Dada zetu Mna Mambo!

Dada zetu Mna Mambo!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Msema kweli hakika, huyo mpenzi wa Mungu,
Kalamu nimeishika, nilisemalo ni langu
Beti ninaziandika, mzisome dadazangu,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo.

Dada zetu mwatutega, twategwa tukategeka,
Mikogo mnayomwaga, twajikwaa twaanguka,
Na nyuma mkigeuka, toba! Tunanusurika,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo.

Mkilegeza sauti, wagumu wanayeyuka,
Mtu mzima na suti, kiwewe kinamshika,
Chini akija kuketi, miguu yatetemeka,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo.

Hasa mnaponong’ona, mwatupandisha presha,
Tunabakia kuguna, na milio ya kutisha,
Na tukiwa tumenuna, wadada mwatuchekesha,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Nguo zinavyowabana, mwatusukuma dhambini,
Twamuomba Maulana, tutoke majaribuni,
Wa dada mna hiana, mwajua mwafanya nini,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Mara mnatukonyeza, mwapiga jicho kwa vile,
Twabaki twajiuliza, ana nini dada yule,
Tukija twajibamiza, twalishwa chenga za Pele,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Mwajua kutuchombeza, kama samaki na chambo,
Magoma tukiyacheza, kama ndege na ulimbo,
Wenzenu mwatumaliza, mkitingisha majambo,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Mwajua kututuliza, mwauma na kupuliza,
Tena mnatuliwaza, twalala twapitiliza,
Kweli mnatushangaza, twabaki twajiuliza
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Mengi tunawakosea, machozi tunawaliza,
Matusi twawatolea, na maneno ya kubeza,
Mengi tunawatendea, twatenda bila kuwaza,
Dada zetu mna mambo mambo yenye vijimambo!!

Mwisho mnakimbilia, kwa mwingine kutulia,
Mapenzi kutafutia, vidumu mwajipatia,
Mioyo ikitulia, kimoja mnazamia,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Wengine mwavumilia, na miaka inapita,
Watoto kutukuzia, kumbe mioyo yajuta,
Na siku ikifikia, na ninyi mbele mwapeta,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Ukweli nawaambia, bila nyinyi tumekwisha!
Tunakaa twajutia, na mawazo tunakesha,
Ulabu twafakamia, machungu kuyaondosha,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Dada zetu twawapenda, Bila ninyi tunakonda,
Kila siku zikienda, twajuta tunayotenda,
Msiache kutupenda, twapenda mnavyopenda,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Vidole vinaniuma, kalamu naiachia,
Nililotaka kusema, hilo nimewaambia,
Hivyo kutama natama, miye nawabarikia,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
 
Msema kweli hakika, huyo mpenzi wa Mungu,
Kalamu nimeishika, nilisemalo ni langu
Beti ninaziandika, mzisome dadazangu,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo.

Dada zetu mwatutega, twategwa tukategeka,
Mikogo mnayomwaga, twajikwaa twaanguka,
Na nyuma mkigeuka, toba! Tunanusurika,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo.

Mkilegeza sauti, wagumu wanayeyuka,
Mtu mzima na suti, kiwewe kinamshika,
Chini akija kuketi, miguu yatetemeka,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo.

Hasa mnaponong'ona, mwatupandisha presha,
Tunabakia kuguna, na milio ya kutisha,

Na tukiwa tumenuna, wadada mwatuchekesha,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Nguo zinavyowabana, mwatusukuma dhambini,

Twamuomba Maulana, tutoke majaribuni,
Wa dada mna hiana, mwajua mwafanya nini,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Mara mnatukonyeza, mwapiga jicho kwa vile,
Twabaki twajiuliza, ana nini dada yule,
Tukija twajibamiza, twalishwa chenga za Pele,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Mwajua kutuchombeza, kama samaki na chambo,
Magoma tukiyacheza, kama ndege na ulimbo,
Wenzenu mwatumaliza, mkitingisha majambo,

Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Mwajua kututuliza, mwauma na kupuliza,
Tena mnatuliwaza, twalala twapitiliza,

Kweli mnatushangaza, twabaki twajiuliza
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Mengi tunawakosea, machozi tunawaliza,
Matusi twawatolea, na maneno ya kubeza,
Mengi tunawatendea, twatenda bila kuwaza,
Dada zetu mna mambo mambo yenye vijimambo!!

Mwisho mnakimbilia, kwa mwingine kutulia,
Mapenzi kutafutia, vidumu mwajipatia,
Mioyo ikitulia, kimoja mnazamia,

Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Wengine mwavumilia, na miaka inapita,
Watoto kutukuzia, kumbe mioyo yajuta,
Na siku ikifikia, na ninyi mbele mwapeta,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Ukweli nawaambia, bila nyinyi tumekwisha!
Tunakaa twajutia, na mawazo tunakesha,
Ulabu twafakamia, machungu kuyaondosha,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Dada zetu twawapenda, Bila ninyi tunakonda,
Kila siku zikienda, twajuta tunayotenda,
Msiache kutupenda, twapenda mnavyopenda,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Vidole vinaniuma, kalamu naiachia,
Nililotaka kusema, hilo nimewaambia,
Hivyo kutama natama, miye nawabarikia,
Dada zetu mna mambo, mambo yenye vijimambo!

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Mwanakijiji una mambo yenye vijimambo
 
Yani mwanakijiji hakika ww ni multipurpose, huwa nashndwa hata kukutengenezea taswira how do u look? Hebu tupia picha yako basi mkuu.
 
ni kweli uloyasema,wala hujadanganya kitu,wafanya waume kuhema,kama miti kwenye misitu,wanajua kutetemesha,wakuache hauna kitu,kweli wadada wana mambo,makubwa kuliko mfano
 
hapo kwenye nguo za kubana tu hapo. Siku hizi unaona Mdada anatembea utafikiri yupo uchi lakini kapakwa Rangi nyeusi. kumbe kapiga mavazi meusi ya kubana
 
Back
Top Bottom