ya 20% maana yake kama tungewalipa kwa fedha yao wakati huo basi wangetufanyia kazi bure kwa puunguzo la 20%, kama tungesema tuwalipe kwa awamu basi thamani ya mradi ingeongezeka kwa zadi ya 20%.

So issue ya uhaba wa dola pia husababishwa na udhaifu wa sera za nchi husika, mfano sisi tunauza raw materials na unakuta wanasiasa tena wa upinzani waliotakiwa wawe na mawazo mbadala wanashabikia wakulima wakiuza mazao yao kwa madalali. Hili ni eneo ambalo lilitakiwa lituletee fedha za kigeni

Serikali yetu imekuwa too soft kwa maduka ya kubadilishia fedha
 
Mtoa mada changa akili vizuri tena, ata batter trade ilikuwa na utaratibu haikuwa ya kienyeji kama unavyotaka kutuaminisha.
 
Ila ungesema kwanini unayo akaunti ya Dollar benki ila ukienda kutoa hizo Dollar zako uzipati hapo ndo ningekuona wa maana iwapo ungetoa solution. Pia, unalipa Kodi pamoja na charges zingine kwa Dollar ila ukirudi tena benki kubadilisha Tsh kwenda Dollar unakutana na maajabu.
 
Ila ungesema kwanini unayo akaunti ya Dollar benki ila ukienda kutoa hizo Dollar zako uzipati hapo ndo ningekuona wa maana iwapo ungetoa solution. Pia, unalipa Kodi pamoja na charges zingine kwa Dollar ila ukirudi tena benki kubadilisha Tsh kwenda Dollar unakutana na maajabu.
Nimekuelewa ndugu
 
Back
Top Bottom