Dancer wa Wasafi "Bajuni" aachana na kazi ya kucheza mziki rasmi

Mhaya

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2023
Posts
1,831
Reaction score
5,489
Aliyekuwa Dancer wa Wasafi chini ya Diamond Platnumz, Bajuni H. Bajuni ametangaza gafla kuachana na kazi iliyompa umaarufu ya kucheza mziki katika Shows na Video za mziki.

Ameandika kuwa leo ameamua kuachana na kazi hiyo ambayo amekuwa akiifanya kwa muda mrefu toka utotoni na mpaka sasa amepita vingi kama dharau na mafanikio ndani yake, anaongezea kusema Umri sio rafiki, majukumu yanamuandama hivyo mwisho akatoa shukrani za dhati kwa mashabiki na kwa MUNGU. Na kuhitimisha hivyo.



Your browser is not able to display this video.

 
Madansa ni kama wahudumu wa salon za kiume hawakaagi

Sema bajuni na mose iyobo wamekaa sana.

Tangu diamond anaanza anza yupo nao.

Miaka zaidi ya 10 wamekaa na diamond..

Nahisi amepata hasira kuona Diamond ametajirika ila wao wanabaki vile vile na umaskini wao, wanaishia kupata hela ya kula na kodi tu ya kuishi vijumba vya kupanga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…