Dan Friedkin mmiliki wa AS Roma anamiliki ardhi kubwa Tanzania, mamlaka zimchunguze

Hiyo Tanzania kuwa na mapori ni mengi ni uongo mkubwa na propaganda tu. Na wenye akili wengi pia wanazungumza wageni kuchukua maeneo yenye madini, gesi na mafuta. Tanzania wako watu milioni 60 na wanazidi kuongezeka kwa kasi, hayo mapori mengi yanatoka wapi??
 
Hawa wanaweza kuwa ndio wale wafadhili wa Royol tour ambao tulifichwa , sasa wanapewa mapande ya aridhi, na wana binasifisha, fikiria Mzungu ana binasifisha Aridhi ya Umma.

View attachment 2610183
Acha wivu au wewe unafikiri uwekezaji ni nini! Hayo mapori hata yakiachwa wewe unafikiria yana maana gani! Wewe hujui kitu chochote Urusi yeyewe iliuza eneo la Alaska kwa USA!

Ukiwa Huna kitu cha kupost huku ni bora uwe unasoma hata madaftari ya wanao kuangalia maendeleo yao kuliko kuleta umbea na wivu huku, na kama huridhishwi nenda mahakamani kwani katiba inakupa nafasi hiyo nyambafu wewe!
 
Ndio maana nilisema humu nchi haiwezi kuendelea kwa kutegemea wawekezaji!!!! Tutafute business partners jamani tutakapostuka nchi yetu itakuwa nusu kwa nusu yaani nusu ina wananchi na nusu ina wawekezaji. Kila mwenye fedha ulaya na Marekani anawaza kumiliki ardhi na nchi ambayo ipo weak kulinda ardhi yake ni Tanzania. Inawezekanaje mtu binafsi anakodishwa Game reserve? next utasikia anakodishiwa National park au kipande cha bahari kutoka Mtwara mpaka Mafia, tusubiri wakati ni muda
 
Ni mwekezaji ..poor tz
 
Mimi ni UVCCM, nasemaje CCM OYEEE...Sisi tunaupiga Mwingi
Teh teh teh...
 
Unaongea lugha ya mwaka 1970 wakati wa Ujamaa,mabepari wameshika mpini hivi sasa hata ndani ya nyumba yako unachimba sharti mkono wa birika uwe unatoa.
Hakuna hicho. Hizi ni taharuki tu mnaleta. Kwanza huyo Mwiba Holdings yupo Tanzania zaidi ya miaka 10. Huko Maswa ana vitega uchumi vyake
 


Tanzania ni nyumbani kwa moja ya hifadhi bora za wanyama barani Afrika, ambayo inafanya iwe sehemu ambayo inapenda kutembelewa sana na watu wengi ulimwenguni, lakini kisichojulikana ni kuwa kuna hifadhi ya wanyama ya Mwiba ambayo inamilikiwa kibinafsi na bilionea Mmarekani.

Mmiliki wa hifadhi hiyo anajulikana kama Bilionea Dan Friedkin, ambaye makao yake makuu yako Texas, ni Mwenyekiti wa Gulf States Toyota.


Bilionea Dan Friedkin

Kulingana na makala ya Forbes, mfuko wa familia yake, Friedkin Conservation Fund (friedkinfund.org), unashiriki kikamilifu katika uhifadhi wa Afrika Mashariki na umekodisha ekari milioni 6 za eneo la pori la Tanzania kwa lengo la kulilinda.

Haijulikani bilionea alilipa kiasi gani kuipata hazina hii, lakini inasemekana kuwa hifadhi hiyo ilifanywa kuwa ya binafsi mwaka 2009.

Mwiba, ambayo inaenea zaidi ya ekari 125,000, inapakana na mpaka wa Magharibi wa eneo la uhifadhi la Ngorongoro na sehemu ya Kusini ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Uhamaji wa nyumbu wa Serengeti hupita kupitia Mwiba kati ya Desemba na Aprili. Ikiwa na vilima virefu, msitu mnene, mashimo ya maji na mito (iliyokauka) ambapo mabwawa hutokea, maji yake ya kudumu huvutia wanyama pori mwaka mzima.

Wageni ambao wamewahi kufika Mwiba wanasema ni kama sumaku ya wanyama wakati sehemu ya Kusini ya Serengeti na maeneo ya Hifadhi ya Ngorongoro yanakauka kati ya Julai na Novemba kila mwaka.

Kulingana na Friedkin, Logde ya Mwiba, ambayo gharama yake ni dola za Kimarekani 1,800 (Milioni nne na ushee za Kitanzania) kwa mtu, ilijengwa ili kuwa na uwepo unaofanana na mandhari ya sehemu hiyo.

"Utekelezaji wa muundo ulikuwa jitihada ya pamoja, lakini mke wangu, Debra, ndiye anayepewa sifa zote kwa wazo kumbukumbu tuliotaka kuwapa wageni wetu," anasema.

The Citizen
 
Nafikiri ni wawekezaji tu sidhani kama ni wamiliki wa ardhi hiyo kwa kuwa sheria yetu ya ardhi bado hairuhusu ardhi kumilikiwa na mgeni bali mwekezaji tu kwa masharti.
Ndugu yangu we acha tu, kwa akili ya lawaida ni kweli haiwezekani ila ukifuatilia utashangaa utakapokutana nayo, " wapo wageni wamemilikishwa ardhi" ushahidi ninao hasa kwa wenye pesa zao!.

Sent from my SM-A235F using JamiiForums mobile app
 
Duh
 
Wewe toa toa mimacho. Nunua na wewe ardhi.
 
Nafikiri ni wawekezaji tu sidhani kama ni wamiliki wa ardhi hiyo kwa kuwa sheria yetu ya ardhi bado hairuhusu ardhi kumilikiwa na mgeni bali mwekezaji tu kwa masharti.
Sheria zenyewe zinafuatwa sasa[emoji23]
 
Nashukuru Mbowe kuitaja tena, huyu Dan Friedkin ni mmoja bila kupepesa.macho alie fadhili Royol Tour ya Mama na mshahara wake ndio ulikuwa kumegewa Hakari zio Million 1+.

Nchi inauzwa kwa Waarabu na Wazungu, sasa kuna wapumbavu na zile elimu zao kila kitu wanaingiza Udini.

 
Duh!
Kweli awamu hii imeamuwa kuimaliza TANGANYIKA MPAKA MIFUPA! KHAAA!
😠😡🤬
 
Kuna wajinga walishabikia ufadhili wa royol tour wakidhani ni wajomba zetu wanaweza kutoa fedha yao bure. Now we are all paying the price!! Kasi ya kumega mapande ya ardhi na raslimali nyingine za nchi na kuwauzia wageni kwa mikataba isiyoeleweka, imekuwa kubwa sana ktk utawala huu. Sijuhi wenzetu wanaochukulia haya mambo kishabiki, uwe ushabiki wa kidini au kisiasa, wote tumepanda boti hiihii tutazama pamoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…