Damascus: Urusi imeanza kuwaondoa wanajeshi wake nchini Syria kwa msaada wa Uturuki

Damascus: Urusi imeanza kuwaondoa wanajeshi wake nchini Syria kwa msaada wa Uturuki

MTZ 255Dar

JF-Expert Member
Joined
Sep 25, 2018
Posts
1,149
Reaction score
3,963
Shirika la Habari la Serikali ya Syria,SANAA limeripoti kwamba,Msafara wa wanajeshi kadhaa wa Urusi pamoja na vifaa vya kijeshi vimeanza kuondoka nchini Syria.

Video kadhaa zimeonesha msafara wa magari ya kijeshi ikiwemo mifumo ya ulinzi wa anga aina ya S-300/400, Vifaru aina ya T-64 na Magari ya kubeba Silaha yakiondoka kutoka eneo la KHMEIMIM AIRBASE iliyoko katika ufukwe wa Bahari ya Mediterannea.

Kumekuwa na mazungumzo kadhaa ya siri kati ya Uturuki na Urusi wa kuiruhusu Urusi kupitisha misafara ya wanajeshi wake na vifaa vya kijeshi kwenye maeneo yanayodhibitiwa na jeshi la Uturuki nchini Syria ili kuwarudisha nchini Urusi. Hii ni baada ya Waasi wa kundi la HTS kuipindua serikali ya Bashar Al Assad Mshirika wa Iran na Urus na kumlazimu kuomba hifadhi ya kisiasa nchini Urusi mnamo Desemba 08.

Urusi ilikuwa na wanajeshi wanaokadiriwa 12,000 nchini Syria tangu mwaka 2015 ilipojiingiza kijeshi nchini Syria ili kumsaidia Assad kupambana na waasi waliotaka kuiteka nchi hiyo. Hata hivyo,Baada ya Urusi kuivamia nchi ya Ukraine,Urusi iliwapunguza wanajeshi wake kutoka Syria kuwapeleka uwanja wa vita nchini Ukraine. Mpaka sasa,Urusi ilikuwa na wanajeshi wafikao 5,000 nchini Syria wengi wao wakiwa ni Washauri wa Kijeshi waliokuwa wakitoa mafunzo kwa jeshi la Syria tangu mwaka 2015.


View: https://youtube.com/shorts/nzwQYRddFAY?si=wn1CEHPgA5PK36Ex
 
Supa pawa la mchongo! Mission iliyompeleka huko imetimia? Au ilikuwa ni kumlinda Assad; ameondoka nao wanaondoka? Let's wait and see kuona influence ya Urusi na Iran ukanda huo.
 
Supa pawa la mchongo! Mission iliyompeleka huko imetimia? Au ilikuwa ni kumlinda Assad; ameondoka nao wanaondoka? Let's wait and see kuona influence ya Urusi na Iran ukanda huo.
Aja kimbia kwa aibu kama yule alie kimbia wavaa kobazi wa Somalia, Afghanistan
 
Hayo ni maridhiano mapya kati ya Trump na swahiba wake Putin.
Trump: I take Syria
Putin: I retain Ukrainian liberated region
 
Putin kaambiwa wanajeshi wake wapo salama waendelee tu kukaa syria.. sasa wanajeshi hawaelewi waendelee kukaa for what? maana lengo lao ni kuwapiga HTS na Al Qaeda ambao ndio wapo madarakani and Israel kafyeka silahakazi za stria 70% yakiwemo machuma S-300 na Pantsir scud n.k

Hivi hao Qauda wangepata kila kitu na zile ndege Israel angesumbuka kwa muda japo angesinda vita ila maumivu angepata.. sasa waasi wakitaka ku march to Jerusalem kama wasemavyo na hizo AK 47 wataishia kuzikana wenyewe njiani
 
Putin kaambiwa wanajeshi wake wapo salama waendelee tu kukaa syria.. sasa wanajeshi hawaelewi waendelee kukaa for what? maana lengo lao ni kuwapiga HTS na Al Qaeda ambao ndio wapo madarakani and Israel kafyeka silahakazi za stria 70% yakiwemo machuma S-300 na Pantsir scud n.k

Hivi hao Qauda wangepata kila kitu na zile ndege Israel angesumbuka kwa muda japo angesinda vita ila maumivu angepata.. sasa waasi wakitaka ku march to Jerusalem kama wasemavyo na hizo AK 47 wataishia kuzikana wenyewe njiani
Kambi za urusi zipo' Syria kabla osama hajaanza kunyoa,muwe mnadadisi mambo siyo kukurupuka tu na ushabiki wenu wa kidini
 
Back
Top Bottom