Dangote Cement penetrates giant Kenyan Cement Market

Dangote Cement penetrates giant Kenyan Cement Market

Viongozi waliposema tanzania ya viwanda walimaanisha viwanda vya wagonga nyundo kama sido. Sasa nyie mnawasuprise na likiwanda lenu kubwa hivyo unategemea nini. Lifungeni bana
Umenifanya nicheke bila kufungua kinywa maana sijaswaki bado.
Ningefungua kinywa mbu wangekufa.
 
Kuna tabia ya waTanzania kupenda kuiponda serekali yao bila hata kuujua ukweli,ilimradi tu awe ametoa kashifa kwa nchi yake na kuisifia ya pembeni,ni kawaida kabisa kwa waTanzania,kila ukifika vijiweni,kwenye mkusanyiko wa watu kidogo utakuta raia wanasema vibaya tu kwa kila kitu hata kama kuna jema hawalioni,hapa wewe ndugu hata unaweza usijue undani wa huyo Dangote alitaka yamkini kutubadilikiaje,ogopa sana ukiwa na watoto wa kike nyumbani kwako afu anaibuka tu jamaa anasema ataweka ofc ili watoto wako wapate ajira pia,kuna siku utajuta na utatamani kumfukuza lakini atakua keshazalisha watoto wako wote na hauwezi mfukuza kwa kua wajukuu zako watalelewa na nani.
UNA HEKIMA SANA . ..UBARIKIWE SANA . ........anaye chukia kwao MTUMWA
 
Viongozi waliposema tanzania ya viwanda walimaanisha viwanda vya wagonga nyundo kama sido. Sasa nyie mnawasuprise na likiwanda lenu kubwa hivyo unategemea nini. Lifungeni bana
Hata kàma ni nchi ya viwanda, kumbuka kwamba tunatakiwa kureview mikata yote, ili ikae kimaslahi zaidi, co kwa kuwa aliahidiwa kupewa gesi ya bure wakati huo, je cc ni kwa ajili ya kumnufaisha yy? kama hawezi andoke, na huko Kenya ndo alitaka kujenga hiki kiwanda kabla na baadae kuamua kukijenga hapa tz na kama pia kaamua kurudi Kenya bado sio mbaya, inawezekana ndo namna ya uwekezaji wake huo.
 
Hii ndio shida ya kuwapa watu uongozi wa mambo ya biashara wakati ajawai kumiliki kibanda cha kuuza nyanya.
 
Hata kàma ni nchi ya viwanda, kumbuka kwamba tunatakiwa kureview mikata yote, ili ikae kimaslahi zaidi, co kwa kuwa aliahidiwa kupewa gesi ya bure wakati huo, je cc ni kwa ajili ya kumnufaisha yy? kama hawezi andoke, na huko Kenya ndo alitaka kujenga hiki kiwanda kabla na baadae kuamua kukijenga hapa tz na kama pia kaamua kurudi Kenya bado sio mbaya, inawezekana ndo namna ya uwekezaji wake huo.

Usiandike usichokijua,umesoma taarifa ya TPDC?
 
Watu mnapenda sana kuabudu wawekezaji. Yaani mnaona demand zao ni za msingi kuliko maslahi ya taifa. Haohao tena mnakuja kuanza kuponda kwamba serikali inaingia mikataba inayowanufaisha zaidi wawekezaji kuliko taifa. Hizi mindset za namna hii hazitalijenga taifa hata kidogo. Lazima tufike mahali tukubali kuweka maslahi ya taifa kwanza kuliko kukubaliana na kila anachokitaka mwekezaji. Tulishafanya makosa kwenye madini hatuwezi tena kurudia makosa kwa wawekezaji wapya eti kisa tu wataenda nchi jirani. Bora tubaki na umaskini wetu pamoja na natural resources zetu kuliko kushangilia umati wa wawekezaji wasiokuwa na faida pana kwa taifa.
 
Kuna tabia ya waTanzania kupenda kuiponda serekali yao bila hata kuujua ukweli,ilimradi tu awe ametoa kashifa kwa nchi yake na kuisifia ya pembeni,ni kawaida kabisa kwa waTanzania,kila ukifika vijiweni,kwenye mkusanyiko wa watu kidogo utakuta raia wanasema vibaya tu kwa kila kitu hata kama kuna jema hawalioni,hapa wewe ndugu hata unaweza usijue undani wa huyo Dangote alitaka yamkini kutubadilikiaje,ogopa sana ukiwa na watoto wa kike nyumbani kwako afu anaibuka tu jamaa anasema ataweka ofc ili watoto wako wapate ajira pia,kuna siku utajuta na utatamani kumfukuza lakini atakua keshazalisha watoto wako wote na hauwezi mfukuza kwa kua wajukuu zako watalelewa na nani.
Kuna uzi humu una sound clip ya mfanyakazi mmojawapo wa Dangote.
Maelezo yake yanaonesha serikali hii imekiuka makubaliano
Order za makaa ya mawe zinacheleshwa na tani hutolewa kidogo kidogo wakati kiwanda kinahitaji tani nyingi kwa wakati mmoja.
Ninaamini huo ndo ukweli maana waziri mmoja aliongea jambo kuhusu Dangote halafu siku iliyofuata akasema alificha baadhi ya taarifa(Dangote alitaka apewe gesi bure).
Kwangu huu ni uongo mkubwa.
Ametujicha mangapi?
Je, hajaficha habari zingine kweli?
Viongozi wa TZ wanasahau kuwa nyuma ya mwekezaji mmoja, kuna wawekezaji saba. Kushabikia mwekezaji mmoja kuondoka ni kushangilia na hao wengine kuondoka kwao.

Nagu alieleza kuwa lengo la kumleta Dangote ni kudhibiti mfumko wa bei ya saruji ambayo ilikuwa inapangwa na kikundi cha wazalishaji wa saruji. Dangote alitakiwa ajipangie bei yake (kutokana na uhalisia)
Watanzania ni mashahidi. Wengi tumejenga na saruji ya Dangote.
Iasemekana kuna fitina ya wazalishaji wa saruji ambao ni wahanga ktk ushindani wa soko la saruji. Ndo maana walishangilia sana ktk mkutano na waziri(ambao Dangote hakwenda) walipoambiwa wanatakiwa kununua makaa ya mawe nchini.
Kama sijaeleweka nisamehe mkuu maana hata mi sielewi hii movie.
Tafakari
 
Hili sakata la Dangote ni kielelezo tu kuwa kama taifa hatujajipanga kwa kwa ajili ya kupata maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Hakuna nchi iliyopata maendeleo endelevu ya kiuchumi bila kuwa na taasisi huru na imara za kiuchumi na za kisiasa.

Tanzania haitaweza kwenda kokote kiuchuni chini ya katiba iliyopo. Badala ya kuweka taasisi huru na zenye nguvu za kiutawala, katiba yetu inamfanya rais kuwa kila kitu; halazimiki kukubali ushauri wowote kutoka kwa mtu yeyote na kwa hivyo inampa "leeway" ya kuendesha nchi kwa utashi wake tu! Nilishawahi kusema tena hapa JF kuwa kinyume na watu wengi wanavyoamini, urais wa JMT siyo taasisi bali ni utashi wa anayekalia kiti cha urais.

Katika mazingira haya, nchi ikiwa na rais mwenye weledi mdogo wa mambo ya kiuchumi na kijamii au anayefanya maamuzi kwa kuzingatia hisia zake tu inakuwa ni janga. Kama kwa mfano, kama rais anahisi tu kuwa kuna "dili" za watu katika mradi wa kiwanda cha Dangote, basi hiyo pekee inatosha kusabababisha sintofahamu iliyotokea. Hii inahushisha pia matumizi ya sheria kiupendeleo kwa kulenga "maadui wa kisiasa" kama ilivyoyokea kwa Mbowe kufurumushwa Billicanas ilhali wadaiwa wengine wa NHC wanaendelea kupeta; na Sumaye kunyang'anywa shamba ilhali kuna maelfu kwa maelfu wengine wenye mashamba tena kwa muda mrefu zaidi hawajaendeleza na hawajaguswa!

Habari kama hizi zimeripotiwa sana na vyombo vya kimataifa. Je ni ujumbe gani unapelekwa kwa wawekezaji watarajiwa (potential investors)? Kwamba Tanzania ni nchi hatari kwa uwekezaji kwa sababu inaendeshwa "arbitrarily". But this is self-inflicted damage!

Katiba iliyopo haifai pia kwa sababu inazalisha watawala wasiofaa na wasio na uzalendo kwa sababu ya kukosekana kwa taasisi huru na imara za kisiasa.
Kinachosikitisha ni kuona awamu ya nne ilijitolea kuandaa Katiba mpya, lakini wahafidhina wakampotosha kiongozi na kuleta Inayopendekezwa yenye mambo yaleyale ya kizamani. Ama kwa hakika Maoni ya Wananchi ambayo Jaji Warioba waliyakusanya, yalikua na mambo mazuri sana kwa mustakabali wa nchi, lakini looo, tumebaki palepale.
 
Back
Top Bottom