Dada yetu anaishi na Virusi vya UKIMWI, tumwambie ukweli mchumba wake?

Dada yetu anaishi na Virusi vya UKIMWI, tumwambie ukweli mchumba wake?

Fanya maamuzi magumu,umuokoe huyo jamaa hata km dada yako atakuchukia lkn elewa kuwa mbele ya Mungu upo sahihi.
 
Tena usipoteze muda jamaa yangu,kamwambie leo hii. Kama unaogopa mwambie mtu mwingine mpigieni hata simu kwa kutumia simu ya mtu mwingine. Jiulize je ingekuwa ni wewe? Usipomwambia utakuwa umeshiriki moja kwa moja kuchinja mtu. Tena wewe ndio zambi yako itakuwa juu ya wengine wote,ksbb una uelewa tofauti na hao. Ukimwambia thawabu yako ipo
 
Habari zenu wana Jf,

Nina mdogo wangu wa kike baba mmoja ila mama ndio tofauti, mzee alikua na wake wawili. Huyu binti alikuwa akifanya biashara za kusafiri kwenda Kampala na Nairobi kwa miaka mingi, ni mdogo wangu wa nne kuzaliwa, tupo tisa kwa hao mama wawili, ila mama zetu hawapo duniani, mzee ndio bado yupo katika hizi safari za kibiashara bahati mbaya akapata ugonjwa huu wa kisasa, aliugua sana hapo katikati, nadhani ilikua 2006-2009.

Baadae akapona akainuka kabisa kutoka kitandani lakini akaambiwa asiache dawa za kurefusha maisha, tukamzuia kuendelea na hizo business za kusafiri, akaokoka na bado anaabudu hadi sasa, amenona hasa, amekuwa kipande cha mtu. Simzungumzi vibaya Dada yangu, ila kwa kweli amekuwa na wowowo lenye kumvutia mwanaume yeyote yule.

Nadhani ni katika muonekano huo ndipo akajitokeza mlokole mwenzie huko kanisani kwao kutaka kumuoa, huyo jamaa kachanganyikiwa na yuko resi mno, ameshaniletea barua nami nikaipokea pamoja na wenzangu, baadae tukamtajia mshenga wake mahari nayo akalipa na tulishaila, tuligawana makaka, nae binti tukampa kidogo.

Sisi hatujaanza utaratibu wa vikao ila wao upande wa jamaa walikaa vikao viwili tayari, wakati wote huu mimi nilidhani dada alishamweleza status yake huyu mchumba, na pengine nikadhani wote wana status hiyo hiyo ya HIV positive wameamua ku team up kuunda familia, kumbe sivyo huyu jamaa hajui chochote kuhusu hali ya huyu dada yangu.

Kuna dada yetu mkubwa aliyempeleka kanisani huyu binti na wanasali pamoja, juzi alimuuliza muolewaji kama amemwambia mchumba hali yake, akajibu hajamwambia, anaogopa akimwambia atakosa ndoa, na yeye anahitaji kuwa na familia yake kama mwanamke, na kwamba yeye mwenyewe aachiwe jambo hilo atalimaliza mwenyewe, na kwamba tusimwambie mchumba chochote.

Roho yangu inanisuta sana kushiriki jambo hili, hasa ukichukulia kuwa nyumba na mji wangu ndio unaochukuliwa kama nyumbani kwao na bibi harusi, na tupo karibu sana kimawasiliano na huyo jamaa. Mfano ni juzi tu kanitumia laki mbili akisema ni ya chai.

Pia ni msomi mwenye carrier yake na future inayoeleweka, hivyo nafsi inanisuta, wenzangu wanadai afya za maharusi sio kazi yetu, kwamba sie kazi yetu ni kusherekea tu, kwamba ni miaka sasa hatujawa na harusi tunachangia watu tu.

Wadau, nahitaji msaada wa mawazo

Au na mimi nipotezee tu watajuana wenyewe?
Mmmh
 
Tena usipoteze muda jamaa yangu,kamwambie leo hii. Kama unaogopa mwambie mtu mwingine mpigieni hata simu kwa kutumia simu ya mtu mwingine. Jiulize je ingekuwa ni wewe? Usipomwambia utakuwa umeshiriki moja kwa moja kuchinja mtu. Tena wewe ndio zambi yako itakuwa juu ya wengine wote,ksbb una uelewa tofauti na hao. Ukimwambia thawabu yako ipo
 
Usishiriki kwenye hiyo murder case, lazima mhusika aambiwe hiyo issue au jifanye kuwa lazima vipimo vipatikane ndo muibariki hiyo ndoa. Hapo dadaaa hatakuwa na ujanja. Lakini sishauri nyote mkae kimya imagine wewe ndo unafanyiwa hiyo kitu

Ikija chai nyengine ikatae maana mnazidi kumpa matumaini kijana wa watu.
 
Ukisema ni vizuri ila huyo dada hamtaelewana tena.

Halafu huyo muoaji kama yuko huku atakuwa ameshajijua
 
Ni rahisi sana cha kufanya. Wewe muulize muoaji katika maongezi je mmepima? Mwambie Ni vizuri sana mchukue hatua ya kwanza mkapime pamoja. Kama umeshindwa kwa huyo mwambie hata Mchungaji wake atakaewafungisha ndoa. Muombe awashinikize kwamza wakapime pamoja kabla ya chochote.

Hapo utakuwa umefanya kwa nafasi yako. Vinginevyo usipotanya hivyo hivyo itakutesa hiyoaisha yako yote. Wewe tulia waza chukua nafasi ya huyo kijana. Piga picha hiyo.
Japo huyo muoaji nae mzembe kweli utajitwishaje kiholela hivyo bila kupima kwanza?
 
Nadhani ni katika muonekano huo ndipo akajitokeza mlokole mwenzie huko kanisani kwao kutaka kumuoa, huyo jamaa kachanganyikiwa na yuko resi mno, ameshaniletea barua nami nikaipokea pamoja na wenzangu, baadae tukamtajia mshenga wake mahari nayo akalipa na tulishaila, tuligawana makaka, nae binti tukampa kidogo.
Fikisha taarifa kwa mchungaji wao, iwe ni taarifa ya siri, na mchungaji atambue niaa njema uliyonayo, ili kwa utaratibu sahihi taarifa imfikie shemeji yako matarajiwa kwa njia nzuri na isiyo na emotional damge.

Makanisani wana utaratibu wa kuhakikisha afya za wanandoa, watajua njia sahihi ya kuzungumza nao kwa kabla ya ndo yao. Hapo utakuwa umemsaidia shemeji yako na dada yako.
 
=
Thread ni ya 2015. Mleta mada kama bado yuko hapa JF, alete mrejesho kulindaje.
 
Mnaingilia business za watu wazima zisizowahusu, waacheni wamalizane wenyewe na 99% chance jamaa kishakula kavu, na ukimwi sio murder watu wanaishi maisha ya kawaida mpaka wanazeeka, kama ni lazima sana ongea na dada yako lakini sio jamaa
 
Habari zenu wana Jf,

Nina mdogo wangu wa kike baba mmoja ila mama ndio tofauti, mzee alikua na wake wawili. Huyu binti alikuwa akifanya biashara za kusafiri kwenda Kampala na Nairobi kwa miaka mingi, ni mdogo wangu wa nne kuzaliwa, tupo tisa kwa hao mama wawili, ila mama zetu hawapo duniani, mzee ndio bado yupo katika hizi safari za kibiashara bahati mbaya akapata ugonjwa huu wa kisasa, aliugua sana hapo katikati, nadhani ilikua 2006-2009.

Baadae akapona akainuka kabisa kutoka kitandani lakini akaambiwa asiache dawa za kurefusha maisha, tukamzuia kuendelea na hizo business za kusafiri, akaokoka na bado anaabudu hadi sasa, amenona hasa, amekuwa kipande cha mtu. Simzungumzi vibaya Dada yangu, ila kwa kweli amekuwa na wowowo lenye kumvutia mwanaume yeyote yule.

Nadhani ni katika muonekano huo ndipo akajitokeza mlokole mwenzie huko kanisani kwao kutaka kumuoa, huyo jamaa kachanganyikiwa na yuko resi mno, ameshaniletea barua nami nikaipokea pamoja na wenzangu, baadae tukamtajia mshenga wake mahari nayo akalipa na tulishaila, tuligawana makaka, nae binti tukampa kidogo.

Sisi hatujaanza utaratibu wa vikao ila wao upande wa jamaa walikaa vikao viwili tayari, wakati wote huu mimi nilidhani dada alishamweleza status yake huyu mchumba, na pengine nikadhani wote wana status hiyo hiyo ya HIV positive wameamua ku team up kuunda familia, kumbe sivyo huyu jamaa hajui chochote kuhusu hali ya huyu dada yangu.

Kuna dada yetu mkubwa aliyempeleka kanisani huyu binti na wanasali pamoja, juzi alimuuliza muolewaji kama amemwambia mchumba hali yake, akajibu hajamwambia, anaogopa akimwambia atakosa ndoa, na yeye anahitaji kuwa na familia yake kama mwanamke, na kwamba yeye mwenyewe aachiwe jambo hilo atalimaliza mwenyewe, na kwamba tusimwambie mchumba chochote.

Roho yangu inanisuta sana kushiriki jambo hili, hasa ukichukulia kuwa nyumba na mji wangu ndio unaochukuliwa kama nyumbani kwao na bibi harusi, na tupo karibu sana kimawasiliano na huyo jamaa. Mfano ni juzi tu kanitumia laki mbili akisema ni ya chai.

Pia ni msomi mwenye carrier yake na future inayoeleweka, hivyo nafsi inanisuta, wenzangu wanadai afya za maharusi sio kazi yetu, kwamba sie kazi yetu ni kusherekea tu, kwamba ni miaka sasa hatujawa na harusi tunachangia watu tu.

Wadau, nahitaji msaada wa mawazo

Au na mimi nipotezee tu watajuana wenyewe?
Hayo maswala ya magonjwa na mahusiano ni very private, na kitaalam mtu anayetumia dawa vizuri hawezi kuambukiza inategemea na viral load, mtu mwenye virusi ana haki na uwezo wa kuingia kwenye mahusiano kama mtu mwingine, na akazaa mtoto negative na asimuambukize mtu mwenza
 
Mm dada yangu anakula Dozi na.kunajamaa kamuoa hivyohivyo ilibidi niulize jamaa anajua status ya sister wanasema anajua eeehhh kumbe kinawamba wanajilipua tu!! Jamaa aambeie ukweli harafu aamue mwenyewe
 
Habari zenu wana Jf,

Nina mdogo wangu wa kike baba mmoja ila mama ndio tofauti, mzee alikua na wake wawili. Huyu binti alikuwa akifanya biashara za kusafiri kwenda Kampala na Nairobi kwa miaka mingi, ni mdogo wangu wa nne kuzaliwa, tupo tisa kwa hao mama wawili, ila mama zetu hawapo duniani, mzee ndio bado yupo katika hizi safari za kibiashara bahati mbaya akapata ugonjwa huu wa kisasa, aliugua sana hapo katikati, nadhani ilikua 2006-2009.

Baadae akapona akainuka kabisa kutoka kitandani lakini akaambiwa asiache dawa za kurefusha maisha, tukamzuia kuendelea na hizo business za kusafiri, akaokoka na bado anaabudu hadi sasa, amenona hasa, amekuwa kipande cha mtu. Simzungumzi vibaya Dada yangu, ila kwa kweli amekuwa na wowowo lenye kumvutia mwanaume yeyote yule.

Nadhani ni katika muonekano huo ndipo akajitokeza mlokole mwenzie huko kanisani kwao kutaka kumuoa, huyo jamaa kachanganyikiwa na yuko resi mno, ameshaniletea barua nami nikaipokea pamoja na wenzangu, baadae tukamtajia mshenga wake mahari nayo akalipa na tulishaila, tuligawana makaka, nae binti tukampa kidogo.

Sisi hatujaanza utaratibu wa vikao ila wao upande wa jamaa walikaa vikao viwili tayari, wakati wote huu mimi nilidhani dada alishamweleza status yake huyu mchumba, na pengine nikadhani wote wana status hiyo hiyo ya HIV positive wameamua ku team up kuunda familia, kumbe sivyo huyu jamaa hajui chochote kuhusu hali ya huyu dada yangu.

Kuna dada yetu mkubwa aliyempeleka kanisani huyu binti na wanasali pamoja, juzi alimuuliza muolewaji kama amemwambia mchumba hali yake, akajibu hajamwambia, anaogopa akimwambia atakosa ndoa, na yeye anahitaji kuwa na familia yake kama mwanamke, na kwamba yeye mwenyewe aachiwe jambo hilo atalimaliza mwenyewe, na kwamba tusimwambie mchumba chochote.

Roho yangu inanisuta sana kushiriki jambo hili, hasa ukichukulia kuwa nyumba na mji wangu ndio unaochukuliwa kama nyumbani kwao na bibi harusi, na tupo karibu sana kimawasiliano na huyo jamaa. Mfano ni juzi tu kanitumia laki mbili akisema ni ya chai.

Pia ni msomi mwenye carrier yake na future inayoeleweka, hivyo nafsi inanisuta, wenzangu wanadai afya za maharusi sio kazi yetu, kwamba sie kazi yetu ni kusherekea tu, kwamba ni miaka sasa hatujawa na harusi tunachangia watu tu.

Wadau, nahitaji msaada wa mawazo

Au na mimi nipotezee tu watajuana wenyewe?
Leo ni 2024 tupe mrejesho
 
Back
Top Bottom