Dakika 45: Job Ndugai asisitiza wananchi wafikirie uwezekano wa serikali tatu.

Dakika 45: Job Ndugai asisitiza wananchi wafikirie uwezekano wa serikali tatu.

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,207
Reaction score
13,839
Katika kipindi cha Dakika 45 jioni hii Ndg J Ndugai kwa kweli amenikosha sana.

Amesema yale ambayo wana CCM wengi wanaogopa kusema hadharani, Na amelisema suala la serikali tatu ndani ya muungano bila woga wala kujificha ficha.
Na kuna wakati mwandishi wa habari Selemani Seminyu alionekana akishangaa shgaa kutokana na msimamo huo wa Ndugai.
Ndugai amesema kazi iliyofanywa na wazee wetu hawa Warioba,Salim A Salim na hata kina Palamagamba Kabudi na Prof Baregu na kina Mvungi, wamejitahidi sana kuzunguka nchi nzima kupata maoni ya wananchi katika suala la aina ya muungano wetu.

Kwa hiyo , Ndugai kasema, pendekeo la serikali tatu lina uhalali wake kwa vile miundo mingine inaonekana kutofaa kwa sasa, nakwa vyovyote serikali moja au zile zile mbili hazikubaliki kabisa na wenzetu Wazanzibari.

Sasa hivi kuna bunge la wawakilishi Zanzibar na akasema ni wakati muafaka kuwa na bunge la Tanganyika sasa, na baadaye mfumo mpya wa serikali ya tatu ya muungano.

Binafsi mimi naona ni mawazo ambayo hata wana CCM wa Tanganyika wanayaunga mkono.

Hongera Ndg J Ndugai kwa kutokuwa mnafiki.
 
...Kwa hiyo , Ndugi kasema, pendekeo la serikali tatu lina uhalali wake kwa vile miundo mingine inaonekana kutofaa kwa sasa, nakwa vyovyote serikali moja au zile zile mbili hazikubaliki kabisa na wenzet Wazanzibari....
Ngoja naye asubiri kibano kwenye vikao vya chama kama walivyopewa akina Filikunjombe, Lugora etc
 
Lakini hayo siyo mawazo ya Chama. Chama kinasema serikali mbili kama zilivyo. Yeye anapingana na chama chake?

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Lakini hayo siyo mawazo ya Chama. Chama kinasema serikali mbili kama zilivyo. Yeye anapingana na chama chake?

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
Wakati mwongine chama kinachelewa sana kuweka msimamo wake wazi na kukumbuka shuka wakati ndo kunakucha.
Wengi tunajiuliza kilikuwa wapi wakati wa muafka wa Zanzibari, kitu ambacho ndio msingi mkubwa wa Wazanzibari kupenda kujitoa katika mfumo wa sasa na hatimaye nayo Tanganyika kung'amua kuwa tunacheza mchezo ambao si endelevu.
 
Katika kipindi cha Dakika 45 jioni hii Ndg J Ndugai kwa kweli amenikosha sana.

Amesema yale ambayo wana CCM wengi wanaogopa kusema hadharani, Na amelisema suala la serikali tatu ndani ya muungano bila woga wala kujificha ficha.
Na kuna wakati mwandishi wa habari Selemani Seminyu alionekana akishangaa shgaa kutokana na msimamo huo wa Ndugai.

Binafsi mimi naona ni mawazo ambayo hata wana CCM wa Tanganyika wanayaunga mkono.

Kwa nyaraka ambazo nimebahatika kuziona, wana CCM (wakiwemo wa mabaraza ya katiba) waliopata semina ya Nape na baadhi ya wakuuwa chama hicho bado wanataka serikali 2. Wana - CCM wa kawaida kama wewe tuko pamoja kudai serikali ya Tanganyika.
 
Ndio inavyotakiwa kuwa Taifa kwanza na shengesha ya vyama baadae
 
Kwa nyaraka ambazo nimebahatika kuziona, wana CCM (wakiwemo wa mabaraza ya katiba) waliopata semina ya Nape na baadhi ya wakuuwa chama hicho bado wanataka serikali 2. Wana - CCM wa kawaida kama wewe tuko pamoja kudai serikali ya Tanganyika.
Msingi wa hoja ya serikali tatu umesisitizwa vile vile na Mwenyekiti wa Tume ya Rasimu ya Katiba mpya Waziri Mkuu mstaafu Joseph Warioba na wazee wenziwe kama S A Salim (ambao ni CCM damu damu)na hata wale wa vyama vingine kama Prof Baregu, Mvungi na msomi Palamagamba.
Hili si swala la itikadi tu bali aina ya Taifa tunalolitaka.
 
kasema tu kuwafurahisha watazamani moyoni anajua mamuzi ya chama chake kupinga serikali tatu.
hakuna watu ninaowaogopa kama vingozi wenu wa CCM
hawatekelezi wanayoyasema majukwaani.
ni wepesi kusahau waliyoahidi kwa wananchi wao.
kama kamati kuu ishaamua na kuna waraka kwenda kwa Warioba kupinga serikali tatu na hata boss wake mama makinda
anapinga serikali tatu sasa iweje aseme kama ulivomnukuu???
 
Ngoja naye asubiri kibano kwenye vikao vya chama kama walivyopewa akina Filikunjombe, Lugora etc
Hapo ndipo CCM inapozidi kujichimbia kaburi.
Yani mtu akiwa mkweli hawezi kukubalika ndani ya CCM. wanataka wanafki tuu.
NB: Mkuu avatar yako imenichekesha mno.
 
Msingi wa hoja ya serikali tatu umesisitizwa vile vile na Mwenyekiti wa Tume ya Rasimu ya Katiba mpya Waziri Mkuu mstaafu Joseph Warioba na wazee wenziwe kama S A Salim (ambao ni CCM damu damu)na hata wale wa vyama vingine kama Prof Baregu, Mvungi na msomi Palamagamba.
Hili si swala la itikadi tu bali aina ya Taifa tunalolitaka.

Sikatai.. Uliyoyasema hapa nayakubali. Lakini semina anazoendesha Nape na maoni (ambayo wameyafanya kuwa ya chama) wanataka serikali mbili. Wanapinga kabisa serikali tatu. Hebu fuatlilia, waraka huu upo siyo wa siri.
 
ndungai mjamja san....ukiangalia siasa anazofanya sasahivi kashaona upepo unavyokwenda...
 
Uspika raha bana.,Unajua katika rasimu ya katiba mpya ya Muungano inaonyesha spika hatakiwi kuwa mbunge au kiongozi katika chama katika muda wa miaka mitano iliyopita. Ndugai ameliona hili kwamba kwa sifa hizi hawezi tena kuwa spika na worse enough bado anautaka uspika rejea mazungumzo yake ya awali alipohojiwa juu ya maoni yake katika rasimu mpya alisema haiwezekani spika asiwe mbunge akitoa mifano anuai kama vile chama cha madaktari kisivyoweza kuongozwa na mtu asiye daktari. Wapi kwa kutokea ni kupush kwa serikali tatu ambayo itasababisha kuwa na bunge la Tanganyika ambalo Bw. Job ndo analitolea macho. Hofu yangu kukiwa na vipengele vinavyokinzana na matakwa yake tutapata kauli nyingine tata........
 
Katika kipindi cha Dakika 45 jioni hii Ndg J Ndugai kwa kweli amenikosha sana.

Amesema yale ambayo wana CCM wengi wanaogopa kusema hadharani, Na amelisema suala la serikali tatu ndani ya muungano bila woga wala kujificha ficha.
Na kuna wakati mwandishi wa habari Selemani Seminyu alionekana akishangaa shgaa kutokana na msimamo huo wa Ndugai.
Ndugai amesema kazi iliyofanywa na wazee wetu hawa Warioba,Salim A Salim na hata kina Palamagamba Kabudi na Prof Baregu na kina Mvungi, wamejitahidi sana kuzunguka nchi nzima kupata maoni ya wananchi katika suala la aina ya muungano wetu.

Kwa hiyo , Ndugai kasema, pendekeo la serikali tatu lina uhalali wake kwa vile miundo mingine inaonekana kutofaa kwa sasa, nakwa vyovyote serikali moja au zile zile mbili hazikubaliki kabisa na wenzetu Wazanzibari.

Sasa hivi kuna bunge la wawakilishi Zanzibar na akasema ni wakati muafaka kuwa na bunge la Tanganyika sasa, na baadaye mfumo mpya wa serikali ya tatu ya muungano.

Binafsi mimi naona ni mawazo ambayo hata wana CCM wa Tanganyika wanayaunga mkono.

Hongera Ndg J Ndugai kwa kutokuwa mnafiki.

........acha uongo hakuna mwana ccm asiyekuwa mnafiki, including you!
 
Duh njaa mbaya jamani kila anayepiga kona anamipango ya kuizungukia kwa mbele akafunge goli
 
Lakini hayo siyo mawazo ya Chama. Chama kinasema serikali mbili kama zilivyo. Yeye anapingana na chama chake?

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
Saa ipo nayo yaja ambapo kila mwenye mwili atashangaa maana wimbo ambao haukuzoeleka utaimbwa na kila mmoja na sauti hiyo itatetemesha wengi......Tanzania njema ni lazima izaliwe watu wapende ama wasipende! Acha wafy wazike wafu wao kama kuna anayeweza kumrudisha Yesu kaburini kwa mara ya pili na asinane sasa na kuipinga hii dunamis nami nitajua ya kuwa kilichokwisha nenwa na Mungu yupo wa kulipinga! Kila iitwapo leo tunaikaribia hiyo siku huku maadui wa nchi hii wakidhani labda upepo utabadili mwelekeo. To their surprise hata nawe yanaanza kuwageuka!

Mafisadi the only safe ways ni kutubu na kufanya sawasawa na sheria za nchi otherwise the worst is to come.
 
Back
Top Bottom