KERO Danadana za Serikali kwenye kuanza kutumika kwa Treni ya SGR kipande cha Dar - Moro, nini kinaendelea pande hizo?

KERO Danadana za Serikali kwenye kuanza kutumika kwa Treni ya SGR kipande cha Dar - Moro, nini kinaendelea pande hizo?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
SGR na Stiglers ni White elephants
Na hicho ndicho mnataka kitokee..."mtamezwa wabichi" ohoo.!!

Mradi ili uweze kuhitimu kuwa white elephant lazima ukamilike kwa viwango vinavyotakiwa kisha Mradi huo ushindwe kupata wateja wa huduma yake hiyo.

Kamilisheni miradi hiyo bila hujuma yoyote ya kuiba sementi na nondo kwa viwango vinavyotakiwa na ianze kutoa huduma kisha tuone Wanaohitaji hiyo huduma kama wataisusa.
 
Vision and mission holder wa ujenzi wa SGR amekufa na Hilo lilitegemewa sana kutokea

Ule wasiwasi wa Watanzania juu ya mwendelezo wa miradi aliyoianzisha kwa momentum kubwa na ujasiri wa ajabu mategemeo yetu baada ya kufa kwake ni kukosekana kwa maajabu hasa baada ya mbeba mamlaka kukiri mwenyewe kuwa viatu ni oversized kwake.

Kuingiliwa na wezi ndani ya msafara ambao hawawezi kuhusu nalo linachangia haya yanayoendelea maana ukitaka kujua mradi huu ulimuhitaji sana JPM ili ukamilike angalia gharama za vipande walivyosaini wahuni ikoje. Almost double the cost ambazo JPM aliziacha.

Sasa basi ili kuprove kuwa they are right to their double cost wamemamua kumkwamisha mkandarasi na mpaka tunahofia ataondoka ili watu wafanye waliyazoea.

Tumwombee Sara Rais Samia Mungu aendelee kumjalia kupata wasaidizi wenye MWANGA na Nia ya kweli ya kuongoza nchi ifike mahala inatakiwa kuwa. Tumeshihudia MWANGA huo siku za karibuni na tumeanza kupata matumaini SAsa kwamba mambo huenda yatabadilika tofauti na miaka hii miwili ambayo wanyang'anyi wamekuwa wakijifanyia wanavyotaka.
 
Ujenzi wa reli hii ya kisasa kwa awamu ya kwanza kati ya Dar es salaam - Morogoro (Km 300), ulizinduliwa na Rais wa awamu ya tano, John Pombe Magufuli Aprili 12, 2017. Ilielezwa ujenzi wa mradi huu ungekamilika ndani ya miezi 30 mpaka kufikia Novemba 2019, haikuwezekana.

Uliongezwa muda wa miezi 18 mpaka Aprili 2021, ikashindikana pia. Aliyekuwa waziri wa Ujenzi wakati huo, Leonard Chamuriho akaeleza reli hiyo ingeanza kufanya kazi ndani ya miezi minne, yaani Agosti 2021, ikashindikana tena.

Maelezo zaidi yakaonesha ingeanza kufanya kazi Disemba 2021, na waziri wa ujenzi na uchukuzi, Makame Mbarawa wakati akieleza mafanikio ya miaka 60 ya sekta ujenzi na uchukuzi.

Januari 17, 2022 Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Gerson Msigwa akaeleza awamu ya kwanza ya kipande cha Dar es Salaam-Morogoro utakamilika na majaribio yataanza April, 2022.

September 2022, Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Atupele Mwakibete, alisema Treni ya umeme kutoka Dar es Salaam, hadi Morogoro itaanza kufanya kazi rasmi mwezi Februari 2023, kwani vichwa vya Treni, mabehewa ya abiria na mizigo yanatarajiwa kufika nchini mwezi Novemba.

Mei 2023, Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ilisema imepokea mabehewa sita ya reli ya kisasa ya (SGR) ambayo yamewasili kutoka nchini Ujerumani tayari kwa kuanza majaribio Juni 2023.

Kimya kizito mpaka sasa, kwani nini kinaendelea huko?
Wanangoja bwawa la Mwalimu Nyerere likamilike upatikane umeme usio wa jenerata ya Maharage yenye Makambakamba!
 
Back
Top Bottom