CVT gear box problem

CVT gear box problem

Wadau, sikupata solution ya kutengeneza gia box hyo, so Nilibidi kununua nyingine nkaweka and the problem was solved. It run properly by this time ingawa fundi alie nitia hasara hii nimemuweka lock-up kidogo akili ikamkae sawa.View attachment 626113
Safi kama ulimuweka ndani akulipe hela ya gear box mpya
 
Una uhakika Hiyo Tiida inatumia Matic J fluid..?
Kuna kitu hakijakaa sawa..
Hizo matic J ni za Nissan Xtrail ambayo inatumia automatic transmission ya kawaida..

Nissan tiida inatumia CVT na fluid yake ni CVT fluid NS 2...iko kwenye kopo la lita 4 inauzwa kati ya sh 120000 mpaka 140000 inategemea upo mkoa gani.

Kwa hizo fluid nasikitika kusema huenda umeshaua gear box.
Hapo nunua NS 2 dumu mbili, dumu la kwanza ufanyie flash na dumu na dumu la pili uweke....
Ikigoma tena utakuwa umeshaua gearbox

IM SORRY FOR THIS
Hii kitu huwa inauma sana. Unamwaga mchuzi wa laki na ishirini huku unauona hivi hivi.
 
Habari wadau gari yangu ni progress haimalizi gia nimeweka oil T -Iv lkn haimaliz ukikanyaga sana inajiweka Neutral mwenye uzoefu naomba msaada
 
Pole sana kwa fundi kukuingiza hasara sababu ya ujinga wake huyo fundi.

Mimi magari yangu napeleka kufanya service kwenye hizi filling stations na haswa PUMA, oil na vifaa vyote nanunua mwenyewe na wakati gari linafanyiwa service nasimamia.

Epuka kuwaamini mafundi. Nilishakutana na issues tofauti kwa kumuachia fundi gari atengeneze.

Mojawapo alifanya kazi ya kubadilisha break pads na bushings nikamuachia gari sababu nilikuwa busy na kazi, akanirudishia gari jioni. Asubuhi najiandaa kusafiri nalo nakagua nuts za kwenye matairi nakuta nut 1 haipo, nampigia anadai ilikuja hivyo hivyo wakati yeye ndiye alikuwa mtengenezahi wa ilo gari siku zote, baadae akasema hapo nut aifungi stadi yake imeharibika. Nikamwambia sio kweli, tukutane dukani tutafute, tukakutana akapata alafunga ikafunga.

Issue nyingine nikapeleka kwa fundi kufanya matengenezo ya gari kubadili break pads, bushings na vitu vingine, kesho nikasafiri km zaidi ya 1,000, uko ugenini kulikuwa na mlio kwenye mguu wa mbele, nikapeleka kwa fundi wakati wa kufungua Nats za matairi, nuts 3 za tairi la upande mmoja zilifungwa vibaya, ilibidi afungua kwa kulqzikisha ila zile stadi zikawa zimeharibika nikaingia gharama kwenda kununua stadi zingine 3 ambazo nj Genuine. Nikasema kama ningepata panchayat njiani ingekuwaje alafu inanipatia nikiwa porini.
 
Back
Top Bottom