Dada kanifananisha au anataka nimtafune. Ushauri tafadhali

Dada kanifananisha au anataka nimtafune. Ushauri tafadhali

Kuna siku ataibuka mwalimu original halafu utaonekana tapeli.

Ukwl humweka mtu huru ..
 
Wewe jamaa unanyota ya kuwa mwalimu .

Shida yetu buana, kichwa kidogo kishaanza kusumbua tayari.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kwa akili hizi hata tukihamishiwa marekani sasa hivi baada ya miezi miwili tutaomba msaada kwa nchi tajiri
Trump alishawahi kulisema hili. Kwamba tukibadilishana mabara Wamarekani waje Africa na sisi twende Marekani baada ya miaka mitano tu tutakuja Afrika kuwakopa wazungu..

Our priorities are wack!
 
Afu ukute Dada wa watu hana hili wala lile…we ushamuwazia kumtafuna!
 
Alikua/ulikua mwl mzuri ulizokizalisha kinauza duka la mangi .....pelekea moto huwezi jua mbleni ,weka alama
 
Wakuu! Heri ya Mwaka 2023. Mwenzenu mwaka Jana umeisha Kwa kufananishwa na dada mmoja mrembo ambaye anauza duka la bidhaa za jumla na rejareja jirani na ninapokaa.

Huyu dada siku nimekaa Kwa Hilo duka Kuna ka pub jirani take,na yeye ni mtu asiyetumia kilaji kabisa na amenyooka katika Imani, lakini alinifuata hapo pub mbele ya watu na kuniambia teacher habari za siku ,ilibidi nimuulize nilikufundisha shule gani, akanitajia secondary moja huko Moro twn,nikauliza Tena SoMo Gani akasema civics .

Ilibidi nimkubalie tu maana niliona nitamfedhehesha mbele za watu lakini kiukweli Mimi sijawahi kuwa mwalimu na sijawahi kufundisha popote.

Baada ya hapo amekuwa akifurahi sana akiniona na akijitapa kwa wenzie kuwa Mimi ni mwalimu mzuri sana,nilimfundisha vizuri na pia amekuwa akinipa vi OFA vya kulazimisha hata kama sitaki. Nifanyeje wakuu.
Hahaha
 
Back
Top Bottom