mageuzi1992
JF-Expert Member
- Apr 9, 2010
- 2,502
- 256
Katika kipindi cha Dakika 45 jioni hii Ndg J Ndugai kwa kweli amenikosha sana.
Amesema yale ambayo wana CCM wengi wanaogopa kusema hadharani, Na amelisema suala la serikali tatu ndani ya muungano bila woga wala kujificha ficha.
Na kuna wakati mwandishi wa habari Selemani Seminyu alionekana akishangaa shgaa kutokana na msimamo huo wa Ndugai.
Ndugai amesema kazi iliyofanywa na wazee wetu hawa Warioba,Salim A Salim na hata kina Palamagamba Kabudi na Prof Baregu na kina Mvungi, wamejitahidi sana kuzunguka nchi nzima kupata maoni ya wananchi katika suala la aina ya muungano wetu.
Kwa hiyo , Ndugai kasema, pendekeo la serikali tatu lina uhalali wake kwa vile miundo mingine inaonekana kutofaa kwa sasa, nakwa vyovyote serikali moja au zile zile mbili hazikubaliki kabisa na wenzetu Wazanzibari.
Sasa hivi kuna bunge la wawakilishi Zanzibar na akasema ni wakati muafaka kuwa na bunge la Tanganyika sasa, na baadaye mfumo mpya wa serikali ya tatu ya muungano.
Binafsi mimi naona ni mawazo ambayo hata wana CCM wa Tanganyika wanayaunga mkono.
Hongera Ndg J Ndugai kwa kutokuwa mnafiki.
Mkuu hata mimi nilimcheki Ndungai kwenye kipindi cha dk 45 kwa kweli kwa hilo la serikali tatu alinikosha sana. Hakumumunya kama wenzake wa chama chake ambao ukiongelea serikali tatu kuna baadhi mapovu yanawatoka mpaka wanafikiria kuchakachua hicho kipengele. Pamoja na hayo kuna maeneo alikuwa anamumunya maneno kidogo mathalani kuhusu nizamu bungeni na uzalendo eti akasema baadhi ya wabunge si wazalendo wanaleta fujo bungeni na kauacha kutetea maslahi ya taifa. Sasa nikajiuliza hivi hao wanaosemekana walikuwa wakileta fujo si ndo walikuwa wakitetea maslahi ya taifa afu wakaonekana waleta fujo?. Mbali na hilo nilikerwa au huwa nakereka sana na hutu mtangazaji anayeitwa Seleman Semunyu...hafai kwa kipindi kama hicho.....kwanza anaonekana mwoga!...anatetemeka.....si jasiri wakuuliza....Anamuachia sana mzungumzaji hata pale unapohisi mzungumzaji kaongea pumba..kiasi cha kuhitaji kuulizwa kitu atoe ufafanuzi...lakini kwa semunyu hilo halipo!!! tena mara nyingine maswali yake huonekana kama kakaririshwa na watu fulani...yaani kaambiwa ukaulize hivi....na vile! Shame on Him....ITV wafikirie kumwambia a Improve au watafute mtu mwingine kama Rainfred Masako....ndio kipindi kitapendeza.....vinginevyo kitazidi kuwa doroooo!