Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kila siku siyo JumapiliKabla ya kuwa offended na imbecilization tunayofanyiwa, ni muhimu kukumbuka nchi yetu wenye kufikiri ni minority. Wakubwa wanapozungumza, wanajua hadhira yao ni watu wa namna gani kwa hiyo haishangazi wanapotoa hoja wanazotoa.
unaniuliza mimi? muulize ndumaroKabla ya katiba hii mbovu huko nyuma mlielimisha wangapi ndio mkapata hii mliyonayo sasa ?
Wewe bado sana kwenye haya mamboKabla hujampinga Ndumbaro jiulize wewe hapo unajua nini kuhusu katiba zaidi ya kufuata mkumbo wa kudai kuwa maandamano yameruhusiwa kikatiba? Labda na kingine mnachosemaga ni katiba kutoa uhuru wa watu kutoa maoni yao ambapo nyie huwa mnadhani huwa ni uhuru wa kutukana. Ndumbaro yuko sahihi 100% kuwa watu hawaijui kabisa hii katiba. Hiyo 50% aliyotaja ni kuwa 48% ni wafuasi wa chama cha Mbowe.
Wewe wasema.Wewe bado sana kwenye haya mambo
Hii tabia ya wanasiasa kuwakejeli wananchi ikome.kwanza muulize kule majimaji alifanya nini?View attachment 2732418
Mh Damas Ndumbaro ambaye ni Waziri wa Katiba na Sheria , ametamka hadharani kwamba zaidi ya 50% hawaijui Katiba ya sasa , Kwa tafsiri ya Kawaida ni kwamba zaidi ya nusu ya Wananchi hawaijui Katiba yao .
Kumuamini Ndumbaro kunahitaji roho ngumu iliyojaa Ujasiri wa kutukuka , Ndumbaro amewahi kuwa Wakala wa wachezaji wa FIFA , ambaye alifungiwa kushiriki masuala ya soka na Wachezaji kwa muda usiojulikana kwa UDANGANYIFU NA UTAPELI, tunawezaje kumuamini mtu huyu ?
Tanzania kuna watu wazima , Vijana na watoto , hawa ndio wanaounda 100% ya raia wote , na humo wamo ambao kwa umri wao na utoto wao kwa namna yoyote ile hawawezi kujua lolote lile kuhusu Katiba ya nchi , hawa nao wamo kwenye hiyo 50% ya wasioifahamu Katiba ya sasa?
Hata kama Waziri anatunga Uongo ili kuikwepa Katiba Mpya kwa lengo la kuokoa ccm , basi Ajitahidi kuupaka rangi uongo wake , kama kweli watanzani wote hao hawajui Katiba yao basi athibitishe namna alivyokokotoa hesabu hiyo ndani ya siku mbili au tatu za kuandaa huo uongo wake , alimhoji nani na yupi , wapi na lini ? aweke ushahidi mezani tuuone.
Hivi waliompa Uwaziri wa Sheria Ndumbaro walizingatia vitu gani ? mbona ni mwepesi sana ! ccm haina watu wengine wenye weledi hadi kutafuta mtu mwenye makandokando kama huyu , asiyejua juzi na jana aliongea nini ? huyu huyu aliwahi kudanganya kwamba Mchakato wa Katiba mpya utaanza Septemba (Ushahidi uko humu jf) , wakati akiyasema haya hawa Watanzania Mbumbumbu wa Katiba walikuwa % ngapi ?
Naomba nifupishe kwa kusema hivi KATIBA MPYA NI SASA na wala si baada ya miaka mitatu anayoitaka Ndumbaro na waliomtuma , PATACHIMBIKA .
Hajamaanisha namba yako ya simu bali amemaanisha namba ya kiutafiti inayopingana na hiyo ya waziri juu ya 50% ya watanzania kutojuwa na kuwa na ufahamu wa kutosha juu ya masuala ya katiba yetu. Soma kwa kutulia na jibu kwa utulivu. Sasa kama alichoandika tu hujakielewa vipi utaweza ielewa katiba vizuri? Ndio maana mh waziri amependekeza watu aina yako mpewe Elimu ndani ya miaka mitatu ili muielewe na kutunukiwa vyeti safi.Namba yangu ya nini ? Hivi mnadhani mnaweza kuua kila mtu ?
Waliipomuuzia Mwarabu Bandari walitoa elimu kwa muda gani ?Hajamaanisha namba yako ya simu bali amemaanisha namba ya kiutafiti inayopingana na hiyo ya waziri juu ya 50% ya watanzania kutojuwa na kuwa na ufahamu wa kutosha juu ya masuala ya katiba yetu. Soma kwa kutulia na jibu kwa utulivu. Sasa kama alichoandika tu hujakielewa vipi utaweza ielewa katiba vizuri? Ndio maana mh waziri amependekeza watu aina yako mpewe Elimu ndani ya miaka mitatu ili muielewe na kutunukiwa vyeti safi.
Mwarabu hajauziwa Bandari. Lakini pia katika masuala ya uwekezaji yanasimamiwa na kuongozwa na sheria zetu za uwekezaji. kwa kutumia wanasheria wetu waliosheheni uzoefu wa kutosha na kwa kila eneo Ndio wanaongalia na kuhakikisha kuwa sheria zinafuatwa na kuzingatia maslahi ya Taifa letu.Waliipomuuzia Mwarabu Bandari walitoa elimu kwa muda gani ?
Hawa akina Profesa Mruma ?Mwarabu hajauziwa Bandari. Lakini pia katika masuala ya uwekezaji yanasimamiwa na kuongozwa na sheria zetu za uwekezaji. kwa kutumia wanasheria wetu waliosheheni uzoefu wa kutosha na kwa kila eneo Ndio wanaongalia na kuhakikisha kuwa sheria zinafuatwa na kuzingatia maslahi ya Taifa letu.