Zurie
JF-Expert Member
- Jul 6, 2014
- 2,012
- 5,571
Dalili zinazoashiria magonjwa ya akili ni nyingi sana, baadhi tu ni ambazo zimegawanyika katika makundi matatu ni kama ifuatavyo:
i) Kihisia
· Kukosa furaha na kuhuzunika sana
· Kuwa na furaha sana kupita kiasi
· Wasiwasi na/ au woga kupita kiasi
· Kupunguza kuongea au kutokuongea kabisa au kuongea sana kupita kiasi
· Hasira za haraka haraka hata kufikia kupiga wengine
· Kuwa na msongo wa mawazo
· Kujitenga na watu na kupenda kukaa mwenyewe muda mwingi au kupenda kuwa na watu sana kuliko kawaida
· Kutokuwa na ari ya kufanya kazi au kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja bila ya kuzikamilisha
· Kutokuonyesha hisia yoyote usoni mwake (mf. furaha au huzuni nk)
· Kutokujijali usafi na muonekano wake
· Kuhisi maisha hayana thamani na kuona bora kufa kuliko kuishi na hatimaye kufikia uamuzi wa kujiua na hata kuua wengine.
ii) Kimwili
· Mwili kukosa nguvu au kuhisi mwili una nguvu sana kupita kiasi
· Kukosa usingizi au kulala usingizi sana kupita kiasi
· Kukosa hamu ya kula au kuwa na hamu sana ya kula
· Kutokutulia (kuhamanika) au kutulia sehemu moja muda mrefu bila ya kujisogeza
· Maumivu sehemu mbalimbali za mwili kama vile kichwa, mabega, mgongo, na viungo mbalimbali ambavyo akienda hospitali vipimo havionyeshi tatizo lolote la kimwili.
iii) Kiakili
· Kukosa umakini wa shughuli zake za kila siku
· Kusahau kwa haraka au kupoteza kumbukumbu
· Kukosa uwezo wa kupambanua mambo kwa mitazamo tofauti
· Kusikia sauti ambazo hazipo na kuona vitu ambavyo havipo
· Imani ya ajabu ambazo haziendani na mila, imani au desturi za jamii yake ; kama vile yeye ni mtu maarufu, au anaamini kuwa yeye ni Nabii
au anaamini kupokea taarifa kutoka kwenye redio au mitandao ya simu
· Pia anaamini ana nguvu ya ziada kutoka nje ya mwili yake inayomsababishia kutenda au kuwaza mambo anayoyawaza
· Anaamini mawazo yake yanapunguzwa au kuongezwa na watu wasiojulikana, vyombo vya habari kama vile Radio na TV kuwa vinazungumzia yeye, au vinaongea mawazo yake yeye
· Mawazo yake hayana mtiririko unaoeleweka.
i) Kihisia
· Kukosa furaha na kuhuzunika sana
· Kuwa na furaha sana kupita kiasi
· Wasiwasi na/ au woga kupita kiasi
· Kupunguza kuongea au kutokuongea kabisa au kuongea sana kupita kiasi
· Hasira za haraka haraka hata kufikia kupiga wengine
· Kuwa na msongo wa mawazo
· Kujitenga na watu na kupenda kukaa mwenyewe muda mwingi au kupenda kuwa na watu sana kuliko kawaida
· Kutokuwa na ari ya kufanya kazi au kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja bila ya kuzikamilisha
· Kutokuonyesha hisia yoyote usoni mwake (mf. furaha au huzuni nk)
· Kutokujijali usafi na muonekano wake
· Kuhisi maisha hayana thamani na kuona bora kufa kuliko kuishi na hatimaye kufikia uamuzi wa kujiua na hata kuua wengine.
ii) Kimwili
· Mwili kukosa nguvu au kuhisi mwili una nguvu sana kupita kiasi
· Kukosa usingizi au kulala usingizi sana kupita kiasi
· Kukosa hamu ya kula au kuwa na hamu sana ya kula
· Kutokutulia (kuhamanika) au kutulia sehemu moja muda mrefu bila ya kujisogeza
· Maumivu sehemu mbalimbali za mwili kama vile kichwa, mabega, mgongo, na viungo mbalimbali ambavyo akienda hospitali vipimo havionyeshi tatizo lolote la kimwili.
iii) Kiakili
· Kukosa umakini wa shughuli zake za kila siku
· Kusahau kwa haraka au kupoteza kumbukumbu
· Kukosa uwezo wa kupambanua mambo kwa mitazamo tofauti
· Kusikia sauti ambazo hazipo na kuona vitu ambavyo havipo
· Imani ya ajabu ambazo haziendani na mila, imani au desturi za jamii yake ; kama vile yeye ni mtu maarufu, au anaamini kuwa yeye ni Nabii
au anaamini kupokea taarifa kutoka kwenye redio au mitandao ya simu
· Pia anaamini ana nguvu ya ziada kutoka nje ya mwili yake inayomsababishia kutenda au kuwaza mambo anayoyawaza
· Anaamini mawazo yake yanapunguzwa au kuongezwa na watu wasiojulikana, vyombo vya habari kama vile Radio na TV kuwa vinazungumzia yeye, au vinaongea mawazo yake yeye
· Mawazo yake hayana mtiririko unaoeleweka.