manchoso
JF-Expert Member
- Jul 27, 2011
- 1,605
- 2,055
Mechi hii imechezwa jana majira ya saa 11 alfajir
mechi ilianza kwa kasi na toka mwanzo mwa mchezo Yanga ilitaka kuonyesha umwamba wake mbele ya simba na wakajipatia goli la mapema dakika ya 2 kupitia kwa Bernad Morrison.llilkuwa moja ya magoli matamu kabisa kushuhudiwa ndani ya uwanja wa taifa kwani alianza kutambaa na mpira kwenye chaki na akaingia nao ndani ya box kwa kasi ya swala na kumchambua manula na kuwaacha mabeki wa simba wameduwaa, -0baada ya kuingia goli walilalamika kuwa wakati anatambaa na mpira ulikuwa umeshatoka lakin refa alishaweka kati
hazikupita dakika nyingi ndani ya dakika ya 8 Morrison aliwaliza tena simba kwa goli la pili amabalo lilifanana sana na lile goli la kwanza baada ya kuwafunga tela mabek wa simba akaingia nayo kwenye box na kumtungua manula.baada ya hapo kukawa na kosa za hapa na pale ila kiukweli simba walizidiwa sana na yanga kila idara, kidogo mchezaji alieonyesha uhai ni yule kahata na hata kuna muvu moja alijaribu kuwatoka mabek wa yanga ila alipigwa tackling na mchezaji mmoja wa yanga ambae alionekana ni mdogo sana ila ye sio feitoto, sizani hata kafikisha hata miaka kum kwa umrii kwa kweli nilimuona ni mdogo mno jina lake simjui sura yake ni ngen la nilijua ni kawaida yanga kuibua yoso mahiri walipita pia kina silvatus ibrahim vijana wadogo waliokuwa wakipiga mpira ulioenda shule
Hadi aftertime mbili bila, wakati wa mapumziko nilienda jukwaa la simba nikawa nabadilishana mawazo na mjomba angu shabiki wa simba alietoka morogoro kuja kushuhudia timu yake alikuwa na huzuni sana ila akaniambia wametuachia kwa vile eti washachukua ubingwa, niliwaona pia marafiki zangu kina amos sikuwa najua amos ni mshabiki wa timu gani lakin kwa jinsi alivyonuna nilijua atakuwa simba sababu yanga wote walikuwa na furaha.pia nilijaribu kuangaza bila mafanikio kama ningeweza kumuona yule mzee wa utopolo lakin watu uwanjani walikuwa wengi sana sikuweza kumuona
wakati wa mampumziko nilikaa nikatafakari haya magoli yote mawili yamepitia upande wa kulia wa huyu beki shomari kapombe nikawa najiuliza kapombe leo ana nini?ndo huyu kweli mrithi wa nsajigwa? hakuwa mchezon kabisa kuna wakati alipigwa kibaiskel akaanguka kama gunia la mkaa, mashabiki wa yanga walishangilia sana lile tukio ila mimi lilinihuzunisha
kipindi cha pili kilianza pia kwa kasi huku yanga wakiendelea kulisakama lango la simba amabao hawakuwepo mchezoni kabisaaa na kwenye dakika ya 56 morrison alipenyezewa pasi safi akabaki yeye na manula lakin alipiga shuti kubwa likapaa hewani, pamoja na kukosa hilo goli morrison leo alionyesha uwezo mkubwa ambao ulimshangaza kila mtu alikuwa akiifanya beki ya simba anavyotaka alinikumbusha usiku ule zizzou alivyowatesa wabrazil pale frankfurt au siku ile fernando redondo alipowanyanyasa manchester kwa pasi za kisigino pale uingereza, morrison leo alikuwa na vitu vyote chenga za redondo,akili ya zizzou,stamina ya roberto carlos na akienda hewani alikuwa akipiga vichwa mithili ya jurgen klinsman kwa kweli ilikuwa ni burudani leo kumtazama morrison
kwenye dakika ya 70 nchimbi alimtoka beki wa simba ule ule upande wa kapombe na kupiga shuti kali iliyomshinda aishi manula na kuiandikia yanga goli la tatu, goli hili lilinistua nikapiga kelele nyingi hadi nikaamsha majirani kumbe bhana nilikuwa ndotoni
Ndoto ya leo ilikuwa taamu sana tena nimejilaumu sana kwa nini hili goli la tatu nimepiga kelele sana hadi usingizi ukakata nikaamka ningerelax nadhan ningejionea magoli meng leo tukimtandika mnyama.
NB
Kuna imani inanijia Usiku wa leo ntaota nipo peponi, nimekuwa nikiwaza sana raha za peponi ambazo jicho wala sikio la binadamu haliwahi kuona wala kusikia!!!!Namuomba Mungu anisaidie niote nipo janatul firdaus pepo ya juu kabisa nikiwa na Mitume na watu wema usiku wa leo pia sitashiba sana nisije nikavimbiwa nikashindwa kula vitamu vitamu vya pepon.
mechi ilianza kwa kasi na toka mwanzo mwa mchezo Yanga ilitaka kuonyesha umwamba wake mbele ya simba na wakajipatia goli la mapema dakika ya 2 kupitia kwa Bernad Morrison.llilkuwa moja ya magoli matamu kabisa kushuhudiwa ndani ya uwanja wa taifa kwani alianza kutambaa na mpira kwenye chaki na akaingia nao ndani ya box kwa kasi ya swala na kumchambua manula na kuwaacha mabeki wa simba wameduwaa, -0baada ya kuingia goli walilalamika kuwa wakati anatambaa na mpira ulikuwa umeshatoka lakin refa alishaweka kati
hazikupita dakika nyingi ndani ya dakika ya 8 Morrison aliwaliza tena simba kwa goli la pili amabalo lilifanana sana na lile goli la kwanza baada ya kuwafunga tela mabek wa simba akaingia nayo kwenye box na kumtungua manula.baada ya hapo kukawa na kosa za hapa na pale ila kiukweli simba walizidiwa sana na yanga kila idara, kidogo mchezaji alieonyesha uhai ni yule kahata na hata kuna muvu moja alijaribu kuwatoka mabek wa yanga ila alipigwa tackling na mchezaji mmoja wa yanga ambae alionekana ni mdogo sana ila ye sio feitoto, sizani hata kafikisha hata miaka kum kwa umrii kwa kweli nilimuona ni mdogo mno jina lake simjui sura yake ni ngen la nilijua ni kawaida yanga kuibua yoso mahiri walipita pia kina silvatus ibrahim vijana wadogo waliokuwa wakipiga mpira ulioenda shule
Hadi aftertime mbili bila, wakati wa mapumziko nilienda jukwaa la simba nikawa nabadilishana mawazo na mjomba angu shabiki wa simba alietoka morogoro kuja kushuhudia timu yake alikuwa na huzuni sana ila akaniambia wametuachia kwa vile eti washachukua ubingwa, niliwaona pia marafiki zangu kina amos sikuwa najua amos ni mshabiki wa timu gani lakin kwa jinsi alivyonuna nilijua atakuwa simba sababu yanga wote walikuwa na furaha.pia nilijaribu kuangaza bila mafanikio kama ningeweza kumuona yule mzee wa utopolo lakin watu uwanjani walikuwa wengi sana sikuweza kumuona
wakati wa mampumziko nilikaa nikatafakari haya magoli yote mawili yamepitia upande wa kulia wa huyu beki shomari kapombe nikawa najiuliza kapombe leo ana nini?ndo huyu kweli mrithi wa nsajigwa? hakuwa mchezon kabisa kuna wakati alipigwa kibaiskel akaanguka kama gunia la mkaa, mashabiki wa yanga walishangilia sana lile tukio ila mimi lilinihuzunisha
kipindi cha pili kilianza pia kwa kasi huku yanga wakiendelea kulisakama lango la simba amabao hawakuwepo mchezoni kabisaaa na kwenye dakika ya 56 morrison alipenyezewa pasi safi akabaki yeye na manula lakin alipiga shuti kubwa likapaa hewani, pamoja na kukosa hilo goli morrison leo alionyesha uwezo mkubwa ambao ulimshangaza kila mtu alikuwa akiifanya beki ya simba anavyotaka alinikumbusha usiku ule zizzou alivyowatesa wabrazil pale frankfurt au siku ile fernando redondo alipowanyanyasa manchester kwa pasi za kisigino pale uingereza, morrison leo alikuwa na vitu vyote chenga za redondo,akili ya zizzou,stamina ya roberto carlos na akienda hewani alikuwa akipiga vichwa mithili ya jurgen klinsman kwa kweli ilikuwa ni burudani leo kumtazama morrison
kwenye dakika ya 70 nchimbi alimtoka beki wa simba ule ule upande wa kapombe na kupiga shuti kali iliyomshinda aishi manula na kuiandikia yanga goli la tatu, goli hili lilinistua nikapiga kelele nyingi hadi nikaamsha majirani kumbe bhana nilikuwa ndotoni
Ndoto ya leo ilikuwa taamu sana tena nimejilaumu sana kwa nini hili goli la tatu nimepiga kelele sana hadi usingizi ukakata nikaamka ningerelax nadhan ningejionea magoli meng leo tukimtandika mnyama.
NB
Kuna imani inanijia Usiku wa leo ntaota nipo peponi, nimekuwa nikiwaza sana raha za peponi ambazo jicho wala sikio la binadamu haliwahi kuona wala kusikia!!!!Namuomba Mungu anisaidie niote nipo janatul firdaus pepo ya juu kabisa nikiwa na Mitume na watu wema usiku wa leo pia sitashiba sana nisije nikavimbiwa nikashindwa kula vitamu vitamu vya pepon.