Dada yetu anaishi na Virusi vya UKIMWI, tumwambie ukweli mchumba wake?

Dada yetu anaishi na Virusi vya UKIMWI, tumwambie ukweli mchumba wake?

Kama unajali kweli kama unavyodai, usikubali haya yatokee.
Lakini sio wewe unayepaswa kumweleza huyo jamaa!
La kufanya ni uzungumze kwa marefu na mapana na huyo dada juu ya analotaka kulifanya.

Mweleze haki ya jamaa kujua hali yake ya kiafya na umwambie ni jukumu lake kama mate/partner wake kumwambia hayo.

Mwambie kama hatomwambia kuhusu hali yake ya afya, utamwambia wewe.
Sasa kama huyo dada ana akili timamu hatokubali mtu mwingine kumwelezea mchumbake hali yake ya afya. Atamwambia.

Hakikisha anamwambia kabla hawajaoana.
Sasa utakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe moja.
 
Nakumbuka maneno ya Alhaji Mwinyi (Mzee wa Ruksa) "Ndugu Watanzania huu ugonjwa umekaa pabaya, tena pabaya sana"
 
Habari zenu wana Jf,

Nina mdogo wangu wa kike baba mmoja ila mama ndio tofauti, mzee alikua na wake wawili.Huyu binti alikua akifanya biashara za kusafiri kwenda Kampala na nairobi kwa miaka mingi, ni mdogo wangu wa nne kuzaliwa, tupo Tisa kwa hao mama wawili, ila mama zetu hawapo duniani, mzee ndio bado yupo katika hizi safari za kibiashara bahati mbaya akapata ugonjwa huu wa kisasa, aliugua sana hapo katikati, nadhani ilikua 2006-2009.

Baadae akapona akainuka kabisa kutoka kitandani lakini akaambiwa asiache dawa za kurefusha maisha, tukamzuia kuendelea na hizo business za kusafiri, akaokoka na bado anaabudu hadi sasa, amenona hasa, amekua kipande cha mtu.Simzungumzi vibaya Dada yangu, ila kwa kweli amekua na wowowo lenye kumvutia mwanaume yeyote yule.

Nadhani ni katika muonekano huo ndipo akajitokeza mlokole mwenzie huko kanisani kwao kutaka kumuoa, huyo jamaa kachanganyikiwa na yuko resi mno, ameshaniletea barua nami nikaipokea pamoja na wenzangu, baadae tukamtajia mshenga wake mahari nayo akalipa na tulishaila, tuligawana makaka, nae binti tukampa kidogo.

Sisi hatujaanza utaratibu wa vikao ila wao upande wa jamaa walikaa vikao viwili tayari, wakati wote huu mimi nilidhani dada alishamweleza status yake huyu mchumba, na pengine nikadhani wote wana status hiyo hiyo ya HIV positive wameamua ku team up kuunda familia, kumbe sivyo huyu jamaa hajui chochote kuhusu hali ya huyu dada yangu.

Kuna dada yetu mkubwa aliempeleka kanisani huyu binti na wanasali pamoja, juzi alimuuliza muolewaji kama amemwambia mchumba hali yake, akajibu hajamwambia, anaogopa akimwambia atakosa ndoa, na yeye anahitaji kuwa na familia yake kama mwanamke, na kwamba yeye mwenyewe haachiwe jambo hilo atalimaliza mwenyewe, na kwamba tusimwambie mchumba chochote.

Roho yangu inanisuta sana kushiriki jambo hili, hasa ukichukulia kuwa nyumba na mji wangu ndio unaochukuliwa kama nyumbani kwao na bibi harusi, na tupo karibu sana kimawasiliano na huyo jamaa.Mfano ni juzi tu kanitumia laki mbili akisema ni ya chai.

Pia ni msomi mwenye carrier yake na future inayoeleweka, hivyo nafsi inanisuta, wenzangu wanadai afya za maharusi sio kazi yetu, kwamba sie kazi yetu ni kusherekea tu, kwamba ni miaka sasa hatujawa na harusi tunachangia watu tu

Wadau, nahitaji msaada wa mawazo

Au na mimi nipotezee tu watajuana wenyewe?




Fanya kama kutoa nasaha tuu ya ki utu uzima@wasisisitize wasisahau kwenda ku chek afya Zao@kupitia apo nazan utapata defenc mechanism hata yakija kubumbuluka badaye
 
Kisheria hakuna ndoa inayofungwa bila vipimo vya daktari so itajulikana na km wataamua kuoana pia inawezekana.
kwa kweli mkuu wakapime kabla ya ndoa, ila wasiwasi ni kama ameanza tendo la ndoa kabla ya ndoa-hapo uaminifu wake kwenye ulokole wake utakuwa umepungua na atajutia.hatuwezi kusema ni wa kawaida, LAZIMA UKWELI USEMWE
 
hivomnaoana tuu kienyeji kisa niniau eti ni walokole ndio mnaaminiana....kulaleki hakuna utaratibu wa kuoana kienyeji kansanixo huyo jamaa naye ntamshangaa akitakaresi na huyo dada naye muuaji tu hana utu
 
Siku hizi si hauozeshwi mpaka uwe na cheti cha kupimwa HIV?

Uungwana ni kuambiana ukweli.

Huyo dada'ko kama anamficha huyo mchumba bado hajaokoka kama unavyodai, anajidanganya tu.

Pengine na mchezo kisha mpa. Si mnasema siku hizi hamuoani mpaka mlane kwanza!

Kuokoka kiukweli ni kujisalimisha kwa Mwenyeezi Mungu aka Kusilimu, vinginevyo ni uongo tu.
 
Nadhani hela mlizokula ni chache kuliko mtakazopewa baada ya kumwambia mtu ukweli na kuokoa ndoto zake kufutika!Hofu yangu ni kama kweli bado hajapewa mzigo kavukavu maana hapo sioni element za ulokole kabisaa, ni full matamanio!Ukishindwa kumwambia nitumie namba za jamaa PM na jina la dada yako nikusaidie kuwaweka sawa
 
Nadhani hela mlizokula ni chache kuliko mtakazopewa baada ya kumwambia mtu ukweli na kuokoa ndoto zake kufutika!Hofu yangu ni kama kweli bado hajapewa mzigo kavukavu maana hapo sioni element za ulokole kabisaa, ni full matamanio!Ukishindwa kumwambia nitumie namba za jamaa PM na jina la dada yako nikusaidie kuwaweka sawa
Safi sana!Wewe unastahili dhima ya hata kupewa udiwani aisee
 
Habari zenu wana Jf,

Nina mdogo wangu wa kike baba mmoja ila mama ndio tofauti, mzee alikua na wake wawili.Huyu binti alikua akifanya biashara za kusafiri kwenda Kampala na nairobi kwa miaka mingi, ni mdogo wangu wa nne kuzaliwa, tupo Tisa kwa hao mama wawili, ila mama zetu hawapo duniani, mzee ndio bado yupo katika hizi safari za kibiashara bahati mbaya akapata ugonjwa huu wa kisasa, aliugua sana hapo katikati, nadhani ilikua 2006-2009.

Baadae akapona akainuka kabisa kutoka kitandani lakini akaambiwa asiache dawa za kurefusha maisha, tukamzuia kuendelea na hizo business za kusafiri, akaokoka na bado anaabudu hadi sasa, amenona hasa, amekua kipande cha mtu.Simzungumzi vibaya Dada yangu, ila kwa kweli amekua na wowowo lenye kumvutia mwanaume yeyote yule.

Nadhani ni katika muonekano huo ndipo akajitokeza mlokole mwenzie huko kanisani kwao kutaka kumuoa, huyo jamaa kachanganyikiwa na yuko resi mno, ameshaniletea barua nami nikaipokea pamoja na wenzangu, baadae tukamtajia mshenga wake mahari nayo akalipa na tulishaila, tuligawana makaka, nae binti tukampa kidogo.

Sisi hatujaanza utaratibu wa vikao ila wao upande wa jamaa walikaa vikao viwili tayari, wakati wote huu mimi nilidhani dada alishamweleza status yake huyu mchumba, na pengine nikadhani wote wana status hiyo hiyo ya HIV positive wameamua ku team up kuunda familia, kumbe sivyo huyu jamaa hajui chochote kuhusu hali ya huyu dada yangu.

Kuna dada yetu mkubwa aliempeleka kanisani huyu binti na wanasali pamoja, juzi alimuuliza muolewaji kama amemwambia mchumba hali yake, akajibu hajamwambia, anaogopa akimwambia atakosa ndoa, na yeye anahitaji kuwa na familia yake kama mwanamke, na kwamba yeye mwenyewe haachiwe jambo hilo atalimaliza mwenyewe, na kwamba tusimwambie mchumba chochote.

Roho yangu inanisuta sana kushiriki jambo hili, hasa ukichukulia kuwa nyumba na mji wangu ndio unaochukuliwa kama nyumbani kwao na bibi harusi, na tupo karibu sana kimawasiliano na huyo jamaa.Mfano ni juzi tu kanitumia laki mbili akisema ni ya chai.

Pia ni msomi mwenye carrier yake na future inayoeleweka, hivyo nafsi inanisuta, wenzangu wanadai afya za maharusi sio kazi yetu, kwamba sie kazi yetu ni kusherekea tu, kwamba ni miaka sasa hatujawa na harusi tunachangia watu tu

Wadau, nahitaji msaada wa mawazo

Au na mimi nipotezee tu watajuana wenyewe?

Mwambie kijana wa watu, na dada yako oia kuwa anachofanya ni dhambi na mshahara wake ni mauti.
 
ushauri wangu ni kua tatizo la dada yako ni lake na ni maisha yake na huyo mchumba wake. si jukumu lako wewe kuingilia mambo yasiyokuhusu. Jali maisha yako na waache waendelee. Jiweke kwenye nafasi ya dada yako, halafu dada yako angeenda kusema kwa mchumba wako status yako, how would you feel.... Kama ni lazima usaidie, jitahidi kumuongoza dada yako a built ujasiri wa kumwambia mchumba wake yeye mwenyewe na sio wewe ndio uwe msemaji. Ukimwi sio ugojwa kama cancer na diabetes bali ni mfumo kubadilika mwilini. wewe mwenye kiherehere unaweza ukaondoka duniani kwa jambo dogo sana ukawaacha wakaendelea kuishi miaka mingini 20 na watoto wenye afya tele. achana na hii kitu, its too personal. nyinyi kama familia endeleeni na maandalizi ya harusi wala msizungumzie hili jambo maana si lenu bali ni la dada yenu, atajua mwenyewe jinsi ya kulitatua kwa mchumba wake. kwanini uumie moyoni kwa jambo ambalo si lako. binadamu tuna mambo ya ajabu sana. Kabla hawajaamua kuoana ilikua ni jukumu lao wenyewe kuamua kwenda kucheki afya zao maana mwisho wa siku ni kwa maisha mazuri, sasa kama hawakufikiria hilo wewe nini wa kutaka kuropoka. incase unamwambia halafu asikuamini akakuona unamfanyia roho mbaya hasa kwa kuhisi unaharibu kwa vile ni ndugu wa kambo, utajisikiaje? kama si aibu iliyokithiri. waache na maisha yao, na wewe endelea na ya kwako.
 
hapo kazi bure vijana wengi hawawez kutangaza ndoa km hawaja onjana.ila unatakiwa umwambie hata kw indirect way hivi
 
Back
Top Bottom