Dalili za jezi za Simba na Yanga

Dalili za jezi za Simba na Yanga

HIZI hesabu za kwenye calculator raha sana.
mashabiki wenyewe hawa buku tu ya ada kwa mwezi hawalipi ndo wanunue jezi og 30000?
asilimia 50 ya jezi za hapa bongo ni feki

Yanga waweke wazi wameuza JEZI ngapi za Yanga toka kuanza kwa mkataba na GSM. Simba wao wataingiza Bilioni Moja ama JEZI ziuzwe ama zisiuzwe
 
Wewe ni mfanya biashara kweli wewe?
Unajua kodi inayolipwa?Unadhani kuna biashara yenye faida kubwa namna hiyo?
Habari za mchana wadau wa Soka. Napata pilau langu hapa nikiandika uzi huu.

Kwanza kabisa, pongezi kwa Simba kwa kuweka wazi kiasi itakachopokea kwenye mauzo ya Jezi kutoka kwa Vunja Bei Group.

Mkataba Ni wa Tsh. 2 Bilioni kwa kipindi cha miaka miwili. Kwa maana nyingine ni Tsh. 1 Bilioni kwa mwaka.

Kwa bahati mbaya sana waandishi wetu hawakuuliza maswali ya msingi kwenye ile press conference.

Ningependa kujua hiyo Tsh. 2 Bilioni Simba inaipata kwa namna gani na kwa muda gani.

Je kila Mwezi, Robo ya Mwaka, Nusu ya Mwaka ama kwa mwaka. Je Vunja Bei anapaswa kuweka wazi idadi ya JEZI atakazoingiza na kuziuza nchini?

Mwenye majibu ya maswali hayo anijuze.

Sasa tuje Yanga, hapa kuna shida kubwa kwa sababu hatujui ni mkataba wa kiasi gani na wa muda gani.

Ningependa kujua mkataba wa GSM kutengeneza jezi za Yanga ni wa kiasi gani na wa muda gani?

Kwa miaka mitatu iliyopita klabu ya Yanga imepokea kiasi gani kutoka kwa GSM kwenye mauzo ya JEZI? Idadi ya JEZI zilizoingizwa na kuuzwa?

Je Mkataba huo unaisha lini? Na mchakato wake uko vipi?

Lazima tukubale Biashara ya JEZI inalipa sana especially kwa Simba na Yanga kwa sababu na fan base kubwa.

Tufanye hesabu za haraka.

Kwa mujibu wa mtandao wa Ali Baba, kutengeneza jezi 10,000 inagharimu $2 sawa na Tsh. 5,000. Kumbuka unaponunua mzigo mkubwa una enjoy economies of scale.

Kadiria unaweka order ya JEZI 200,000

Gharama ya manunuzi - Tsh. 1 Bilioni
Gharama za kuingiza mzigo - 30% sawa na Tsh. 300 Millioni.

Jumla ya Gharama za Manunuzi - Tsh. 1.3 Bilioni

Tuje Sokoni sasa.

Wastani wa Bei ya JEZI - Tsh. 30,000
Mauzo ya JEZI Laki Mbili - Tsh. 6 Bilioni

Toa Gharama za Manunuzi itabaki Tsh. 4.7 Bilioni
Toa Gharama zingine kama Tsh. 700 Milioni.

Kwa makisio, muigizaji anabakiwa na kama Tsh. 4 Bilioni.

Sasa Swali klabu inapokea kiasi gani?

Ni vizuri tupate taarifa hizi. Na sio kwa Yanga Bali hata kwa Simba. Maana hizi na timu za wananchi.

Karibuni tujadiliane.
 
Nahisi alimaanisha wapenzi ama mashabiki kwa lugha nyepesi.
Kwanza si kweli kimahesabu na pili hata tukisema ni kweli, mashabiki wa kununua mataulo ya Simba hawafiki hata 100,000.

Mashabiki wenyewe ukiwaangalia karibu 60% wanavaa jezi za mwaka Jana uwanjani.

Halafu clubs zetu huwa hazitoi mahesabu yake kwa jamii. Ni klabu feki tu na maelezo yake ni fake.
 
mkataba wa simba na vunja bei sio jezi peke yake yake.. Vunja bei kakodishwa trade mark ya simba..

so anaweza akatengeneza chochote kile akakiwekea nembo ya simba na kuuza.. na hata anaruhusiwa kuandaa matamasha kwa kutumia nembo ya simba

nje ya simbe kupata hizo 2b za jersey pia kila mauzo ya bidhaa yenye nembo ya simba kuanzia jersy hadi shanga kama ataziweka basi simba anapata % .

sijajua ni % ngapi hawajaiweka wazi ila kwenye mauzonya bidhaa zenye. nembo ya simba vubja bei anaipa simba percent.

na kwenye events pia vubja bei akiandaa tamasha kwa kutumia nembo ya simba wanakula
percent pia.


hivi unafikiri Mhindi (Mo) akubali 2b kavu bila marupurupu mengine wakat yeye mfanyabiashara anajua umuhimu wa trademark angalia


ukisoma between the line alichosema Vunja bei wakat anatangazwa mshindi wa tenda alisema kilicho mfanya Simba wampe yeye, sio hizo 2B maana hata washindani wengine walitoa kama hizo na zaid.

sema yeye alipewa sababu aliwaonyesha simba PROPOSAL YAKE JINSI ATAKAVYOIKUZA BRAND YA SIMBA.

utaona kuwa kwa maana nyingine aliwaonyesha simba kuwa watapata pesa zaidi kwa njia zingine maana simba atapata zaid ya hizo 2B. kitakachoongezeka itategemea na mauzo na matasha. Vunja bei akizembea promo asiuze sana imekula kwake kwa sababu simba minimum 2B yake iko pale pale. Vunja bei akiuza sana simba anafaidika zaid

washinda. wengine waliweka tu fixed amount basi

Yanga mkataba mpya wa jersy wawaige simba wasidiki na swala la kupewa fixes amount na 5% ya mauzo
 
mkataba wa simba na vunja bei sio jezi peke yake yake.. Vunja bei kakodishwa trade mark ya simba..

so anaweza akatengeneza chochote kile akakiwekea nembo ya simba na kuuza.. na hata anaruhusiwa kuandaa matamasha kwa kutumia nembo ya simba

nje ya simbe kupata hizo 2b za jersey pia kila mauzo ya bidhaa yenye nembo ya simba kuanzia jersy hadi shanga kama ataziweka basi simba anapata % .

sijajua ni % ngapi hawajaiweka wazi ila kwenye mauzonya bidhaa zenye. nembo ya simba vubja bei anaipa simba percent.

na kwenye events pia vubja bei akiandaa tamasha kwa kutumia nembo ya simba wanakula
percent pia.


hivi unafikiri Mhindi (Mo) akubali 2b kavu bila marupurupu mengine wakat yeye mfanyabiashara anajua umuhimu wa trademark angalia


ukisoma between the line alichosema Vunja bei wakat anatangazwa mshindi wa tenda alisema kilicho mfanya Simba wampe yeye, sio hizo 2B maana hata washindani wengine walitoa kama hizo na zaid.

sema yeye alipewa sababu aliwaonyesha simba PROPOSAL YAKE JINSI ATAKAVYOIKUZA BRAND YA SIMBA.

utaona kuwa kwa maana nyingine aliwaonyesha simba kuwa watapata pesa zaidi kwa njia zingine maana simba atapata zaid ya hizo 2B. kitakachoongezeka itategemea na mauzo na matasha. Vunja bei akizembea promo asiuze sana imekula kwake kwa sababu simba minimum 2B yake iko pale pale. Vunja bei akiuza sana simba anafaidika zaid

washinda. wengine waliweka tu fixed amount basi

Yanga mkataba mpya wa jersy wawaige simba wasidiki na swala la kupewa fixes amount na 5% ya mauzo

Kweli Kabisa Yanga wana chakujifunza hapa maana kwa mkataba wa sasa hivi wanapata kiduchu sana.

Wapitie tena mkataba wao na GSM.
 
GSM anakula faida ya jezi za Yanga 2bn kwa mwaka, anatumia 1bn kwa njia ya ufadhili wa ops za team na bado ananyenyekewa kama Mfalme, viongozi wa Yanga ni majuha na ma chief Mangungo.
 
GSM anakula faida ya jezi za Yanga 2bn kwa mwaka, anatumia 1bn kwa njia ya ufadhili wa ops za team na bado ananyenyekewa kama Mfalme, viongozi wa Yanga ni majuha na ma chief Mangungo.

Kwa mahesabu hayo hakuna ufadhili hapo bali GSM ndio anayefadhiliwa na Yanga.

Swali. Nani atamfunga paka kengele?
 
Kwa mahesabu hayo hakuna ufadhili hapo bali GSM ndio anayefadhiliwa na Yanga.

Swali. Nani atamfunga paka kengele?
Viongozi wa Yanga na wao wanapata mgao wake kutoka GSM ndio maana wanashinda ofisi za GSM kila siku, hakuna wa kumfunga paka kengele.
 
Basi mkataba wa Yanga una matatizo makubwa.

Kama Bei ya JEZI moja ni Tsh. 30,000 iweje Yanga wapewe Tsh. 1,500. Hiyo ni asilimia ni 5% tu

Kama hiyo ndio hali halisi Mkataba wa Simba Ni bora zaidi maana wana uhakika wa kupata Bilioni 1 kwa mwaka Vunja Bei auze ama asiuze.

Hata GSM wakiuza JEZI Laki Moja kwa mwaka klabu ya Yanga wataambulia Tsh. 150 Milioni Tu wakati Jumla ya Mauzo ni Tsh. 3 Bilioni kwa JEZI Hizo Laki moja.

Viongozi wa Yanga wanasimama wapi kwenye hili jambo.
Wanalipwa posho..pamoja na kusajiliwa wachezaji...
 
Sasa hapo inaelekea mkataba wa Yanga una utata. Kama GSM wanailipa Yanga sh. 1,500/= kwa kila jezi wanayoiuza, lakini idadi ya jezi zinazouzwa haijulikani, si anaweza kusema ameuza jezi 20,000 tu na hakuna atakayehoji maana hakuna takwimu? Basi heri mkataba wa Simba, maana wao hawahitaji kujua idadi ya jezi zitakazouzwa, wanachohitaji ni 2B ndani ya miaka miwili, msala wa wateja na idadi yake wamemuachia muuzaji
Sahihi kabisa
 
Wanalipwa posho..pamoja na kusajiliwa wachezaji...

Daaa kweli Bongo Nyosso. Ndio maana Uongozi wa Yanga hautaki kuitisha mkutano mkuu wa wanachama.

Taarifa itolewe tujue JEZI ngapi zimeuzwa ndani ya miaka mitatu iliyopita na Yanga wamepokea kiasi gani.
 
Back
Top Bottom