Dah! hawa COET-UDSM, wamezidi sasa

Hyo mbona wachache sisi tulianza 90 tumebaki 20 DIT hyo
 

Dah unanikumbusha machungu ila na mimi nilitoboa.
 

ninasoma hapa department flani aisee hawa jamaa ni complicatorrs balaa
 
Yani! Alafu kuna tangazo la kazi walikuwa wanataka engineer wa Civil na wakaandika eti mshahara laki tano. Yani niliyaona hayo ni matusi balaa!
 
Duuh
 
Kuna maisha Bora hata kabla ya hiyo PhD!
Achaneni nayo,masters mliyonayo mbona inawafaa
 
watoto wa siku hizi starehe nyingi.Mi niko hapa tangu FOE hadi leo, naona tofauti kubwa sana iliyopo kati ya wanafunzi wa FOE na COET.Siku hizi yaani wanafunzi wanakula raha kama mangwini.
Wanakulaje raha wakati hata bumu hawana, au wanapewa kiduchu.

Enzi za FoE ilikuwa ada yote unalipiwa, unakaa hosteli za chuo (darasani unaenda kwa miguu tu, masuala ya nauli, kodi, tozo za serikali za mitaa, kuchangia LUKU na kukabwa njiani au kutobolewa dirisha hayakuwepo), unapewa pesa yote ya matumizi (aka bumu) hakuna cha asilimia wala means testing, unapewa faculty requirements kama vile calculator, drawing board, overall na mabuti ya karakana, na mashati ya bluu ya kiafisa bure na serikali.

Madogo wa siku hizi wanasoma kwa shida aisee. Wazazi wao ndo tulikifaidi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 
Udsm na vyuo vingine vinapaswa kubadili mitaala na kufundisha vitu practical. Kuna wakati tunaona wanachuo wa engineering hapo udsm, wakisolve papers tu na wanafaulu vizuri. Wakirudi utasikia wakisema karudisha ya mwaka huu au ule.
Tatizo nyingine kubwa ni kuwa, siasa zimeanzia hadi NECTA huko, siku hizi ni kama hakuna kufeli, jambo ambalo linafanya vyuo kuwa na wanavyuo wengi walio na uwezo usioridhisha.
 
Endeleeni kupambana Mkuu... Japo Huku Kitaa Akili Za Darasani Hazina Undugu Na Akili Za Mtaani
 
Miaka inaenda Perry ulishamaliza chuo,kuolewa na sasa una mapacha kabisa,hongera sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…