Daktari: Tanzania inaongoza kwa unywaji pombe Afrika. Kwa mwaka kila Mtanzania anakunywa ndoo ndogo

huyo Dr Omar Ubuguyu hizo data amezitengenezea chumbani kwake. Tanzania haiko hata katika top twenty ya nchi zinjazokunywa bia kwa wingi africa.

 
Muongo Tanzania hakuna wanya pombe aache masikharaa kabisa..
Huko bonge anapajua?
 
Huo utafiti utulipe fidia kw sisi ambao hatunywi pombe...anaposema kila mtanzania...
Au hyo pombe inaingia mwilini by diffusion?
 
Ngoja nicheki vzr sheria ya takwimu kama inamruhusu kutangaza hizi data, anyway kwanza lita 9.1 karibu ni sawa na kreti moja la serengeti lite, kwa mwaka??? Mm haya ni matumizi yangu kwa wiki
 
Kuna mtu kufikia mwezi huu ana litre 1000 sa mwaka ukiisha atakua anaela na kuzama
 
Labda ndoo ndogo kwa wanaokunywa pombe kali
lakini kwenye bia ni mwendo wa pipa kwa mwaka.
 
Ni rahisi kupata hizo data; unaangalia uzalishaji kwa mwaka pamoja na mauzo kwa mwaka katika viwanda vyetu (lita).
Ni muhimu pia, angesema madhara yake ni nini?​
 
Uongo
Sasa lita 10 au 20 kwa Mwaka ndio nyingi!?
 
Kindoo kwenye kikao changu mwanana nyama za kutosha, nikianza saa5 asbh siku ya jmos wallah kabla watoto hawajarudi sunday school ntakuwa nimekifuta muda tu tena naomba nyongeza ya kindoo kingine ili nisukutue maheng'oo.

Hii ripoti ni batili inaudhurumu mtima wangu.
Nauhakika kwa mwaka mi nagida pipa5 za bia, chingili maringo vindoo4, lusuo debe3 na chimpumu geleni5.
 
Tusisingiziane kwa sababu sisi wengine hatunywi
 
acheni uongo tupe chanzo cha hiyo takwimu, sidhani hata kumi bora tumo
 
Daktari atembelee Burundi hasa pale buja baada ya kila hatua 3 kuna groccery wanauza visungura..Baa za kule zipo nje yani ikifika jioni mtaa mzima kuna Baa ni wewe na meza yako tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…