Dah! Afande Mwita Kaniokoa kwa Waifu

Dah! Afande Mwita Kaniokoa kwa Waifu

Hahahahaha lol! Chezeya akili ya kiumeni weye! Njemba mmoja Boss mkubwa sana kwenye taasisi moja ya umma ilibidi alazwe Muhimbili kupitia ndugu yake ambaye alikuwa kingunge pale prof nanihii 🙂🙂

Njemba ilikwaa STD mkoani na ilikuwa mkoani kwa mwezi mzima, siku inaondoka mkoani kurudi Dar ikagundua imekwaa gonjwa. Njemba ikajua tu wife lazima atachangamkia dushe baada ya kulikosa kwa mwezi mzima na kugegeda kutamuambukiza mama ngina gonjwa.

Hivyo njemba ikalazwa Muhimbili kwa kisingizio kwamba baada ya kuwasili Airport ikaanza kusikia kihindi hindi cha nguvu hivyo imelazwa ili kuchekiwa vizuri ni kitu gani hasa kimesababisha hali ile kumbe inatibiwa STD!

Jana nimepiga vyombo balaa. Pembeni nilikuwa na kinikia la UDSM. Linasoma Masters pale COET na limepanga mtaa wa pili jirani na nyumba yangu. Siku moja nililichanganya nikalinunulia panti kwa Mama Tarimo Boutique, lakini mama Tarimo akaja kuleta soo kwa kumuuliza Bi. Mkubwa kama chupi zilimtosha. Na mimi nilivyo mwendawazimu Bibi Mkubwa alipokuja kwa hasira kuniuliza kulikoni nilipopeleka chupi, wala sikumchelewesha kujifanya nimezisahau kwenye gari. Mama Junior alitafuta chupi hadi kwenye chesisi!!!! Alipozikosa akajua waosha gari watakuwa walizitua.

Sasa leo saa 12 asbh nimeamka. Mikono ya Amina iko kifuani mwangu. Ebwanae, pamoja na ukora wangu sijawahi lala nje ya kitanda changu. Najua Bi. Mkubwa atakuwa amepiga simu hadi kwa wakwe zake.

Uzuri nikamkumbuka Afande Mwita. Huyu OCD nimetoka naye mbali sana. Nilijua hatoniangusha. Nikampa mkanda mzima. Mwita akanitia ndani. Akampigia simu Bi Mkubwa aje Polisi kunichukua. Ati kanikuta kituoni nimetiwa ndani, baada ya msako uliofanywa Bar jana usiku. Yaani Agness na maneno yote yalimwisha. Akawa ananionea huruma tu. Ati hawa Polisi kwanini wawabebe bar nzima hata wikiendi wakati watu mpo kwenye starehe zenu. Hawajui wewe ni TISS?

Basi mimi nikiwa mpole kabisa nikamshika mkono Bi. Mkubwa. Shhhh. Hayo mambo ya TISS ni yangu na wewe. Hizo ni ajali za kawaida za kwenye masanga.
 
Back
Top Bottom